Barcelona Legends


Barcelona Legends


Full Time #AfconU17
Klabu ya Simba Sc inatarajia kuanza kulifanyia kazi pendekezo la kocha wake Mkuu Patrick Aussems kuwania saini ya beki wa kushoto wa Yanga Sc Gadiel Michael ili kurithi mikoba ya Asante Kwasi ambaye anaonekana kuwa dhaifu kwasasa mbele ya Mohamed Hussein. .
.
Inasemekana klabu hiyo itaachana na Asante Kwasi na kwa mujibu wa kocha mkuu wa klabu hiyo amependekeza jina la Gadiel Michael kuchukua nafasi hiyo
.
.
Mkataba wa Gadiel na Yanga Sc unatarajia kumalizika mwishoni mwa msimu huu.
“Dunia ya soka kwasasa inajua Tanzania ilipo, shukrani pekee kwa Simba. Kila shabiki wa Simba inapaswa kujivunia timu yake. Tutarudi msimu ujao tukiwa imara zaidi.”- Kocha Patrick Aussems. #SIMBASC #NguvuMoja
Ratiba ya mechi za leo #TanzaniaPremierLeague

Uongozi wa Yanga umewataka viongozi wa Matawi kuwakumbusha wanachama wahakiki majina yao kwenye ‘ledger’ zilizo kwenye matawi yao
Wanachama wa Yanga pia wamekumbushwa kulipia ada za uanachama ili kuwa na sifa ya kuchagua viongozi katika uchaguzi utakaofanyika May 05
Uchaguzi utahusisha wanachama wote wenye kadi za kitabu na wale wenye kadi za posta.

Kutupwa nje ya michuano hiyo kwa Simba kuliibua shangwe kubwa miongoni mwa mashabiki wa Yanga na hii inatokana na Simba kutumia mafanikio yao msimu huu ‘kuwanyanyasa’ watani zao Yanga ambao wanapita katika kipindi kigumu
Ten amesema Yanga na Simba ni watani wa jadi hivyo ni vyema wakavumilia matani wanayokutana nayo mtaani kwani na wao wamekuwa wakifanya hivyo wakati wote ambao Yanga inakumbwa na changamoto
“Ndiyo Sisi na ninyi ni watani na tunataniana kweli hasa timu zetu zinapokosa matokeo,” ameandika Ten kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram
“Bahati mbaya ni kwamba ninyi mnapenda kutania wenzenu lakini mkitaniwa ninyi ‘Nongwa’ mnahamia kwenye kashfa..! Mkikashifiwa nanyi mnaanza kulialia”
“Hongereni kwa hatua mliyofika, muhimu ni kuangalia wapi mmekosea ili mfanikiwe zaidi siku za usoni”
“Wakati sisi tunajiuliza nanyi mjiulize zaidi. Msimvuruge @moodewji ili aendelee kuwabeba..!”
Aidha Ten amewakaribisha Simba kwenye ligi kuu huku akiwatupia ‘dongo’ kuwa mitandao yao ya simu itakuwa imejaa tayari kwa kufanya miamala
“La huko limeisha, mrudi bongo sasa najua simu zenu zina line mbili mbili yaani full network kama siyo Mpesa basi Tigopesa…!”
Baada ya kutolewa Simba inarejea kwenye ligi ikikumbana na rundo la ‘viporo’ ambavyo watatakiwa wavimalize ndani ya kipindi cha mwezi mmoja
Katika kipindi hicho Simba wanapaswa kucheza michezo 16 kwani ligi imepangwa kumalizika mwishoni mwa mwezi wa tano ili kupisha maandalizi ya timu ya Taifa ambayo mwezi Juni inaelekea Misri kushiriki fainali za AFCON 2019

Tanzania ni mwenyeji wa michuano hiyo inayoanza kutimua vumbi leo katika viwanja vya Azam Complex na Taifa
Nahodha wa kikosi cha Serengeti Boyz Morris Michael amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi uwanja wa Taifa watakapokuwa wakiikabili Nigeria leo
“Nimezungumza na wenzangu na kuwashusha presha kwamba tunaenda kucheza mchezo wa kawaida kama michezo mingine ambayo tumecheza, kwa hiyo tuuone wa kawaida,” amesema
“Ni mechi kubwa lakini hatutakiwi kuwa na presha, tunatakiwa kupambana hadi mwisho kupata ushindi.”
“Tukishinda mchezo huu tutapata picha nzuri ya matarajio yetu hapo mbele tofauti na tukipoteza au kupata sare.”
“Watanzania waje kutuunga mkono kwa sababu tupo nyumbani naamini tutafanya kitu ambacho watanzania hawataamini”
Viingilio vya mchezo huo VIP ni Tsh 5,000/- na upande wa mzunguuko ni Tsh 2,000/-

Simba ilitolewa kwenye michuano hiyo jana katika hatua ya robo fainali baada ya kufungwa mabao 4-1 na TP Mazembe
Makonda amesema matokeo hayo hayapaswi kuwavunja moyo bali iwe chachu ya kutafuta mafanikio zaidi
Aidha Makonda amempongeza mlinda lango namba moja Aishi Manula kwa kazi kubwa aliyofanya kwenye mchezo dhidi ya TP Mazembe akiahidi kumpa zawadi
“Najua matokeo ya leo (jana) yatatupa tabu sana mtaani ila wewe (Manula) umekuwa nyota wangu ukifika tu DSM njoo uchukue zawadi yako,” amesema
“Watani zangu Naomba mjuwe hatua tuliyofikia ni kubwa sana na hakika Simba inastahiri kupongezwa na Usku nitakuwepo Airpot kuwapokea Makamanda na wapambanaji wetu Simba”

Tanzania ni mwenyeji wa michuano hiyo inayoanza kutimua vumbi leo katika viwanja vya Azam Complex na Taifa
Nahodha wa kikosi cha Serengeti Boyz Morris Michael amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi uwanja wa Taifa watakapokuwa wakiikabili Nigeria leo
“Nimezungumza na wenzangu na kuwashusha presha kwamba tunaenda kucheza mchezo wa kawaida kama michezo mingine ambayo tumecheza, kwa hiyo tuuone wa kawaida,” amesema
“Ni mechi kubwa lakini hatutakiwi kuwa na presha, tunatakiwa kupambana hadi mwisho kupata ushindi.”
“Tukishinda mchezo huu tutapata picha nzuri ya matarajio yetu hapo mbele tofauti na tukipoteza au kupata sare.”
“Watanzania waje kutuunga mkono kwa sababu tupo nyumbani naamini tutafanya kitu ambacho watanzania hawataamini”
Viingilio vya mchezo huo VIP ni Tsh 5,000/- na upande wa mzunguuko ni Tsh 2,000/-