Msenegal wa kwanza kutimiza magoli 50 PREMIER LEAGUE

Msenegali wa kwanza kutimiza magoli 50 katika Premier League – muafrika wa 7 kutimiza idadi hiyo.
:
Wengine ni:-
:
🇨🇮 Didier Drogba (104)
🇹🇬 Emmanuel Adebayor (97)
🇳🇬 Yakubu (95)
🇨🇮 Yaya Toure (59)
🇳🇬 Nwankwo Kanu (54)
🇳🇬 Efan Ekoku (53)
🇸🇳 Sadio Mane (50)
:
:
Liverpool 4-1 Cardiff City

Liverpool vs Cardiff City Leo: HAPATOSHI

LIVERPOOL vs CARDIFF CITY.

– Liverpool Ambao ndio vinara katika Msimamo wa Premier League wakichuana vikali na Mabingwa Watetezi Manchester City, Wikendi ya leo watakuwa nyumbani Anfield Kuwaalika Cardiff City. .
👉 Takwimu zao (head to head).
– Liverpool na Cardiff hawajawahi kukutana tokea msimu wa 2013-14 katika Premier League – Liverpool walishinda mechi zote, 3-1 ndani ya Anfield na wakashinda 6-3 ugenini.
.
– Mara ya mwisho Cardiff kushinda mechi Dhidi ya Liverpool katika ligi ni December 1959, Raundi ya pili waliipiga Liverpool 4-0 ndani ya Anfield, majogoo chini ya kocha Bill Shankly mwaka huo waliishia Nafasi ya tatu PL.
.
– Kuna Magoli matatu au zaidi hufungwa timu hizi zinapokutana Katika mechi 10 zilizopita, jumla zimefungana Magoli 45 Katika Mashindano yote kwenye hizo mechi 10.
.
– Liverpool wamepoteza mechi Moja tu Katika mechi 45 zilizopita wakiwa home Katika Dhidi ya timu zilizotoka kupanda Daraja (W35 D9), kipigo Pekee ni Dhidi ya Blackpool msimu wa 2010-11 – lakini wameshinda mechi zote saba chini ya kocha Jurgen Klopp ndani ya Anfield, wamefunga Magoli 21-2.
.
– Liverpool wamepoteza mechi Moja tu kati mechi 49 wakiwa home katika Premier League Dhidi ya timu Zinazoishia na ‘City’ (W30 D18), kipigo pekee kutoka kwa Swansea City January 2017.
.
– Cardiff wamepoteza mechi 14 Kati ya 15 Dhidi ya Vilabu vya “big six” Katika Premier League (D1), wameruhusu kufungwa magoli mawili na kuendelea kwenye mechi 12 Kati ya hizo 14.
.
– Magoli matatu na Assist tatu, Mshambuliaji wa Liverpool Mohammed Salah amehusika Katika Magoli Sita kwenye mechi tano zilizopita Dhidi ya timu zilizotoka kupanda Daraja.
.
– Kocha wa Cardiff Neil Warnock akiwa Kama kocha mkuu amekutana na Liverpool Mara Nne ugenini na zote kapokea kipigo na timu aliyo iongoza haijafunga Goli hata Moja – Pia Kafungwa na makocha tofauti Souness, Houllier, Benitez ba Dalglish.
.
– Mlinda lango wa Liverpool, Alisson anatafuta kuweka rekodi ya kuwa kipa wa pili wa Liverpool Katika historia yq Premier League kuwa na clean sheets 7 kwenye mechi 10 alizoanza msimu huu baada ya Jose Reina (7). Alisson Ana Clean Sheets 6 Katika mechi 9 Mpaka Sasa..

Brasil vs Cameroon November 20 : HAPATOSHI

– Hapatoshi jijini London Novemba 20, The Indomitable Lions “Cameroon” uso kwa uso dhidi ya Mabingwa Mara tano wa Dunia “Brazil” katika mechi ya kirafiki.

.
– Shirikisho la Soka Nchini Brazil limethibitisha kuwa November 20 watashuka Dimbani kukipiga Dhidi ya Cameroon, zitakuwa zimepita siku Nne baada ya Cameroon kutoka kucheza mechi Dhidi ya Morocco Katika mechi ya kuwania kufuzu AFCON 2019 wao ndio watakuwa Wenyeji.
.
– Cameroon Wakiwa wao kama wenyeji wa fainali kubwa Barani Afrika hapo mwakani, wanaona kucheza Dhidi ya Brazil Itakuwa ni maandalizi tosha Kuelekea kulitetea taji lao, kwani wao ndio Mabingwa Watetezi.
.
– Mara ya Mwisho kukutana Kwa Nchi hizo Mbili Brazil walishinda 4-1, huku nahodha wao Neymar akiingia nyavuni Mara Mbili.
.
– Mechi hii Itakuwa ni kipimo kingine Kwa kocha wa Cameroon, Clarence Seedorf, ambaye kapewa kibarua hicho mwezi Agosti ambapo kaiongoza nchi hiyo katika mechi za sare dhidi ya Comoros na Malawi pia na mechi ya ushindi 1-0 Dhidi ya Malawi.
.
– Kwa kocha wa wa Brazil, Tite hii Itakuwa ni mechi yake ya kwanza akiwa Kama kocha mkuu kukutana Dhidi ya timu ya Taifa kutoka Bara la Afrika

Tottenham: DELE ALLI Atakuwa Fiti kuwavaa MANCHESTER CITY

– Kocha mkuu wa klabu ya Tottenham, Mauricio Pochettino Amesema kuwa anaamini kiungo wake Dele Alli atakuwa fiti mpaka siku ya jumatatu kwa ajili ya kuivaa Manchester City, Muingereza huyo Amerejea Katika Mazoezi kamili ya Klabu yake na huenda akapangwa Katika Kikosi cha Klabu yake kitakachowavaa Mabingwa hao Watetezi wa Premier League.
.
– Kiungo huyo alikuwa Nje ya Uwanja akiunguza maumivu ya misuli Mpaka kupelekea kukosekana Katika mechi za Premier League ambazo ni Dhidi ya Watford, Huddersfield, Cardiff na West Ham, pia alikosa mechi tatu za Champions League ambazo ni dhidi ya Barcelona, Inter na PSV.
.
– Alli amecheza mechi Sita tu za Michuano yote Kwa Klabu yake na kafanikiwa kufunga Magoli mawili tu Dhidi ya Newcastle Katika Premier League na Dhidi ya Watford Katika EFL Cup – Siku ya Jumatatu tutashuhudia kiungo huyo akirejea wakati vijana wa Pep Guardiola watakapotembelea Wembley.
.

– Baada ya mechi dhidi ya City, Spurs wataivaa West Ham kwenye Carabao Cup kisha Wolves Katika Premier League na baadae watarejea Katika anga za Ulaya kwenye Champions League Dhidi ya PSV.

LiverPool Kuendelea kumkosa NABY KEITA

– Kiungo wa Kimataifa wa Guinea, Naby Keita ataendelea kukosekana katika majukumu ya kuitumikia klabu yake ya Liverpool baada ya kutopona majeraha yake aliyopata akiwa na timu yake ya Taifa.
.
– Kocha mkuu wa Majogoo hao, Jurgen Klopp Amethibitisha hii leo kuwa kiungo huyo atakuwa Nje wakati jeshi lake litakaposhuka Dimbani kukipiga Dhidi ya Cardiff City Wikendi hii Katika mechi ya Premier League..
.
– Pia Klopp Amesema wazi wataendelea kumkosa nahodha wao Jordan Henderson.
.
“[Keita na Henderson] wote hawatocheza kesho, lakini wapo katika hali nzuri ya kupona, lakini hawapo tayari kwa kesho” Klopp amethibitisha kwenye pre-match conference.

Real Mdrid Bila CHRISTIANO RONALDO

Matatizo ya Madrid – Nini Shida? Perez? Kocha au wachezaji?
:
:
Real Madrid wamekuwa na mwanzo mbovu wa ligi kuliko wakati wowote kwenye historia yao, baada ya mechi 9, wana pointi 14, ushindi 4, sare 2, wamefungwa 3. Katika mechi 5 zilizopita wana goli 1 tu. Nini shida?
:
Yawezekana matatizo ya sasa kimatokeo si kitu kipya kwani hata msimu uliopita muda kama huu waliangusha pointi za kutosha njiani kwenye michezo dhidi ya Levante, Valencia na Rea Betis.
.
Lakini kipindi hicho bado Madrid ilikuwa na Zidane, mtu ambaye uwepo wake ulisaidia sana kuficha mapungufu ambayo Madrid walikuwa nayo muda mrefu .
Zidane kwa nyakati tofauti amewahi kushika nafasi zote zinazohusiana moja kwa moja na soka kwenye Real Madrid, kuanzia mchezaji mkubwa enzi zake, kocha wa timu za vijana, mkurugenzi wa ufundi na mtaalamu wa usajili, kocha msaidizi kwenye kikosi cha kwanza na kocha mkuu hapo baadae.
:
Kama mtaalamu wa usajili na mkurugenzi wa ufundi ni Zidane aliyecheza sehemu muhimu ya usajili wa watu kama Varane ambaye isingekua mfaransa huyu mwenye upara Varane alikua anaelekea OT, ni Zizzou ambaye alimshawishi Perez kukiukwa matakwa yake na kumsajili Isco toka Malaga huku Perez akimuona si galactico.
.
Akiwa kocha Zizzou hakutegemea sana mbinu bora na mifumo sahihi, aliamini kuwa ana wachezaji sahihi ambao uwezo waliokuwa nao ungetosha kushinda mechi yoyote.
Wakati Zizzou anaondoka sababu iliyotajwa ni kutokukubaliana na Perez juu ya mwelekeo wa timu kwenye upande wa usajili, Zidane aliona kuwa Madrid ina tatizo la wachezaji kubweteka na kunyanyua ari yao kwa mechi au michuano mikubwa na kudharau michezo midogo hasa kwenye ligi .Leo hii Julen Lopetegui anaangushiwa jumba bovu katika mazingira ambayo wala hastahili lawama zozote.
.
Kuondoka kwa Zidane kulipaswa kuwakumbusha viongozi wa Real kuwa kiungo muhimu kwenye usajili. Walipaswa kuajiri mkurugenzi wa ufundi ambaye angekua na jukumu la kuandaa mkakati wa muda mrefu.
:
Perez alidharau mchango wa CR7 aliyekuwa akifunga angalau magoli 50 kila msimu – akaacha kusajili mbadala.
.
Swali gumu kujibika ni hili, Je wakimfukuza kocha Julen Lopetegui hali itabadilika?
:
El Clasico live on @azamtvtz J’pili saa 12:15 jion

Yanga Sc: kumsajili beki wa kimataifa wa RWANDA

Imeripotiwa kuwa klabu ya Yanga ipo kwenye mazungumzo na meneja wa beki wa kimataifa wa Rwanda Abdul Rwatubyaye anayecheza klabu ya Rayon Sports ya Rwanda ili kumsajili kipindi cha usajili wa dirisha dogo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia ni kuwa kamati ya Usajili ya klabu hiyo inataka kumuongeza beki huyo mwenye miaka 22 ili kuongeza nguvu kwenye eneo hilo.
Mpaka sasa beki huyo amebakiza mkataba wa mwaka mmoja na Rayon Sports