AISHI MANULA Aipania SEVILLA

Mlinda lango wa Simba Aishi Manula amesema mchezo dhidi ya Sevilla una maana kubwa kwa wachezaji wa timu hiyo kwani watakuwa na nafasi ya kuonyeshwa ukubwa wa timu yao

“Simba kucheza na Sevilla ndani ya uwanja wa Taifa ni jambo kubwa sana,” amesema

“Kwetu sisi wachezaji ni nafasi kubwa sana kuonyesha ubora wetu na kutimiza malengo ya timu yetu ambayo ni kufanya vizuri Kimataifa”

“Nawaalika mashabiki waje kwa wingi uwanja wa Taifa May 23 kuipa sapoti SImba, kuipa sapoti Tanzania”

Simba na Sevilla zitachuana Alhamisi, May 23 katika mchezo wa ‘kukata na shoka’ utakaopigwa uwanja wa Taifa kuanzia saa moja kamili jioni

HIKI HAPA KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHO CHEZA LEO DHIDI YA NDANDA FC

Kikosi cha Simba dhidi ya Ndanda leo

  1. Aishi Manula
  2. Zana Coulibaly
  3. Mohammed Hussein
  4. Yusuph Mlipili
  5. Erasto Nyoni
  6. Jonas Mkude
  7. Hassan Dilunga
  8. Haruna Niyonzima
  9. John Bocco
  10. Meddie Kagere
  11. Clatous Chama
WACHEZAJI WA AKIBA
  1. Deo Munishi
  2. Nicolas Gyan
  3. Pascal Wawa
  4. James Kotei
  5. Mzamiru Yassin
  6. Adam Salamba
  7. Rashid Juma

Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu nchini Italia “Serie A” kwa msimu 2018/19

✍🏼 Mshambuliaji wa Klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu nchini Italia “Serie A” kwa msimu 2018/19, Cr7 ametwaa tuzo hii ikiwa ni msimu wake wa kwanza tu kusakata soka nchini Italia.
:
✍🏼 Ronaldo alikuwa sehemu ya kikosi cha Vibibi hivyo vya Turin kwenye kutwaa Scudetto yao ya nane mfululizo huku Cr7 ikiwa ni ya kwanza kwake na yeye mwenyewe akipachika Mabao yake 21 katika Ligi. Tuzo za Serie A kila mshindi anapewa baada ya kumalizika kwa msimu, lakini Ronaldo atapewa tuzo yake kabla ya mchezo wao dhidi ya Atalanta siku ya leo Jumapili.
:
✍🏼 Wachezaji wengine waliotwaa tuzo katika Ligi hiyo ni, Mlinda lango Bora wa Msimu katokea Inter Milan, Samir Handanovic, Beki Bora wa Msimu imebebwa na Muafrika kutoka Senegal, Kalidou Koulibaly anaekipiga Napoli, Kiungo Bora Ligi Kuu Italia imebebwa na fundi wa kumiliki Dimba La Kati, Sergej Milinkovic-Savic kutoka Klabu ya Lazio, Fabio Quagliarella Mshambuliaji hatari wa Sampdoria kabeba tuzo ya Mshambuliaji bora wa msimu na Nicolo Zaniola kinda ambaye anacheza Klabu ya AS Roma, yeye kaibuka Mchezaji bora kijana wa Mwaka ndani ya Serie A.
:
✍🏼 Ronaldo Sasa katwaa tuzo ya Mchezaji bora wa mwaka Italia, England na Hispania pamoja na kutwaa Ubingwa wa Ligi kwa nchi zote tatu.. Koulibaly amekuwa nguzo ya ulinzi ndani ya Napoli blocks 31, Clearance 125, tackles won 60 Kati ya 67, clean sheets 13 katika mechi 31 alizocheza..
#seriea #juventus #napoli #lazio #asroma
@Sokawaytz

HARUNA NIYONZIMA NI MZURI KULIKO CHAMA – Mwl KASHASHA

Mwalimu kashasha katika Sehemu ya tanoya Uchambuzi wake
@mwalimu_alex_kashasha

Mchambuzi wa soka Nchini Tanzania Mwalimu Kashasha amesema kuwa watanzania wakua chanzo cha wachezaji wengi kucheza na Majukwaa

Huku akimsfia niyonzima kuwa hatakama anacheza na Majukwaa ila bado anaspeed katika mpira wake, kashasha amesema kwake yeye Haruna ni Mzuri kuliko chama

Anasema kuwa Haruna Kwa sasa amebadilila na amkua msaada kwa timu kutokan na Uchezaji wake

Usikose Mwendelezo wa Uchambuzi wa Mwalimu kashasha katika Sehemu ya Sita.

Powered By @bikotanzania
Imeandaliwa na @officialchristz video kwa hisani ya @globalpublishers

ZAHERA APEWA MAJUKUMU HAYA YANGA

Katika kuhakikisha timu zote za Yanga zinakuwa imara, uongozi wa timu hiyo umemtangaza Mwinyi Zahera kuwa msimamizi Mkuu wa timu zote

Akizungumza kwenye hafla ya Iftar Gala Dinner iliyofanyika Hotel ya Serena jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo, Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshindo Msolla amesema Zahera ambaye ni kocha wa kikosi cha kwanza, pia atasimamia timu ya Vijana (Yanga B) na timu ya Wanawake (Yanga Princess)

“Kwa sababu ya masuala ya ufundi, natangaza mbele yenu, timu zote zitakuwa chini ya kocha Mwinyi Zahera,” alisema Dk Msolla

“Ni lazima kama timu tuwe na filosofia moja. Hivyo tumeona filosofia inayotumiwa kwenye kikosi cha kwanza ni lazima ikafuatwa na makundi yote. Zahera atakuwa msimamizi Mkuu”

ASISITIZA KUVUNJWA MAKUNDI

Dk Msolla amewataka Wanayanga kudumisha umoja ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea

Aidha amesema ahadi walizotoa wakati wa kampeni watazitimiza ambapo ameahidi kushirikiana na waliokuwa wagombea wengine wa nafasi mbalimbali lakini bahati mbaya kura hazikutosha

“La kwanza lilikuwa kuleta mshikamano na kuirudisha timu kwa Wananchi”

“La pili lilikuwa kubadilisha mfumo na uendeshaji wa timu. Nawaahidi mbele yenu hili tutalifanya ndani ya mwaka mmoja au chini ya hapo”

“La tatu muhimu tutasaidia miradi inayoendelea klabuni sasa ambayo ni ujenzi wa uwanja, ukarabati wa jengo na miradi mipya”

“Nafurahi Igangula hapa amesema yuko tayari kutoa ushirikiano, niliona randama yake wakati wa kampeni, nawaahidi tutashirikiana nae na tutahakikisha atakuwa sehemu ya uongozi wetu”

“Dk Tiboroha ameshindwa kufika hapa kutokana na kuchelewa kutoka safarini Arusha lakini ameahidi kuchangia Tsh Milioni Moja kwa ajili ya shughuli mbalimbali za klabu, na yeye tuko nae pamoja”

“Muhimu nimeomba sote tuvunje makundi yetu baada ya uchaguzi. Umoja na Ushirikiano wetu utatusaidia kusonga mbele kwa haraka”

UTAWALA BORA

Dk Msolla amesema katika uongozi wake watahakikisha wanafuata utawala bora na watakuwa makini katika usimamizi wa fedha

“Maeneo ya ukaguzi wa ndani na nje tutakuwa wakali sana. Tutakuwa tayari kutumia gharama kuwapata wakaguzi wanaoheshimika Kimataifa na tutakuwa tukitoa ripoti wazi kwenye vyombo vya habari kuhusu mapato na matumizi ya klabu kama zinavyofanya taasisi nyingine”

KUIMARISHA KIKOSI CHA YANGA

Dk Msolla amesema kwa ushirikiano ulioonyeshwa na makundi mbalimbali ya Yanga, ndani ya wiki mbili au tatu, zoezi la kukiboresha kikosi litakuwa limeanza

“Nawaahidi ndani ya wiki mbili au tatu zijazo, tutaanza kutengeneza kikosi imara chini ya usimamizi wa kocha Mwinyi Zahera”

SIMBA Kusaka Ushindi Leo Dhidi ya Ndanda FC

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba leo wanashuka uwanja wa Uhuru kuikabili Ndanda Fc katika mchezo ambao matokeo ya ushindi yataisogeza Simba karibu ya ubingwa wa pili mfululizo

Simba inayoongoza ligi ikiwa na alama 85, inahitaji alama nne tu kutetea ubingwa kwa msimu wa pili

Kuhakikisha alama tatu zinapatikana leo, kikosi cha Simba kiliingia kambini juzi baada ya kufanya kikao na Mwekezaji wa klabu hiyo Bilionea Mohammed Dewji ‘Mo’

Hesabu za kocha Patrick Aussems ni kuhakikisha wanashinda mchezo wa leo na ule utakaofuata dhidi ya Singida United ili kujihakikishia ubingwa kabla ya mechi mbili za mwisho

Baada ya mchezo leo, Simba itaondoka jijini Dar es salaam kuelekea Singida ambako keshokutwa Jumanne, May 21 itacheza na Singida United

May 22 Simba itafunga safari kurejea jijini Dar es salaam ambapo May 23 inakabiliwa na mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sevilla

Sevilla inatarajiwa kuwasili keshokutwa tayari kwa mchezo huo ambao utalipaisha jina la Simba na Tanzania Kimataifa kwani utarushwa ‘mbashara’ na vituo vikubwa vya runinga duniani

Kuelekea mchezo wa leo, Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema wachezaji wa timu hiyo wako tayari, wanafahamu Wanamsimbazi wanahitaji ushindi

MAKAMBO : Kawapa Somo Wachezaji Wa YANGA SC

Kuna wakati kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera alifichua kuwa mshambuliaji Heritier Makambo alifukuzwa Hotelini alikokuwa amepanga kutokana na uongozi wa Yanga kushindwa kulipa kodi ya pango

Makambo alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Yanga wenye madai ya fedha za mishahara hadi miezi minne achilia mbali malimbikizo ya bonasi na fedha za usajili

Lakini changamoto hizo hazikumuondoa katika majukumu yake, alijituma kwa moyo mmoja kuhakikisha Yanga inafanya vizuri

Dili nono alilopata klabu ya Horoya AC ni matunda ya uvumilivu na kujituma kwake katika klabu ya Yanga

Hili ni somo kwa wachezaji wengine Yanga hasa wale wenye malengo ya kufika mbali

Migomo na ‘kususa’ kucheza haviwezi kuwasaidia kufikia malengo hayo

Nakumbuka mwanzoni mwa msimu Zahera alikaa na wachezaji wote na kuwaeleza umuhimu wa wao kuifanya kazi kwa bidii bila ya kujali changamoto zinazowakabili

Bila shaka hawa akina Makambo walimuelewa vizuri na ndio maana walifanya kazi kwa bidii, leo wameona matunda yake

Wachezaji wa Kitanzania wajenge utamaduni wa kuwa na malengo ya kufika mbali

Leo hii ukimuangalia Beno Kakolanya alichokipata baada ya kuigomea Yanga utamsikitikia tu

Kama Beno angeendelea kucheza Yanga pengine leo angekuwa kipa namba moja wa kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’

Beno aliigomea Yanga wakati kiwango chake kikiwa juu sana na tayari alishaitwa kikosi cha timu ya Taifa

Angecheza michuano ya AFCON 2019 na kuwa na nafasi kubwa ya kuonekana Kimataifa na kujiongezea nafasi ya kupata timu nje ya nchi

Hawa akina Makambo wawe somo kwa wachezaji wetu.

Wawe makini katika kufanya maamuzi, wajitambue, wawe wavumilivu na kuwa na malengo ya kufika mbali

Muhimu zaidi watafute Wasimamizi ambao wanaweza kuwasaidia kufikia malengo yao