Hazard siwez lazimisha kuvaa jezi number 10 wala kupiga penati

credit: @sokawaytz…

– Eden Hazard amesema kuwa yeye hajali juu kutovaa jezi namba 10 au kutokuwa na majukumu ya kupiga mikwaju ya penalti katika Klabu yake mpya ya Real Madrid; Mshambuliaji huyo wa Kimataifa wa Ubelgiji alijiunga na Blancos kwa €100 (£88m / $112m) kutoka Chelsea wiki iliyopita.

.

— “Nimezungumza na Modric kwa kupitia kwa Kovacic, nikamuuliza kama angeweza kuniachia Mimi jezi No.10, alisema hapana, ni lazima nitafute namba nyingine,” alisema Hazard.

.

— Nyota huyo Pia aliongeza kuwa “Kwangu mimi namba 10 ya jezi si muhimu, lakini kucheza na jezi hii, na nembo hii inatosha”.

.

– Hazard pia amesema hatolazimisha kutaka kuchukua penati ili apige yeye ndani ya Real Madrid, kwani kawakuta wapiga wengine wengi wa penati ndani ya Klabu… Sergio Ramos msimu uliopita alipiga penati Nane Kati ya 12 za Klabu hiyo, Karim Benzema akipiga penati tatu na Gareth Bale akipiga penati moja..

#Updates

@Sokawaytz

Kibabage amfuata Msuva difaa Morocco

credit: @simbamakini…

KIBABAGE AMFUATA MSUVA DIFAA

Mlinzi wa kushoto wa Mtibwa Sugar, Nickson Kibabage amesaini mkataba wa miaka minne kuitumikia klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco ambayo anachezea Mtanzania, Simon Msuva.

Kibabage aling’ara na kuonekana akiwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ kilichoshiriki michuano ya Afcon nchini Gabon mwaka 2017.

Source: Boiplus Media

Messi ndiye mwana michezo anayelipwa pesa nyingi duniani

credit: @sokawaytz…

– Mshambuliaji wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi ndiye Mwanamichezo anaelipwa mkwanja zaidi duniani, akijiingizia $127m (£99.8m) katika miezi 12 iliyopita, kulingana na takwimu zilizo tolewa na Forbes; Nyota wa Juventus ya Ureno, Cristiano Ronaldo ni wa pili akijiinguzia $109m (£85.6m) na Mbrazili wa Paris St-Germain, Neymar anafuatia wa tatu kwa $105m (£82.5m).

.

– Kinara wa mwaka jana alikuwa ni Mwana masumbwi, Floyd Mayweather ambaye ameshuka katika orodha hii; Mcheza Tennis, Serena Williams ni mwanamke pekee aliye juu top 100, akipata dola 29.2m (£22.9m)…Bingwa Mara tano wa Dunia wa mbio za Magari ya Langa langa “Formula 1”, Lewis Hamilton na bingwa wa zamani wa uzito wa Juu katika Ndondi, Anthony Joshua ndio wanaopata mkwanja Mrefu Kama Wanamichezo wa Uingereza wakiwa nafasi ya 13 wakijiinguzia $55m (£43.2m).

.

– Gazeti hilo La biashara la Marekani limehesabu mapato ya wanamichezo na kuongeza fedha zao za mshahara kati ya Juni 2018 na Juni 2019.. Top 100 ni pamoja na wanamichezo kutoka nchi 25 na $4bn (£3,1bn) ndio mapato yao kwa pamoja yakiongezeka kwa 5% kutoka mwaka uliopita, wakati Mayweather alikuwa kinara mwa $285m (£224m).

.

– Messi ni Mchezaji wa Soka wa nane tofauti kuchukua nafasi ya kwanza katika Orodha hii ambapo takwimu zake zilianza rasmi mwaka 1990.. Pia ni mara ya kwanza kwamba ni wanasoka wote wameshikilia tatu bora…Messi ni mmoja Kati ya Wanamichezo 38 wasiokuwa Raia wa kwenye orodha… Paul Pogba kiungo wa Manchester United ni mchezaji Anaeongoza kutoka Ligi Kuu Uingereza akiwa katika nafasi ya 44 akijiingizia $33m (£25.9m).

✋🏻 TOP 10 inasimama hivii

1. Lionel Messi $127m (£99.8m)

2. Cristiano Ronaldo $109m (£85.6m)

3. Neymar $105m (£82.5m)

4. Canelo Alvarez $94m (£73.8m)

5. Roger Federer $93.4m (£73.3)

6. Russell Wilson $89.5m (£70.3m)

7. Aaron Rodgers $89.3m £70.1m)

8. LeBron James $89m (£69.9m)

9. Stephen Curry $79.8m (£62.7m)

10. Kevin Durant $65.4m (£51.3m)..

#Updates #forbessportsmoney #forbes

@Sokawaytz

Misri yaichakaza stars 1-0

credit: @sokawaytz…

FULL-TIME; Kutoka Dimba La Borg El Arab.. Wenyeji Misri wanaibuka na Ushindi Mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania.. Ulikuwa ni Mchezo wa kutest Mitambo, game nzuri imemalizika salamaa… Taifa Stars kabla ya kuanza kibarua cha AFCON watacheza game nyingine ya kirafiki dhidi ya Zimbabwe..

:

Misri 🇪🇬 1-0 Tanzania 🇹🇿

#PreAfcon #TotalAFCON2019 #EGYTAN

Stars yaanza na Senegal Afcon

credit: @sokawaytz…

– Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Emmanuel Amunike, amesema kuwa anaamini kuwa kushinda mechi ya ufunguzi katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika “AFCON” zitasababisha mafanikio kwenye Mashindano hayo kwani kutakuwa na nguvu ya kushinda mechi zinazofuata.

.

– Taifa Stars Imepangwa kuanza na Senegal katika Mchezo wa kwanza wa Kundi la C na legend huyo wa Nigeria anaamini matokeo ya ushindu yataamua muendelezo wa timu katika mashindano huko Misri.

:

🗣 “Tutafungua kampeni yetu ya AFCON dhidi ya Senegal. Kwangu mimi, Senegal ni timu bora Afrika hadi sasa ina wachezaji wengi wazuri, lakini bado tuna wachezaji wetu wazuri ambao wanaweza kuleta matokeo yaliyoridhisha”.

.

🗣 “Unapoingia katika mashindano haya, unapaswa kupata matokeo mazuri ya kwanza ili upate na hakika ya kufanya vizuri na hivyo ndio tutakavyolenga dhidi ya Senegal, kushinda mechi yako ya kwanza katika Mashindano yoyote husaidia sana kuimarisha timu mbele ya mechi nyingine zinazokuja” Amunike aliwaambia Waandishi wa Habari kambini jijini Aleksandria..

#Updates

@Sokawaytz