Simba ina malalamiko ya msingi kubadilishwa kwa waamuzi

Kikosi cha Simba kikiendelea na maandalizi ya kujifua kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya TP Mazembe itakayochezwa Lubumbashi DR Congo uongozi wa timu hiyo ulipokea taarifa ya ghafla na kushtushwa.

Uongozi wa Simba umepokea taarifa hiyo kutoka kwa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuwa wamebadilisha waamuzi waliopangwa hapo awali kuchezesha mchezo wa marudiano kati ya TP Mazembe na Simba utakaochezwa Aprili 13.

Awali CAF ulitangaza waamuzi wa mechi ya kwanza kati yao ambayo ilichezwa hapa Dar es Salaam Aprili 6, na wengine ambao watachezesha mchezo wa marudianio.

Waamuzi wa awali waliopangwa na CAF, kuchezesha mchezo wa marudiano TP Mazembe na Simba ni Bamlak Tessema mwamuzi wa kati kutoka Ethiopia, Temesgin Samuel msaidizi namba moja kutoka Ethiopia, Gilbert Kipkoech Cheruiyot msaidizi namba mbili kutoka Kenya.

Wengine ambao walipangwa awali na CAF, mwamuzi wa akiba Peter Waweru kutoka Kenya.

Katika barua ambayo ilionyesha inatoka CAF, ambayo uongozi wa Simba uliipokea Aprili 7, ilisema kuwa waamuzi hao walibadilishwa kwa sababu ya kiiufundi ingawa hawakuziweka wazi.

Baada ya CAF kufanya mabadiliko waamuzi wapya waliopangwa Janny Sikazwe kutoka Zambia atayekuwa mwamuzi wa kati, Berhe Tesfagiorgis kutokea Eritrea atakuwa msaidizi namba moja, Romeo Kasengele kutokea Zambia atakuwa msaidizi namba mbili, Audrick Nkole kutokea Zambia atakuwa mwamuzi wa akiba.

Wakati Aimable Habimana kutokea Burundi atakuwa Kamishna, Salah Ahmed kutokea Sudan atakuwa msimamizi wa waamuzi.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori alisema wanafahamu miongoni mwa wamiliki wa timu hiyo Moise Katumbi shughuli zake nyingi huwa anafanya nchi Zambia ambapo waamuzi wa wapya waliopangwa kuchezesha mchezo huo wanatoka nchini humu.

Magori alisema awali walishapangwa waamuzi wa kuchezesha mechi zote mbili inakuaje baada ya mchezo wa kwanza umeshachezwa na matokeo yake kufahamika ndio wabadili waamuzi waliopangwa kuchezesha mechi ya marudiano.

Alisema tumeandika barua CAF, kuwalalamikia kuwa hatujalisishwa na jambo hili na atukubali kabisa kwa hali ya kawaida jambo hilo la kubadili waamuzi na kulinganisha ukubwa wa mechi na matokeo ya kwanza yalivyokuwa lazima timu yoyote itakuwa na mashaka.

“Kwa hali ya kawaida ukaribu wa Ndola Mji ambao ata mwamuzi mpya Sikazwe ambaye amepangwa kuchezesha mchezo wetu anatumia saa mbili tu kwa gari mpaka kuingia Lubumbashi DR Congo ambapo tutacheza mechi ya marudiano.

“Ukaribu huu wa waamuzi wapya kiukweli uongozi wa Simba umefikisha malalamiko CAF, ili kuweza kulishuhurikia jambo hili kabla ya mchezo wetu wa marudiano,” alisema Magori.

Cc: Mwanasport

SIMBA – Shabiki Aliyetembea MBEYA -DAR Apata Shavu

Shabiki Ramadhan Mohamed ambaye alikuja Dar es Salaam akitokea Mbeya kwa miguu ili ashuhudie mchezo wa robo fainali ya #CAFCL dhidi ya TP Mazembe, leo amekutana na viongozi, wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi na sekretarieti ambapo amehaidiwa kugharamiwa na klabu kwenda Lubumbashi kuangalia mchezo wa marudiano ambao utachezwa Jumamosi Aprili 13, 2019. #NguvuMoja

SIMBA Yatuma malalamiko CAF – Mabadiliko ya Marefa

Klabu ya Simba kupitia kwa Mtendaji wake Mkuu Crescentius Magori, imeliandikia barua Shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) kufuatia mabadiliko ya waamuzi wa mchezo wa pili wa robo fainali ligi ya mabingwa kati ya TP Mazembe dhidi ya Simba

Mapema leo CAF ilitoa taarifa juu ya mabadiliko hayo ambayo yamefanyika siku tano kabla ya mchezo utakaopigwa April 13 Lubumbashi, DR Congo

TP Mazembe ndio iliyoomba kubadilishwa kwa waamuzi hao

Simba imeeleza hofu yake kwa mabadiliko hayo ya kushitukiza kuwa yasije yakawa na lengo baya

“Tumetuma malalamiko dhidi ya @CAF_Online kwa kufanya mabadiliko ya waamuzi wa mchezo wa marudiano wa #CAFCL ambao tutacheza Jumamosi. / We have formally lodged a complaint against CAF for the abrupt change in referees ahead of match against TP Mazembe in this Saturday in DRC”

Simba kuifuata TP Mazembe Alhamisi ijayo

Kikosi cha Simba kitaondoka jijini Dar es salaam Alfajiri ya Alhamisi, April 11 2019 kuelekea DR Congo tayari kwa mchezo wa marudiano, robo fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe


Uongozi wa Simba umewaalika wapenzi, mashabiki na wanachama wa timu hiyo ambao wangependa kusafiri na kikosi cha Simba nchini Congo, kujiandikisha

Simba inayo nafasi ya kufanya maajabu Congo

Katika michezo minne ya robo fainali ya ligi ya mabingwa iliyopigwa jana, ni Mamelodi Sundowns pekee iliyotumia vyema uwanja wake wa nyumbani kwa kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Al Ahly

Horoya ililazimishwa suluhu ya bila kufungana na Wydad Casablanca kama ilivyokuwa kwa Simba dhidi ya TP Mazembe

CS Constantine ilikubali kipigo cha mabao 3-2 nyumbani dhidi ya mabingwa watetezi Esperance

Michezo ya marudiano inatarajiwa kupigwa wiki ijayo April 13

Wawakilishi wa Tanzania, Simba watasafiri Lubumbashi DR Congo kuikabili TP Mazembe itakayokuwa nyumbani

Kwenye mchezo huo wa marudiano Simba inahitaji matokeo ya aina mbili ili iweze kutinga nusu fainali

Ushindi au sare yoyote ya mabao itaihakikishia Simba kuingia nusu fainali

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wanao uwezo wa kufuzu ugenini baada ya kufanya tathmini ya mchezo wa jana

Amesema watajipanga wakapambane ugenini kuhakikisha wanapata matokeo yanayoweza kuwapeleka hatua ya nusu fainali

Nitarejea uwanjani karibuni – Wawa

Beki kisiki wa Simba Serge Paschal Wawa jana alilazimika kutoka kwenye dakika ya sita mchezo dhidi ya TP Mazembe baada ya kupata maumuvu ya mguu

Wawa amesema maumivu hayo yalimfanya ashindwe kuendelea na mchezo hata hivyo aliwapongeza wachezaji wenzie kwa kufanikiwa kumaliza mchezo huo bila ya kuruhusu bao

Wawa amesema atarejea kikosini hivi karibuni lakini huenda akaukosa mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki ijayo Lubumbashi, DRC

“Nilitoka uwanjani na kuiacha timu yangu inapambana, walinihitaji lakini sikuweza kuendelea kutokana na maumivu niliyokuwanayo hata wakati natembea nilikuwa napata maumivu makali,” alisema Wawa

“Ingawa ninamaumivu makali namwachia Mungu, naamini nitarejea uwanjani hivi karibuni.

“Mchezo wa marudiano utakuwa mgumu lakini ninaimani na wachezaji wenzangu na timu nzima kwa ujumla”

Baada ya Wawa kutoka, nafasi yake ilichukuliwa na Juuko Murshid ambaye alicheza vyema sambamba na kiraka Erasto Nyoni

Bocco asilaumiwe kwa kukosa penati – Aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema matokeo ya suluhu waliyopata dhidi ya TP Mazembe jana yalitokana na timu hiyo kukosa bahati na hakuna jambo jengine

Aussems amesema wachezaji wake jana walicheza kama alivyowaelekeza walitengeneza nafasi nyingi, lakini walikosa bahati

Akizungumzia tukio la nahodha John Bocco kukosa mkwaju muhimu wa penati ambayo huenda ingeiweka Simba katika mazingira mazuri ya kuibuka na ushindi, Aussems amesema Bocco hawezi kulaumiwa kwa kukosa penati kwa kuwa hiyo ni sehemu ya mchezo

“Huwezi kumlaumu mchezaji kwa kukosa penati kwani, hilo ni pigo la bahati pia,” alisema

“Wachezaji wote duniani huwa wanakosa penati hivyo hapaswi kulaumiwa”

Nae msemaji wa Simba Haji Manara amewashukia baadhi ya mashabiki wa timu hiyo ambao wamemshambulia Bocco baada ya mchezo wa jana

Manara amesema Bocco ndiye mchezaji ambaye yuko katika kiwango bora zaidi katika kikosi cha Simba kwa sasa

Kwa siku za karibuni Bocco ameifungia Simba mabao mengi kwenye ligi pamoja na kutoa pasi muhimu bila kusahau amekuwa na rekodi nzuri ya kufunga mikwaju ya penati

“Kumlaumu Bocco kwa kukosa mkwaju wa penati kunasababisha na ugeni wa baadhi ya mashabiki kwenye soka,” amesema Manara

“Bocco huyu ndiye anayefunga penati nyingi za Simba. Hata tulipocheza na Nkana kule Kitwe Zambia, ni Bocco aliyefunga penati muhimu ambayo baadae ilitusaidia kupata matokeo ya kuingia hatua ya makundi”

“penati ni pigo la bahati na halina mwenyewe”

Tutasaka ushindi Congo – Aussems

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema, bado wana nafasi ya kufuzu hatua ya nusu fainali licha ya kupata suluhu na TP Mazembe nyumbani kwa sababu inawezekana.

Kauli hiyo pia imeungwa mmkono na Kocha wa TP Mazembe, Mihayo Kazembe baada ya kutamka, hawawezi kushangilia mpaka watakaposhinda mechi hiyo ya marudiano itakayochezwa Aprili 13, Lubumbashi, DR Congo.

Aussems amezungumza hayo baada ya kumalizika kwa mchezo huo uliochezwa leo Jumamosi Uwanja wa Taifa jIjinj Dar e Salaam.

“Nakubaliana na matokeo na kiwango walichoonyesha wachezaji wangu”

“TP Mazembe ni timu kubwa ingawa tulitakiwa kupata matokeo mazuri zaidi,” alisema Aussems.

Amesema, walipata nafasi lakini walishindwa kufunga. “Nafasi zilikuwepo lakini ndiyo hivyo, sasa tunajiandaa na mechi ya marudiano tutafanikiwa tu,”alisema Aussems.

“Kupata sare nyumbani si kitu kizuri lazima utapata mshtuko kwa sababu tulitegemea kushinda.” Kwa upande wa Kocha wa TP Mazembe, Mihayo Kazembe amesema, haukuwa mchezo rahisi na mashabiki wameshuhudia mchezo mzuri, sisi tulikosa bao na simba pia walikosa.

“Tunarudi Lubumbashi kwa maandalizi mengine na tunakwenda kujipanga na kuweka nguvu tushinde,” alisema Mihayo. Kuhusu suluhu Mihayo amesema : ” Hatuwezi kushangilia sasa kwa sababu ya matokeo ya suluhu tutafurahi baada ya mchezo wa mwisho watakapopata matokeo mazuri.

” Huo ni mchezo wa kwanza wa hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa Simba na TP Mazembe, mechi ya marudiano itachezwa Lubumbashi, DR Congo.

Mwanaspoti