Mshambuliaji wa klabu ya Juventus Cristiano Ronaldo jana amekabidhiwa tuzo yake ya kuwa Mchezaji Bora wa mwaka katika Ligi Kuu Nchini Italia “Serie A” msimu huu uliomalizika.
.
Nyota huyo amekuwa Mchezaji wa kwanza katika Historia kushinda tuzo ya Mchezaji bora wa mwaka katika Ligi kuu tatu tofauti Kati ya Ligi kubwa tano Barani Ulaya..
VIDEO: SIMBA SC ILIVYOTUA DODOMA
Kikosi kimefika salama Dodoma na sasa kinaanza safari kwa basi kwenda Singida. #NguvuMoja #SportPesaChallenge #TukutaneMei23
TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO JUMATATU
TETESI ZA USAJILI YANGA LEO JUMATATU
Kikosi cha Simba kimeondoka jijini Dar es salaam leo Jumatatu kuelekea mkoani Singida
Kikosi cha Simba kimeondoka jijini Dar es salaam leo Jumatatu kuelekea mkoani Singida tayari kwa mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Singida United
Simba imetumia usafiri wa Ndege hadi mkoani Dodoma ambapo kutoka Dodoma itasafiri kwa basi mpaka Singida
Mchezo dhidi ya Singida United utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa Namfua

YASOME HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU YA MAY 20,2019
Mchakato wa Usajili wa Mkambo Uko Mikono Salama -MWAKALEBELA
Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amesema mchakato wa usajili wa mshambuliaji Heritier Makambo uko katika mikono salama
Aidha Mwakalebelea amesema Yanga imepokea ofa nyingi zinazomuhusu mshambuliaji huyo
Amesisitiza bado hakuna mkataba uliosainiwa upande wa Yanga, hivyo amewahakikishia Wanayanga kuwa Makambo bado ni mchezaji wao halali
“Suala la Makambo liko mikono salama, uongozi tunalifahamu na tulitoa baraka zetu kwake pamoja na Mwalimu kwenda Guinea ambako alitakiwa kwenda kufanyiwa vipimo vya afya,” amesema
“Ilikuwa ni lazima aende na Mwalimu kwa sababu kule wanaongea kifaransa”
“Lakini ifahamike Makambo ana ofa nyingi, sio Horoya Fc pekee wanaotaka kumsajili, Jumatatu tutakutana na wengine”
“Tunazipitia ofa zote na kufanya tathmini kabla ya kuamua. Hakuna mkataba ambao umeshasainiwa kwa upende wetu. Na kwa kawaida mkataba lazima uwe wa pande mbili”
“Mpira ni biashara, kama kutakuwa na ofa nzuri tutafanya biashara lakini kama itakuwa tofauti basi tutaendelea kubaki na mchezaji wetu”
Dk Msolla Atangaza kusaka kocha msaidizi – YANGA
Habari njema kwa Wanajangwani ni kuwa uongozi wa Yanga umetangaza kuanza mchakato wa kutafuta kocha Msaidizi Mzawa ambaye atasaidiana na kocha Mwinyi Zahera kukinoa kikosi cha Yanga
Tangu alipoanza kazi mwishoni mwa msimu uliopita, kocha Zahera hakuwa na Msaidizi zaidi ya Noel Mwandila ambaye amekuwa akikaimu nafasi hiyo licha ya kuajiriwa Yanga kama kocha mtaalamu wa viungo
Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshondo Msolla ambaye kitaalam ni kocha, amesema kuna umuhimu kwa benchi la Ufundi kuongezewa nguvu kwa kuajiri kocha Msaidizi mzawa ambaye atakuwa sambamba na Zahera
“Benchi la ufundi linahitaji kuwa na kocha msaidizi mwenye kiwango kizuri ili kuongeza nguvu ndani ya kikosi chetu, tutaangalia zaidi kocha mzawa ili aweze kuwa sambamba na kocha Zahera kufanya kazi,” amesema
Vincent Kompany anarejea Nchini kwao Ubeligiji kwenye Klabu yake ya zamani Anderlecht
Nahodha wa Man City Vincent Kompany anarejea Nchini kwao Ubeligiji kwenye Klabu yake ya zamani Anderlecht anaenda kuwa Kocha Mchezaji.
SIMBA 2-0 NDANDA FC
Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wanahesabu siku za kukabidhiwa ubingwa wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Ndanda Fc mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru
Wakicheza kandanda la pasi fupifupi lililojaa ufundi wa hapa na pale, Simba ilijipatia mabao yake yote mawili kwenye kipindi cha kwanza yote yakiwekwa kambani na Meddie Kagere ‘MK14’


Ushindi huo umeifanya Simba ifikishe alama 88 na kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama tano dhidi ya Yanga inayoshika nafasi ya pili ikiwa na alama 83
Yanga imebaki na michezo miwili, inahitaji kushinda yote ili kuweza kuipiku Simba lakini wakati huohuo Simba bado ina michezo mitatu mkononi
Ni muujiza pekee ambao utaifanya Simba isiweze kutwaa ubingwa!
Aidha Simba inaweza kwenda kumaliza ‘shughuli’ mkoani Singida keshokutwa itakapoivaa Singida United
Kwenye mchezo huo Simba inahitaji alama moja tu kuweza kurejea na ubingwa jijini Dar es salaam
Kinara wa mabao Meddei Kagere amezidi kujiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa kiatu cha dhahabu baada ya leo kufikisha mabao 22
Kagere anaongoza kwa tofauti ya mabao sita dhidi ya Heritier Makambo na SalimAiyee ambao wote wana mabao 16





























