Category: michezo
Zahera ataja sababu ya kumuacha Ajib Dar

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema Ajib hakujumuishwa katika kikosi kwa kuwa bado hajawa ‘fit’ tangu apone majeraha ya misuli
Zahera amesema Ajib anahitaji muda zaidi wa kufanya mazoezi ili aweze kuwa tayari kurejea dimbani
Akizungumzia mchezo huo, Zahera amesema wamejiandaa kikamilifu kuikabili Alliance Fc ambayo inaonekana kupania zaidi mchezo huo
“Tunaufahamu ubora wa Alliance Fc na hata udhaifu wao pia tunaujua, hatuna wasiwasi kuelekea mchezo huo,” amesema Zahera
Mcongoman huyo aliyerejea usiku wa kuamkia jana na kuungana moja kwa moja na kikosi cha Yanga, amesema atatumia siku ya leo na kesho kufanya maandalizi ya mwisho tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumamosi March 30 katika dimba la CCM Kirumba
Bocco Aweka Rekodi Ya Kimataifa
Tetesi za soka barani Ulaya Alhamisi hii, Hudson-Odoi, Sanchez, Rashford, Maguire, Chilwell
Wengine wawili waingia anga za Simba Today

Juzi Jacques Tuyisenge alikuwa nchini kumalizana na mabingwa hao wa Tanzania Bara akitarajiwa kujiunga nao mwishoni mwa msimu wakati huo huo nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib nae akiwa njiani kurejea nyumbani
Anayefuatia ni beki kisiki wa Azam Fc Yakubu Mohammed. Inaelezwa Yakubu tayari amefikia makubaliano ya awali na uongozi wa Simba na atamwaga wino mwishoni mwa msimu
Kakolanya nae safi
Mlinda lango wa Yanga Beno Kakolanya aliyegoma kuitumikia timu hiyo kutokana na ‘ukata’, nae anasubiri kumalizwa kwa mgogoro baina yake na uongozi wa timu hiyo
Kakolanya ameitaka Yanga ivunje mkataba wake na tayari ameliwasilisha suala hilo kwa TFF
Kakolanya anatarajiwa kujiunga na Simba akiwa mchezaji huru
Wakati huo huo Simba inaendelea kumjaribu kiungo mkabaji Jean Vital Ourega aliyetokea nchini Ivory Coast
ARSENAL: Kiungo Huyu kiokosa Newcastle
Kiungo wa klabu ya Arsenal Granit Xhaka anatarajia kuukosa mchezo ujao wa Ligi Kuu Uingereza dhidi ya Newcastle Utd wikiendi hii kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa kimataifa dhidi ya Denmark siku ya Jumanne uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3.
.
Xhaka alifunga bao moja katika mchezo huoCc: sokaonlineupdates
Magazeti ya leo, Alhamis, March 29 2019











UWANJA WA SIMBA SC BUNJU

Hata hivyo Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori amesema tayari TAKUKURU imeziachia nyasi hizo hivyo wakati wowote ujenzi wa uwanja huo utaendelea
Awali uwanja huo ulitarajiwa kukamilika mwezi wa pili lakini sasa baada ya nyasi hizo kuachiwa, Magori amesema ujenzi utakamilika baada ya wiki mbili
Mwekezaji wa klabu ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ aliahidi kuukamilisha uwanja huo tayari kuanza kutumika kabla ya msimu huu kumalizika



Michezo ya robo fainali kombe la FA kuanza leo

KMC itakuwa uwanja wa Taifa kuikabili African Lyon wakati Lipuli Fc itakuwa uwanja wa Samora kuikabili Singida United

Keshokutwa Ijumaa, Kagera Sugar itaumana na Azam Fc kwenye dimba la Kaitaba wakati siku ya Jumamosi Yanga itakamilisha michezo ya robo fainali kwa kuivaa Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa CCM Kirumba
Magazeti ya leo, Jumatano, March 27 2019






















