Kocha wa Ac Milan Gennaro Gattuso ajiudhulu

– Klabu ya AC Milan Imethibitisha kuwa, Gennaro Gattuso ameachana Rasmi na klabu hiyo Kama kocha Mkuu kwa Makubaliano maalumu; Gattuso ameiongoza Milan tangu Novemba 2017, uhamuzi huo kautoa Baada ya Klabu hiyo kushindwa kufuzu kushiriki Michuano ya @championsleague msimu ujao, wakimaliza nafasi ya tano katika Msimamo wa Serie A na kuangukia @europaleague.

.

– Gattuso 41; alisema hatma yake atatoa Baada ya Ligi kumalizika Baada ya game yao dhidi ya SPAL wakishinda 3-2, lakini ushindi wao haikuwafanya kuwashusha Wapinzani wao Inter Milan pamoja na Atalanta waliokuwa wakiwania nao nafasi mbili zilizosalia ukitoa Juventus na Napoli walijihakikishia kufuzu kwa muda mrefu.

.

– Kocha wa Monaco, Leonardo Jardim na kocha wa Lazio, Simone Inzaghi, Sasa wanatajwa kuchukua huenda mmoja wao akatua San Siro; Kwa Kuongeza, Milan Imethibitisha Kwa Mkurugenzi wao wa Michezo, Leonardo nae ametimka Baada ya msimu mmoja kudumu Klabuni hapo.. Anatajwa kutimkia Paris Saint-Germain ambako amewahi kufanya kazi hiyo kabla ya kutua Milan.

#Updates

@Sokawaytz

credit: @sokawaytz

Hali ya Ngolo kante bado ,Mashabiki wa Arsenal wamuombea asipone

– Kocha wa Klabu ya Chelsea, Maurizio Sarri amesema kuwa kiungo mahiri wa Klabu hiyo, Ngolo Kante ana Asilimia 50/50 za kucheza au kutocheza game ya fainali ya Europa league dhidi ya Arsenal wiki hii, Mfaransa huyo anasumbuliwa na majeraha ya mguu wake.. #Updates

credit: @sokawaytz

Yanga yakamilisha usajili wa kiungo mnyaruanda Patrick papy sibomana

✍🏻 Kumekucha Jangwani, Klabu ya Yanga SC Imekamilisha Usajili wa kiungo wa Kimataifa wa Rwanda, Patrick Papy Sibomana kwa Mkataba wa Miaka Miwili akitokea Klabu ya kwao Rwanda, Mukura Victory.

:

✍🏼 Sibomana 22, Aliwahi kuitumikia Klabu ya APR FC ya kwao Rwanda, mwaka 2017 akasaini Mkataba wa kuitumikia Klabu ya Shakhtyor Soligorsk ya Nchini Belarus kisha kurejea Rwanda mwaka huu na kutua Mukura na kisha Sasa Yanga SC ya Tanzania.

:

✍🏼 Nyota huyu ni Miongoni mwaka Wachezaji wanaounda timu ya taifa ya Rwanda “Amavubi” akiichezea timu hiyo tangu mwaka 2013 mpaka Sasa, Kafunga Magoli mawili na Moja ya Goli lake aliifunga Taifa Stars katika Mchezo wa Kimataifa wa Kirafiki Tanzania ikipoteza 2-0 mwaka 2015 ndani ya Dimba La Amahoro Stadium, Kigali..

#Updates #transfers

@Sokawaytz

credit: @sokawaytz

Kikosi bora cha msimu huu mwaka 2018-2019 na Kagawa 10

Makala

TUONGEE KUHUSU MPIRA na kagawa10.

KIKOSI BORA CHA MSIMU KUTOKA KATIKA TIMU 20 ZA LIGI KUU(TPL) 

   Wakati ligi kuu ikielekea ukingoni siku ya leo, nimeona nitoe kikosi bora ambacho kitajumuisha wachezaji waliofanya vizuri katika ligi kuu ya Tanzania(tpl),wachezaji ni wengi waliofanya vizuri katika ligi yetu ya bongo ambayo inachangamoto nyingi sana hila wachezaji wamejitaidi kuonesha uwezo wao.  Kikosi hiko kipo kama hivi

1. Aishi manura (simba) 

2. William lusian gallas ( lipuli) 

3. Bruce kangwa(azam) 

4. Erasto nyoni (simba)  

5. Kelvin yondani (yanga)  

6. Feisal Toto ( yanga)  

7. Clastus chota chama (simba)  

8. Jonas gerrald mkude (simba) 

9. Meddie kagere (simba)  

10. Herriet makambo (yanga)  

11. Ibram ajibu migomba (yanga)  

Sub

1.Aron kalambo ( prison) 

2. Hussein zimbwe (simba)  

3. Salim ayee (mwadui)  

4.Yakubu (azam)  

5. Jonh Boko (simba)  

6. Emmanuel okwi (simba)  

7. Aggrey morris. 

Wengi watajiuliza kwanini ajibu nimemuweka kwenye kikosi,  jibu lao ni hivi namba hazidanganyi naazaje kumuweka nje mtu anaeongoza kwa kusaidia upatikanaj wa magoli(assist 15) kwa msimu huu japo mech nyingi alikua ayupo kutokana na matatizo binafsi na timu yake, pia kumuweka jonas mkude kama namba nane wakati asili yake ni kiungo mzuiaji,  inatoka na kutumika sana eneo ilo na kufanya vizuri katika msimu uku nyuma yake akiwa saidiwa na james kotei napenda kumwita chuma. 

Yote kwa yote wachezaji ni wengi hila kwangu hao nimeona wamefanya vizur sana kwa msimu mzima. 

Makala hii imeandikwa na kagawa 10.