Leo jioni kikosi kitaondoka kuelekea nchini Algeria kwa kupitia Dubai, UAE ambako kitacheza mchezo wa tano wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya JS Saoura, mchezo ambao utachezwa siku ya Jumamosi Machi 9, 2019. Tuikumbuke timu yetu kwenye dua ili ifike salama na ifanye vizuri katika mchezo huo muhimu. #NguvuMoja
KAGERE Atoa NENO Kuelekea SIMBA vs JS SAOURA

Kagere amewataka mashabiki kuiombea na kuiunga mkono timu kwa hali na mali ili kuhakikisha inatinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa
“Nawaambia wote wenye mapenzi mema na Simba, wale wanaoamini kuwa tunaweza kutinga robo fainali, nusu fainali na hata fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa, waungane nasi kwa kutuombea ili tuweze kufanikiwa,” amesema Kagera katika ujumbe mfupi alioutuma kwa mashabiki wa Simba
Simba inatarajiwa kwenda Algeria siku chache zijazo tayari kwa mchezo huo dhidi ya JS Saoura utakaopigwa Jumamosi, March 09
NEYMAR : Kuhusu Kwenda Real Madrid
Neymar Jr on Madrid
Ratiba ya mechi ya leo Tpl
Ratiba ya mechi ya leo Tpl
Magazeti ya leo, Jumanne, March 05 2019















Michango yamkatisha tamaa Zahera
Akihojiwa na moja ya redio maarufu nchini, Zahera amesema amekuwa akijitoa kuisaidia Yanga na alitarajia Wana Yanga nao watafanya hivyo wakati huu ambao timu inapita katika kipindi kigumu lakini hali imekuwa tofauti
“Wanasema Yanga ni timu ya Wananchi lakini mbona wananchi hao hawaonekani kuisaidia timu?” alihoji Zahera
“Msimu huu hatukuwa na malengo ya kutwaa ubingwa, sababu iko wazi, kikosi chetu hakijakamilisha mahitaji ya kuweza kuwa mabingwa”
“Nilitegemea Wana Yanga watachangia timu kama tulivyopendekeza ili msimu ujao tuweze kuwa na kikosi imara zaidi”
“Lakini kwa hali inavyoendelea mimi sitakuwa tayari kufanya kazi kwenye timu ambayo haina malengo.”
“Sitakuwa tayari kuendelea kuwasaidia watu ambao wenyewe hawajisaidii”
Zahera amefanya kazi kubwa msimu huu ambapo licha ya mapungufu yaliyopo, ameweza kuiweka Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ikipoteza michezo miwili tu
Kocha huyo Mcongomani anataka kuiona Yanga inatoka katika ‘ukata’.
Pendekezo la kuwataka Wana Yanga waichangie timu yao ni moja ya njia za muda mfupi zinazoweza kuifanya Yanga ikasimama wakati ikiendelea kuandaa mikakati ya kuweza kujitegemea kama walivyo watani zao Simba
Hata hivyo muitikio mdogo wa Wana Yanga katika kutoa michango umemfanya kocha huyo akate tamaa na pengine huenda akaondoka mwishoni mwa msimu kama mambo hayatabadilika
Wadau wapendekeza Harambee ya kuichangia Yanga

Harambee hiyo inaweza kuandaliwa na kufanyika katika ukumbi utakaofaa ambapo utaratibu wa kutoa mwaliko kwa wadau wa Yanga unaweza kuandaliwa
Hapa waalikwe wananchi wa kawaida, watu maarufu, wafanyabishara, viongozi wa dini, viongozi wa Serikali kiufupi Yanga ina mtaji mkubwa wa watu, siku hiyo inaweza kutumika kuwaunganisha watu wote
Pia unaweza kuandaliwa utaratibu kwa tukio hilo kurushwa ‘mbashara’ katika runinga na redio mbalimbali ili wadau wengine ambao hawakualikwa waweze kushiriki kwenye Harambee hiyo kupitia vyombo vyao vya habari
Uchangiaji utafanyika ukumbini kwa kuwashirikisha wadau walioalikwa huku pia namba za kuchangia zikiendelea kutangazwa kwa wale wanaofuatilia kupitia vyombo vya habari ili waweze kuchangia
Utaratibu huu sio mgeni umekuwa ukitumiwa na watu binafsi na taasisi mbalimbali katika kuzishirikisha jamii zao linapokuja suala la uchangiaji wa fedha
RUGE KUPUMZISHWA LEO
Baada ya kuagwa jijini Dar es salaam, mwili wa Ruge ulisafirishwa jana Jumapili kuelekea Bukoba tayari kwa mazishi hayo
Wananchi wengi walijitokeza uwanja wa Ndege wa Bukoba katika mapokezi ya mwili wa Ruge ambaye enzi za uhai wake alikuwa mtu wa watu
Watu wengi wamesafiri kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania kwenda kumzika Ruge
Kabla ya ibada ya mazishi jioni ya leo, mwili wa Ruge utaagwa kwenye viwanja vya Ghymkhana kijijini Kiziru
Kagere apania kumpiku Aiyee

Leo Meddie Kagere anatarajiwa kuiongoza safu ya ushambuliaji ya Simba kwenye mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Stand United utakaopigwa uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga
Kagere mwenye mabao 12, yuko katika kiwango bora cha upachikaji mabao, akifunga mfululizo kwenye michezo mitano iliyopita
“Kazi yangu mimi ni kufunga, hivyo nitaendelea kufanya hivyo kila ninapopata nafasi ili niisaidie timu yangu iweze kupata ushindi,” alisema Kagere baada ya mazoezi ya jana
Kagere ndiye mchezaji hatari zaidi katika ligi kuu ya Tanzania Bara kwa sasa kutokana na kuwa na wastani mzuri wa kufunga kulingana na uwiano wa michezo aliyocheza
Full Time #UEFAASSIST
Full Time #UEFAASSIST









