FIFA yapiga Marufuku LALIGA kuchezwa USA

FIFA yapiga marufuku La Liga kuchezwa USA
:
Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limeikatalia La Liga ombi la kutoa kibali ili baadhi ya michezo ya ligi kuchezwa nchini Marekani na kusisitiza mechi za ligi ya ndani lazima zichezwe ndani ya mipaka ya nchi husika. :
Kamati ya FIFA imekutana leo Ijumaa kuzungumzia juu ya maombi ya La Liga yaliyowasilishwa na Rais wa La Liga Javier Tebas. :
La Liga walikuwa wanataka mchezo wa Girona vs Barcelona wa tarehe 26, January uchezwe Miami. Hatua hii ilikuja baada ya La Liga kusaini mkataba wa miaka 15 na kampuni ya Relevent Sports ya US.
:
“Nalipinga jambo hili kwa nguvu zote, na nawanyima kibali cha mchezo Girona vs Barca kuchezwa Miami.” – alisema Rais wa FIFA Gianni Infantino.
“Michezo rasmi ya ligi lazima ichezwe kwenye mipaka ya nchi husika, FIFA imeweka wazi uamuzi wake juu ya suala hili.”

MKATABA WA DDG UNAVYOWAUMIZA KICHWA MAN U

Mkataba wa DDG unavyowaumiza kichwa United – Juventus huenda wakamsaini buree.
:
:
Jose Mourinho amesema hana uhakika juu ya golikipa wake David De Gea kusaini mkataba mpya, DDG mkataba wake na United unaishia mwishoni mwa msimu ujao na taarifa mpya zinadai Juventus ambao wana uzoefu na kusajili wachezaji ‘huru’ wameanza kuvizia saini ya De Gea
.
.
Golikipa huyo mwenye miaka 27 mkataba wake wa sasa unaishia mwishoni mwa msimu wa 2019/20, na sasa inaonekana wazi kwamba Juventus wapo tayari kumsubiri amalizane na United na kumsaini bure kama ilivyokuwa kwa Paul Pogba mwaka 2012
.
.

De Gea amekuwa akitegemewa kusaini mkataba mpya na United kwa muda mrefu sasa tangu Thibaut Courtois alipojiunga na Real Madrid wakati wa kiangazi, lakini mpaka sasa hajasaini mkataba mpya na Mourinho leo amesema hana uhakika na kukamilika kwa dili jipya na United na taarifa mpya zinadai Juventus ambao wameshinda Serie A kwa miaka 7 mfululizo wapo katika nafasi nzuri ya kumshawishi DDG kuhamia Italia
.
.
Chanzo cha karibu na Manchester United kimesema: “De Gea amecheza dhidi ya waajiri wake wajao jumanne iliyopita. Endapo United hawatomuuza dirisha kubwa likifunguliwa, basi Juventus watasubiri mpaka mkataba wake umalizike.”
.
Inaelezwa DDG ambaye alishindwa kuhamia Madrid miaka 3 iliyopita kutokana fax machine ya Madrid kusumbua, ameshindwa kusaini mkataba mpya na United kwasababu anaona muelekeo wa klabu sio mzuri, umri wake unasogea na hakuna mafanikio ya maana aliyopata, hivyo sasa anaangalia machaguo tofauti kabla ya kuamua kukubali au kukataa kusaini mkataba mpya na United.
:
Juventus ambayo imetoka kumsaini Cristiano Ronaldo kwa dau la £99m wana utayari wa kuwalipa United ikiwa klabu hiyo itakubali kumuuza DDG, au watamsubiri mpaka mkataba wake umalizike na kumsaini bure ili aje kuziba pengo liloachwa wazi na Gigi Buffon aliyejiunga na PSG.
:
Katika miaka ya hivi karibuni, Juventus imefanikiwa kusajili bure wachezaji wakubwa ambao wameisadia kwa kiasi kikubwa kuirudisha katika listi ya vilabu bora duniani.
:
Wachezaji waliosajiliwa bure na Juventus
✅ 2009: Fabio Cannavaro
✅ 2011: Andrea Pirlo
✅ 2012: Paul Pogba
✅ 2013: Fernando Llorente
✅ 2014: Kingsley Coman
✅ 2015: Sami Khedira

SAMATTA AVUNJA REKODI GENK

SAMATTA KWENYE ORODHA YA WAFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE GENK

Katikati ya juma hili aliyekuwa mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani na Nyota wakimataifa wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta [Samagoal, The Champion boy] pamoja na mchezaji bora wa Afrika Mohamed Sallah [Egyptian King] wamefanikiwa kufikisha mabao 50 ndani ya vilabu vyao.

Mabao mawili ya @samagoal77 dhidi ya golikipa wa zamani wa Liverpool aliyewahi pia kucheza na Mo Sallah Karius yalitimiza idadi ya mabao 50 kwa Samatta. Samatta sasa anaingia kwenye kumbukumbu za wachezaji waliowahi kufunga mabao 50 katika historia ya klabu hiyo.

@mosalah ameweka rekodi ya kufunga mabao 50 ndani ya mechi chache zaidi ikiwa ni mechi 65 tu. Mo Salah sasa anakuwa mfungaji bora ndani ya Liverpool kutoka Afrika na anakuwa mfungaji bora namba 20 katika historia ya wafungaji bora Liverpool.

Mbwana Samatta amebakiza mabao 9 kufikia rekodi ya mfungaji bora namba 5 wa muda wote wa Genk. Samatta anashika namba 6 akiwa na mabao 50 na ndiye mchezaji pekee kutoka Afrika mwenye mabao mengi ndani ya Genk.

Samatta anaifukuzia rekodi ya baba yake Divock Origi, Mzee Mike Origi ambaye anashikilia rekodi ya mchezaji pekee kutoka afrika mashariki mwenye mabao mengi ndani ya ligi kuu Ubelgiji [33]. Samatta kufikia sasa ana mabao 24 tu ndani ya Ubelgiji.
Ikumbukwe pia Origi aliwahi kucheza Genk mwaka 1998 na alifunga mabao 20 katika michezo 80.

Kufikia hivi sasa Samatta msimu huu ndani ya ligi kuu amehusika katika magoli 11 michezo 8 [Magoli 9 na asisst 2]

Samatta msimu huu amehusika magoli 18 kwenye michezo 18. [Magoli 16 na assists 2]
. .
Kwa Ujumla Mpaka sasa Samatta amehusika mabao 63 katika michezo 130, [Mabao 50 na Asissts 13].
.
. 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿

CHELSEA NA ARSENAL JIPANGENI

KUNDI B:
CHELSEA NA ARSENAL MJIANDAE KUMPOKEA HARY KANE

Tottenham msimu UCL wanaelekea kupoteza dira. Wana alama 1 tu. Msimu uliopita katika michezo 6 walishinda 5 na kutoka sare mmoja. Tena walifanya maajabu kwa kumfunga Real Madrid aliyekwenda kutwaa ubingwa mabao matatu. Katika michezo 6, walishinda mabao matatu katika michezo minne.

Msimu huu katika michezo mitatu wanadaiwa mabao matatu. Wamefunga mabao matano wameruhusu manane. Aibu. Hili kundi bado ni gumu sana kwa Inter pamoja na Tottenham katika kupata nafasi ya kusonga mbele.

Tottenham mchezo ujao anakutana na PSV, Tottenham wanapaswa kushinda mchezo huo ili angalu wafikie alama 4. Inter anazo alama 6. Inter ana wakati mgumu kidogo kumfunga Barcelona akiwa kwake ingawa anahitaji hata sare. Inter kama watafungwa watabakiwa na alama zao 6 kama atashinda watapa alama 9 na hii itakuwa balaa zaidi kwa Tottenhan. Lakini faida kubwa waliona nayo Inter watawakaribisha PSV vibonde nyumbani. Hapo watahitaji alama 3 ili wafikishe alama 9. Wakati huo Tottenham atakuwa Camp Nou kama wakifanikiwa kutoka salama basi wakatoe sadaka.

Safari ya Tottenham kufuzu inatiwa dosari na shimo la Camp Nou. Mbaya zaidi Inter watawasubiri Barcelona Guissepe de Meazza kwa hiyo uwezekano wa kuambiwa sare upo. Faida pekee wanayotegemea Tottenham ni mchezo wao wa mwisho na Inter kwenye uwanja wao wa nyumbani. Kwa mawazo yangu Tottenham yupo kwenye wakati mgumu zaidi na bila shaka Chelsea na Arsenal wote kwa pamoja kwa mikono miwili wampokee ndugu yao kutoka London. Hivyo wajiandae kisaikolojia kumkaba Harry Kane.

#UCL Tottenham #hawatoboiii

UEFA : PSG wakiendea hivi Hawatoboi

KUNDI C:
PSG WAKIENDELEZA MPIRA WAO WA KUPAKA PODA HAWATOBOI

Liverpool alama 6, Napoli alama 5, PSG alama 4. Hivi Neymar ataficha wapi sura yake na pesa zote zile alizonunuliwa takribani Paund 222M kama ikitokea wametolewa hatua ya makundi?

Kama kuna kundi gumu mwaka huu basi hili kundi ni la kukata na shoka. Huyu Napoli kama Masikhara vile anaweza akashangaza wengi licha ya kutopewa nafasi kabisa. Tusishangae kuona hawa matajiri wakirudi mtaani kwao kucheza na watoto wenzao huko league 1.

Nahisi mchezo ufuatao wa Napoli na PSG ndio utakaotoa dira haswa kwamba tuendelee kusubiria mvua iishe au tutoke na mwamvuli.

Nafasi ya PSG kusonga mbele bado ipo, Nafasi ya Napoli vivyo hivyo, Liverpool ndo kwanza yupo kilele.

Mpaka sasa PSG na Barcelona ndio timu zilizofunga mabao mengi [10] kwa hiyo lolote laweza kutokea. PSG wana mchezo wa marudiano dhidi ya Liverpool pale Parc des princess nahisi kwa mchezo waliocheza mechi iliyopita kama hawatabadilika basi wanaweza kupigwa nje ndani, lakini Napoli watakaribishwa Anfield. Najiuliza hapa inawezekana Napoli wakatibua vibe lote la Majogoo pale Anfield kweli? Napoli mpaka sasa katika mechi 3 wamefunga mabao 3, bado kwa takwimu hizi ni ngumu sana kumwekea dhamana kupata ushindi pale Anfield kirahisi.
Mechi iliyobakiwa kwa PSG kukata tiketi ni Belgrade ambayo nina amini hata kama itachezwa Kinesi PSG atashinda sio chini ya bao 3.

Uwezekano wa yeyote kati ya Liverpool na PSG au Napoli kutolewa bado upo wazi hasa ukitazamia wote wamepishana alama 1 tu huku michezo ikibakia mitatu.. #UCL Ila hapa PSG wakiendeleza ubishoo #hawatoboiii

Arsenal 1-0 Sporting CP

#EUROPA2018/19

Arsenal wamefanikiwa kupata ushindi Ugenini wa bao 1 kwa 0 dhidi ya Sporting CP bao pekee la Danny Welbeck mnano dakika ya 77. .
.

Welbeck sasa anakuwa mchezaji wa kwanza wa Arsenal kuifunga timu ya Ureno ugenini ambaye jina lake la pili sio Campbell .
.
.
⚽ Danny Welbeck (2018/19)
⚽ Sol Campbell (2009/10)
⚽ Kevin Campbell (1991/92)

Samatta Azidi Kung’ara KRC GENK

SAMATTA Ameweka wavuni mara mbili na kutengeneza bao moja. Genk sasa wanaongoza kundi wakiwa na alama 6 baada ya kushinda michezo miwili na kupoteza mmoja. .
.
Kufikia sasa Genk imefunga mabao 7 na kuruhusu matano. Samatta amecheza mechi 8 za Europa na kufunga mabao 9 [Hatua ya makundi na kufuzu] .
.
.
.
Katika hatua ya Makundi Samatta ana mabao matatu kwenye mechi 3. .
Kufikia hivi sasa Samatta amehusika katika magoli 11 katika michezo 8 [Magoli 9 na asisst 2 .

Takwimu za Jumla za Samatta msimu huu amehusika magoli 18 kwenye michezo 18. [Magoli 16 na assists 2]
Mpaka sasa Samatta amehusika mabao 63 katika michezo 130, [Mabao 50 na Asissts 13].

Sasa Samatta ni miongoni mwa wafungaji waliowahi kufikisha mabao 50 ndani ya klabu ya Genk.

Mbwana Samatta ndiye mfungaji bora namba 6 wa klabu ya Genk

Mbwana Samatta ndiye mfungaji bora wa Genk kutoka bara la afrika 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
#Hainakufeli #Sokaupdates