Matokea ya jana ya mechi za mpira

MATOKEO YA SOKA JANA JUMATANO NA RATIBA YA HII LEO:.

:

– UEFA Europa League FINAL

FT 4 Chelsea 🏆

1 Arsenal

.

– International – Club Friendlies.

FT SpVgg Lindau 2 – 4 FC Bayern München

.

– World Cup U-20 – Group A.

FT Colombia U20 6 – 0 Tahiti U20

FT Senegal U20 0 – 0 Poland U20

.

– World Cup U-20 – Group B.

FT Ecuador U20 1 – 0 Mexico U20

FT Italy U20 0 – 0 Japan U20

.

– Africa – COSAFA:: Group A.

FT Comoros 2 – 1 Mauritius

.

– Kenya – Premier League.

FT Chemelil Sugar 1 – 0 SoNy Sugar

FT Gor Mahia 2 – 2 Mathare United

FT KCB 2 – 2 Zoo FC

FT Kariobangi Sharks 4 – 0 Vihiga United

FT Nzoia Sugar FC 2 – 2 Bandari

FT Sofapaka 2 – 0 Kakamega Homeboyz

FT Tusker FC 2 – 1 Posta Rangers

FT Western Stima 0 – 0 AFC Leopards

.

– South Africa – Premier League.

(qualification)

FT Royal Eagles 0 – 2 Maritzburg United

:

RATIBA YA HII LEO.

– International – Friendlies

21:00 Turkey

Greece

.

– International – Friendlies

(women)

18:45 Germany

Chile

.

– World Cup U-20 – Group C

19:00 New Zealand U20

Uruguay U20

19:00 Norway U20

Honduras U20

.

– World Cup U-20 – Group D

21:30 Nigeria U20

Ukraine U20

21:30 USA U20

Qatar U20

.

– Africa – COSAFA:: Group B

18:30 Mozambique

Malawi

18:30 Namibia

Seychelles

.

– Egypt – Premier League

23:00 El Zamalek

El Entag El Harby

23:00 El Hodood

Pyramids FC

#Updates

@Sokawaytz

credit: @sokawaytz

Zahera simuachi yondani ng’oo

— “Mimi na Yondani mbona tuna mawasiliano mazuri kabisa, akiwa na matatizo yake ananiambia na tunajua tunafanyeje hata hayo anayosema kwamba anagoma kiukweli mimi sifahamu”.

— “Iko hivi mchezaji huyu hawezi kuondoka na nawaambia atazeekea hapa hapa, kwahiyo hayo maneno ya mtaani wala msiyasikilize,”.

👉 Kocha Mkuu wa Yanga SC akiweka wazi kuwa beki kisi wa Klabu hiyo, Kelvin Yondani atacheza Yanga mpaka yeye mwenyewe atakapoamua kusema basi amechoka na anahitaji kupumzika katika Masuala ya Soka.

#Updates

credit: @sokawaytz

TFF yaitangaza stand united kushuka daraja moja kwa moja

– Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB), ameitangaza timu ya Stand United ya Shinyanga kushuka daraja moja kwa moja badala ya Kagera Sugar kama ilivyotangazwa jana kwenye msimamo wa Shirikisho la soka Nchini Tanzania (TFF).

.

– Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPLB, Boniface Wambura Mgoyo, amewaambia Waandishi wa Habari Mchana huu Jijini Dar Es Salaam kwamba, kulikuwa na makosa katika uingizwaji wa matokeo ya mechi moja iliyowakutanisha Kagera Sugar na Stand United ambapo badala ya kuingiza Stand wameshinda 3-1, watu wa Data wa Bodi ya Ligi wakaingiza kimakosa 3-0, hivyo kuharibu uwiano wa jumla wa magoli ya kufunga na kufungwa baina ya timu hizo.

.

– Wambura amewaomba radhi wadau wa soka kwa kosa lililojitokeza na kusema Ofisi yake inawajibika kwa kumpa adhabu Ofisa aliyepotosha takwimu; RASMI: Kagera Sugar wanarejea kucheza Playoff dhidi ya Pamba SC, na Mwadui FC watakabiliana na Geita Gold SC… Game za kwanza za Playoffs kupigwa Juni 02 na Game za Marudiano kupigwa Juni 08 mwaka huu.

#Updates

@Sokawaytz

credit: @sokawaytz

Tuongee kuhusu soka na Kagawa ..kuelekea fainali ya Europa leo

KUELEKEA FAINALI YA UEFA EUROPA LIGI. 

       Leo kuelekea fainali ya ueropa ligi baina ya arsenal na chelsea nimeona nichambue vikosi vyote viwili na kuzipa asimia zao kuelekea fainal hiyo ya kukata na shoka kwasababu vilabu hivyo vinajuana vilivyo maana vimekutana sana katika mshikemshike wa ligi kuu ya uingereza. 

Chelsea

  Wamemaliza ligi vizuri kwa kufika top four ambapo awali katikati mwa ligi walilega lega sana hadi mashabiki wake kuwa na shaka na timu yao kufika top four hila walibadilika wakarudi vizuri hadi kumaliza ndani ya top four,  pamoja na hayo chelsea kama timuhawapo vizuri kuelekea fainal hii sababu ya majerui aliokua nao mfano kiungo tegemezi mkabji wa chelsea ngolo kante ana hati hati ya kukosa mchezo huo kutokana na majeraha,  hii inatosha kuonesha chelsea kwa kukosena kwa ngolo kante litakua tatizo kubwa kwao,  suala jingine chelsea hawana streika wa kat asilia ambaye yupo fomu ya kufunga, wanae top class streika gonzalo higuain hila hayupo katika fomu yake toka ajiunge na chelsea hivyo naona tumain lao lipo kwa giroud ambaye ni moto hasa katika mashindano haya ya ueropa,  na endapo kocha akamuini giroud ambaye akili yake ipo vizuri sana katika europa anaweza saidia chelsea katika fainal hiyo,  pia suala la kocha wa chelsea kutamka hazarani kua ameshindwa kunyanyua morali ya wachezaji wake na anataka kuipa mkon kwaher klabu hiyo, hii inaonyesha ni kiasi gani chelsea haipo sawa kuelekea fainal hiyo, vilevile kunataarifa za chini chini kulitokea ugomvi baina ya wachezaji jambo ambalo naona linawavuruga sana hasa katika kipindi hiki kuelekea fainali ya ueropa. 

Nguvu pekee waliokua nayo chelsea naona hipo kwa streika wao eden hazard ambaye yupo fomu kweli kweli,  juzi tuu ametoka kupokea tuzo ya mchezaj bora wa msimu aliyechaguliwa namashabiki,  hivyo morali yake hipi juu sana kuelekea fainali hiyo, pia suala lake la kuondoka katika clabu hiyo litampa nguvu yakutaka kuwaacha na kikombe cha ueropa kama zawadi yake kwa mashabiki,  hivyo chelsea tumaini lao pekee naona ni eden hazard na namuona ni mchezaji anayeweza kuamua fainali hiyo.  Mi naipa asilimia 40% chelsea kubeba kombe hilo

Arsenal

      Hawakumaliza ligi vizuri hasa baada ya kikosa nafasi ya top four hila katika kuelekea mwishoni mwa ligi arsenal waliwekeza nguvu zao katika kombe hili la ueropa ambapo wamefanikiwa kufika fainali hivyo naona arsenal wapo vizuri kiakili kuelekea fainali hii ya ueropa ligi,  udhaifu wa arsenal nauona katika beki yao abayo naona wanakosa kiongozi kama david luis,  sergio ramos pale madrid,  vincent kampany pale city. Hivyo arsenal kama watashindwa kucheza vizuri katika beki nayo namuona hazard atawafanya atakachojisikia,  pia suala la kuwakosa aron ramsey kiungo hatari sana kaika kufunga na kusaidia wezie kufunga litakua pengo kubwa kwao pia kumkosa mikhtarian nalo litakua pengo kwao katika ubunifu katika final third yao,  faida waliokua nayo ni streika wao wawili pierre aubemiyang na lacazzete,  wapo vizur sana hawa jamaa na wanaushikiano mzuri sana akikukosa mmoja mwingine anakufunga hivyo arsenal watakua hatari sana hasa eneo la mbele.  Pia suala la kuingia uefa kwa mgongo wa nyuma kwa kuchukua ueropa ligi, nahisi litainua hamasa kwao na kuona tumaini pekee ni kujituma na kupata tiketi ya kushiriki uefa msimu ujao, hivyo arsenal watakua na morali sana ukiongezea na ubora wa washambuliaji wao. Arsenal nawapa asimlia 60 kuchukua kombe hilo.  

Hila mchezo wa fainali ni fainali tu haungaliagi huko fomu kiasi gani kushinda mchezo huo kwani wachezaji ujituma sana kuipa heshima mchezo huo,  hivyo naona utakua mchezo mzuri sana ambaye shabiki yoyote wa soka hatotaka kuhukosa. 

Kagawa10

Neymar avuliwa unahodha Brazil ,Daniel Alves apewa Kitambaa

– Siku Baada ya Kuvuliwa unahodha, Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr ameondolewa katika Viwanja vya Mazoezi ya timu hiyo ya taifa Baada ya kupata Majeraha ya mguu wake wa kushoto.

.

– Kocha Tite alitangaza kumpa kitambaa cha unahodha Neymar mwaka jana, na Sasa ameamua kumvisha Dani Alves ambaye atawaongoza wenzake katika fainali za Copa America mwezi ujao wao wakiwa wenyeji.. Neymar alionekana kujilazimisha kufanya mazoezi lakini haikiwa nzuri na baadade Daktari wa timu hiyo ya taifa Rodrigo Lasmar alipoamua atolewe kwenda kufanyiwa uchunguzi zaidi..

#Updates

@Sokawaytz

credit: @sokawaytz