Zahera ataja sababu ya kumuacha Ajib Dar

Nahodha wa kikosi cha Yanga Ibrahim Ajib hajasafiri na timu hiyo kuelekea mkoani Mwanza ambapo keshokutwa Jumamosi itashuka katika uwanja wa CCM Kirumba kuikabili Alliance Fc kwenye mchezo wa robo fainali, kombe la FA

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema Ajib hakujumuishwa katika kikosi kwa kuwa bado hajawa ‘fit’ tangu apone majeraha ya misuli

Zahera amesema Ajib anahitaji muda zaidi wa kufanya mazoezi ili aweze kuwa tayari kurejea dimbani

Akizungumzia mchezo huo, Zahera amesema wamejiandaa kikamilifu kuikabili Alliance Fc ambayo inaonekana kupania zaidi mchezo huo

“Tunaufahamu ubora wa Alliance Fc na hata udhaifu wao pia tunaujua, hatuna wasiwasi kuelekea mchezo huo,” amesema Zahera

Mcongoman huyo aliyerejea usiku wa kuamkia jana na kuungana moja kwa moja na kikosi cha Yanga, amesema atatumia siku ya leo na kesho kufanya maandalizi ya mwisho tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumamosi March 30 katika dimba la CCM Kirumba

Bocco Aweka Rekodi Ya Kimataifa

Bocco Aweka Rekodi Ya Kimataifa
ACHANA na Clatous Chama ambaye alifunga bao lililoipeleka Simba kwenye hatua ya makundi na vilevile akapachika lililoivusha robo fainali.

Kwenye Simba kafanya vizuri lakini Zambia timu yake ya Taifa imechemka. Wameenda kuishukia Namibia mabao kibao yote kazi bure.

Kuna mtu mmoja anaitwa John Bocco. Anastahili heshima ndani ya ardhi ya Tanzania, ameweka rekodi ambayo hata Chama imemshinda pamoja na mbwembwe zake zote.

Ameweka rekodi ya kipekee baada ya kuzisaidia timu mbili za Simba na Taifa Stars kufanya makubwa mwaka huu na kurejesha heshima ya Tanzania.

Bocco ambaye amefunga mabao tisa kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, hadi sasa amehusika kwenye kutengeneza mabao matatu muhimu kuliko wachezaji wengine wote wa Tanzania.
Bocco ambaye ni mchezaji wa zamani wa Azam, alianza kazi yake hiyo kwenye mchezo wa Simba dhidi ya AS Vita Club wa kutafuta nafasi ya kucheza hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Katika mchezo huo, Bocco ndiye alitoa pasi ya bao la ushindi kwa timu yake katika dakika ya tisini ambapo Simba ilipata ushindi wa mabao 2-1 na kwenda robo fainali.
Alipiga pasi ambayo ilirukwa na kiungo Haruna Niyonzima na mpira ukamfikia mfungaji Clatous Chama ambaye aliifungia timu yake bao hilo muhimu na kuipeleka Simba kwenye robo fainali.

Hata hivyo, baada ya kumaliza kazi kwenye klabu yake, Bocco alifanya tena mambo makubwa kwenye mchezo wa Taifa Stars dhidi ya Uganda ambapo aliipa timu hiyo ushindi tena kwa staili ileile.
Bocco alitoa pasi mbili za mabao kwenye mchezo huo ambao Taifa Stars walipata ushindi wa mabao 3-0.
Mshambuliaji huyo mwenye upeo wa kuchanganua mambo, alitoa pasi ya bao la kwanza na la mwisho, huku lile la pili likifungwa na beki Erasto Nyoni kwa mkwaju wa penalti baada ya mchezaji mmoja wa Uganda kuunawa mpira eneo la hatari.

Pasi hizo mbili ni zile za mabao ya Simon Msuva na Aggery Morris, yaliyoifanya Taifa Stars ifuzu Afcon ambapo fainali zake zinatarajiwa kufanyika nchini Misri kuanzia Juni mpaka Julai, mwaka huu.

Tetesi za soka barani Ulaya Alhamisi hii, Hudson-Odoi, Sanchez, Rashford, Maguire, Chilwell

Barcelona wapo tayari kuwapa Manchester United kiungo Philippe Coutinho, 26, ama Malcom, 22, kama sehemu ya ofa ya kumnasa mshambuliaji Marcus Rashford, 21. (Mundo Deportivo, via Mail)
Klabu ya Borussia Dortmund inasisitiza kuwa haina mpango wa kumuuza mchezaji wao raia wa Uingereza Jadon Sancho, 19, ambaye amekuwa akihusishwa na Manchester United. (Mirror)
Chelsea wanaweza wakasikiliza ofa za usajili za zaidi ya Pauni milioni 43 ili kumuachia mshambuliaji kinda wa Uingereza Callum Hudson-Odoi, 18. (Sport Bild, via Metro)

Leicester hawapo tayari kuwatoa mabeki wake Harry Maguire, 26, na Ben Chilwell, 22, ambao wamekuwa wakinyemelewa na vilabu vikubwa vya Manchester United na Manchester City. (Mirror)
Manchester United hawana mpango wa kumuuza mchezaji wao anayepokea mshahara mkubwa zaidi, Alexis Sanchez, 30, licha ya kutoonesha makali uwanjani na ripoti kuwa suala la mshahara wake linatatiza mapatano ya mkataba mpya na kipa David De Gea. (London Evening Standard)

Beki wa Liverpool Dejan Lovren ananyemelewa na vilabu vikongwe vya Italia, Roma, Napoli na AC Milan ili wamsajili mwishoni mwa msimu. (Mirror)
Manchester City ni miongoni mwa vilabu ambavyo vinamfuatilia kwa karibu winga wa Swansea na Wales Dan James, 21. (Sun)

Mshambuliaji kinara wa klabu ya Tottenham Harry Kane, 25, amesema anataka kucheza kwenye ligi ya Marekani NFL “ndani ya miaka 10 au 12 ijayo”. (ESPN)

Kiungo wa Liverpool na Serbia Marko Grujic, 22, ambaye yupo kwa mkopo katika klabu ya Hertha Berlin, anataka kusalia kwenye klabu hiyo ya Ujerumani walau kwa mwaka mmoja zaidi. (Liverpool Echo)
Mshambualiaji wa raia wa Paraguay Sergio Diaz, 21, atasalia Real Madrid baada ya klabu ya Corinthians ya Brazil, ambako amekuwa kwa mkopo msimu huu kuamua kuwa hawatamnunua. (Marca)

Wengine wawili waingia anga za Simba Today

Simba imepania kwelikweli kuboresha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao! Hilo limedhihirika kutokana na michakato ya usajili kuanza mapema

Juzi Jacques Tuyisenge alikuwa nchini kumalizana na mabingwa hao wa Tanzania Bara akitarajiwa kujiunga nao mwishoni mwa msimu wakati huo huo nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib nae akiwa njiani kurejea nyumbani

Anayefuatia ni beki kisiki wa Azam Fc Yakubu Mohammed. Inaelezwa Yakubu tayari amefikia makubaliano ya awali na uongozi wa Simba na atamwaga wino mwishoni mwa msimu

Kakolanya nae safi

Mlinda lango wa Yanga Beno Kakolanya aliyegoma kuitumikia timu hiyo kutokana na ‘ukata’, nae anasubiri kumalizwa kwa mgogoro baina yake na uongozi wa timu hiyo

Kakolanya ameitaka Yanga ivunje mkataba wake na tayari ameliwasilisha suala hilo kwa TFF

Kakolanya anatarajiwa kujiunga na Simba akiwa mchezaji huru

Wakati huo huo Simba inaendelea kumjaribu kiungo mkabaji Jean Vital Ourega aliyetokea nchini Ivory Coast

ARSENAL: Kiungo Huyu kiokosa Newcastle

Kiungo wa klabu ya Arsenal Granit Xhaka anatarajia kuukosa mchezo ujao wa Ligi Kuu Uingereza dhidi ya Newcastle Utd wikiendi hii kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa kimataifa dhidi ya Denmark siku ya Jumanne uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3.
.
Xhaka alifunga bao moja katika mchezo huoCc: sokaonlineupdates

UWANJA WA SIMBA SC BUNJU

Ujenzi wa uwanja wa Simba ulioko Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es salaam ulisimama kwa muda kutokana na nyasi bandia za uwanja huo kushikiliwa na TAKUKURU kwa ajili ya uchunguzi wa kesi iliyokuwa ikiendelea

Hata hivyo Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori amesema tayari TAKUKURU imeziachia nyasi hizo hivyo wakati wowote ujenzi wa uwanja huo utaendelea

Awali uwanja huo ulitarajiwa kukamilika mwezi wa pili lakini sasa baada ya nyasi hizo kuachiwa, Magori amesema ujenzi utakamilika baada ya wiki mbili

Mwekezaji wa klabu ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ aliahidi kuukamilisha uwanja huo tayari kuanza kutumika kabla ya msimu huu kumalizika

Michezo ya robo fainali kombe la FA kuanza leo

Michezo ya Robo Fainali kombe la FA (ASFC) inaanza leo ambapo michezo miwili inatarajiwa kupigwa

KMC itakuwa uwanja wa Taifa kuikabili African Lyon wakati Lipuli Fc itakuwa uwanja wa Samora kuikabili Singida United

Keshokutwa Ijumaa, Kagera Sugar itaumana na Azam Fc kwenye dimba la Kaitaba wakati siku ya Jumamosi Yanga itakamilisha michezo ya robo fainali kwa kuivaa Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa CCM Kirumba