Full Time: Real Madrid 1- 4 Ajax #UEFA Champion League




Duuuh
Full Time: Real Madrid 1- 4 Ajax #UEFA Champion League




Duuuh

Msanii wa muziki wa Pop Anitta ameanza kuingia katika tuhuma za kudaiwa kutoka kimapenzi na mwanasoka wa Brazil ambaye pia ni mchezaji wa Paris Saint Germain ya nchini Ufaransa Neymar, Anitta ameanza kuhusishwa kuwa katika mahusiano na Neymar baada ya ukaribu kuzidi.

Anitta na Neymar wameonekana wakiwa beneti katika jiji la Rio De Janeiro nchini Brazil, ukaribu ambao umeanza kuzua utata mitandaoni kuwa inawezekana wawili hao kuna kitu kinaendelea, Anitta ni moja kati ya wasanii wa Pop maarufu nchini Brazil na Amerika ya Kusini na amekuwa akifanya kazi zake kwa kutumia lugha ya kireno.

Neymar na Anitta wakiwa Rio De Janeiro katika tamasha la Sambadrone wameonekana wakikumbatiana na ku-kiss kitu ambacho kinaaminika kuwa kuna uwezekano wawili hao wakawa mapenzini, Neymar alithibitika kuachana na girlfriend wake ambaye ni muigizaji maarufu nchini Brazil Bruna Marquezine toka October 2018.

Baada ya kufukuzwa kazi na uongozi wa Man Unitedkwa kocha wa kireno Jose Mourinho, mashabiki wengi wa soka wanatamani kujua mreno huyo ana mpango wa kwenda timu gani kuifundisha tena licha ya kuhusishwa na vilabu kadhaa ikiwemo club yake ya zamani ya Real Madrid.
Mourinho alipata nafasi ya kufanya mahojiano na beINSports na alipoulizwa kama ana mpango wa kurudi kufanya kazi katika club aliyowahi kufanya kazi awali alijibu kuwa ndio ni furaha na fahari kubwa kwake kurudi kama watakuwa wameona umuhimu wake na kumuhitaji kama ni Chelsea lakini kwa Real Madrid hapana.

“Kurudi timu ambayo nilikuwa awali sio tatizo kama wameniita tena kama naona ni wakati sahihi, kuna mfumo sahihi na malengo ya mbali hakuna shida kwa mimi kurudi katika club ambayo nimewahi kufanya kazi awali, nafikiri ni fahari kubwa wakati club uliyowahi kuifanyia kazi kukuita tena”>>> Jose Mourinho
“Lakini kwa sasa nina hamu ya kurudi Chelsea sio Real Madrid, hapana naipenda Hispania lakini sichagua timu kwa sababu ya nchi au hali ya hewa”>>> Jose Mourinho
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Jose Mourinho amewahi kufanya kazi na vilabu tofauti tofauti kwa nyakati tofauti ikiwemo Real Madrid na Chelsea, Chelsea amewahi kuifundisha katika vipindi viwili (2004-2007) na (2013-2015) wakati Real Madrid amewahi kuifundisha kwa miaka mitatu (2010-2013).
Full Time
Dortmund 0-1 Tottenham
(Agg. 0-4)
#UCL

Hatimae muda wa furaha umeisha ndani ya club ya Real Madrid ikiwa ni siku moja imepita toka kiungo wa timu hiyo Luka Modric kukiri kuwa timu yao haina mbadala wa Cristiano Ronaldo na wanamkumbuka sana, pia Real Madrid imempoteza kocha wao aliyewaweka katika rekodi ya kihistori na kuwapa Ubingwa wa UEFA Champions League mara tatu.

Real Madrid ikiwa inacheza msimu wake wa kwanza wa UEFA Champions League bila uwepo wa Cristiano Ronaldo wamejikuta wakitolewa katika michuano hiyo na kuvuliwa Ubingwa huo baada ya kutwaa mara tatu mfululizo, kufuatia kipigo cha magoli 4-1 wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani Santiago Bernabeu, ushindi wa ugenini wa 2-1 waliowafunga Ajax wiki mbili zilizopita haujawa na msaada kwao.

Hivyo Real Madrid wamejikuta wanaondolewa katika michuano hiyo kwa ushindi wa Ajax wa jumla ya magoli 5-3, Real Madrid baada ya kutolewa leo katika hatua ya 16 bora ndio wanakuwa wametolewa kwa mara ya kwanza katika michuano hiyo katika hatua ya mapema zaidi, kwani kwa miaka 9 toka (2010-2011) hawajawahi kutolewa hatua ya 16 bora au robo fainali.


Matokeo ya game za UEFA Champions League zilizochezwa usiku wa March 5 2019, Ajax na Tottenham zimefuzu robo fainali.
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Bodi hiyo, mabadiliko hayo huenda yakaanza kutumika kuanzia msimu ujao
Maeneo yaliyoguswa na mabadiliko hayo
1. Pigo la Mkwaju wa Penati
Iwapo mkwaju wa penati utaokolewa na kurudi uwanjani au kugonga mwamba, haitaruhusiwa kupiga tena. Yaani hakutakuwa na nafasi ya kuufuata mpira kujaribu kufunga kwa mara nyingine
2. Goli la mkono
Goli litakalofungwa ambalo litagusa mkono wa mfungaji iwe kwa bahati mbaya au kwa makusudi halitakubaliwa
3. Mabadiliko ya mchezaji
Mchezaji anayefanyiwa mabadiliko sasa taruhusiwa kutokea upande wowote wa uwanja
4. Kuanzisha mpira uliotoka langoni
Mchezaji ataruhusiwa kugusa mpira hata ndani ya eneo la 18 kutoka kwa kipa , ambapo sasa hivi ni mpaka mpira utoke kwenye 18 ndio unaruhusiwa kuugusa.
5. Kadi kwa makocha
Makocha na wasaidizi wao watakuwa wakipewa kadi za njano na nyekundu kulingana na makosa wanayofanya wakiwa benchi. Kadi hizo zitakuwa na athari ya kukosa michezo kama ilivyo kwa wachezaji
6. Ukuta wa kuzuia mipira iliyokufa (freekick)
Wachezaji wa upande ambao wanapiga mipira iliyokufa ( freekick ) hawatoruhusiwa kwenda kujumuika kwenye ukuta wa timu ambayo inazuia mipira hiyo , tofauti na sasa ambapo wanaweza kujichanganya ili kuharibu mpangilio wa wapinzani wao
7. Mlinda lango katika kuzuia Penati
Mlinda lango anaruhusiwa kuweka mguu mmoja tu kwenye mstari na mwingine akaweka popote , tofauti na sasa kwamba miguu yote lazima iwe kwenye mstari kabla ya mkwaju wa penati kupigwa
Matokeo ya mechi za leo TPL
Hali ya mshambuliaji hatari wa Simba Emmanuel Okwi imeshindwa kulishawishi benchi la ufundi ambapo ameondolewa katika kikosi cha wachezaji 20 kilichoondoka jioni ya leo Jumanne March 05 2019 kuelekea nchini Algeria
Pamoja na kuuguza jeraha la chini ya jicho, Okwi alipata maumivu ya goti kwenye mchezo dhidi ya Lipuli Fc na kulazimika kurudishwa jijini Dar es salaam kutibiwa wakati kikosi cha Simba kikielekea mkoani Shinyanga kuikabili Stand United
Hata hivyo yaonekana hali yake haikutengemaa na benchi la ufundi kulazimika kumuondoa kikosini
Kikosi kilichosafiri;
Aishi Manula,
Zana Coulibaly
Nicholas Gyan
Asante Kwasi
Mohammed Hussein
Pascal Wawa
Poul Bukaba
James Kotei
Jonas Mkude
Mzamiru Yassin
Hassan Dilunga
Cletus Chama
Rashid Juma
Abdul Selemani
John Bocco
Maddie Kagere
Adam Salamba
Deo Munishi
Asante Kwasi
Mohammed Ibrahim
Haruna Niyonzima.
Shomari Kapombe anatarajiwa kurejea Afrika Kusini wiki hii kwa ajili ya vipimo vya mwisho kabla ya kuruhusiwa kuanza mazoezi mepesi. Pichani Kapombe akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu Crescentius Magori. #NguvuMoja
Jumamosi ya wiki hii Simba itakuwa ugenini nchini Algeria ikichuana na JS Saoura katika mchezo ambao huenda ukaifanya Simba iandike historia nyingine barani Afrika
Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka baadae leo kuelekea Algeria ambapo Aussems amesema wanakwenda kusaka alama tatu
“Kwa nini tufikirie sare badala ya ushindi? tunaenda Algeria kupambana kupata ushindi ambao kwa kweli utakuwa umetuweka karibu kabisa na kufuzu hatua ya robo fainali ambayo ndio malengo yetu kwa sasa,” amesema Aussems.
Aussems amesema wapo tayari kwa mchezo huo kwani michezo waliyocheza karibuni katika ligi imewasaidia kujiimarisha zaidi
Baada ya mchezo dhidi ya JS Saoura ugenini, Simba itarejea nyumbani kujiandaa na mchezo wa mwisho dhidi ya AS Vita utakaochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Machi 19
Kama Simba itashinda mchezo huo utakaopigwa saa nne usiku halafu AS Vita Club ikashindwa kuifunga Al Ahly kwenye mchezo wa mapema utakaopigwa saa moja usiku, basi mabingwa hao wa Tanzania watajihakikishia kuwa miongoni mwa timu nane zitakazotinga robo fainali