FIFA wamebariki Qatar kuwa mwenyeji wa World Cup 2022 kwa timu 32 sio 48

Shirikisho la soka Ulimwenguni FIFA limetangaza kuwa imelazimika kuacha michuano ya World Cup 2022 itakayofanyika nchi Qatar kuwa na timu 32 na sio 48 kama ambavyo ilikuwa inatarajiwa awali, taarifa hizo rasmi zitatolewa June 5 2019 katika mkutano wa FIFA Paris Ufaransa.
Inaelezwa kuwa Qatar wamekuwa wakijipanga kuwa wenyeji wa timu 32 toka 2010 na hata maandalizi yao yalikuwa yanalenga kutumia viwanja nane vilivyoandaliwa tayari, hivyo kwa miaka mitatu iliyosalia Qatar hawezi kumudu ongezeko la timu kutoka 32 yaliokuwa matarajio yao hadi 48.

Rais wa FIFA Infantino

Hata hivyo wazo la timu 48 linabakia kuwa kama wazo litakaloanza kufanya kazi rasmi 2026 katika fainali za Kombe la Dunia litakalokuwa na wenyeji watatu United States, Canada na Mexico, sababu za kisiasa ndio zimeleta utata kwa Qatar kukubali ongezeko la timu na kuwa mwenyeji kwa ushirikiano na mataifa jirani.

Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amethibitisha kuwa ataondoka KRC Genk mwishoni mwa msimu huu

⚽Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amethibitisha kuwa ataondoka KRC Genk mwishoni mwa msimu huu, na kwamba klabu 6 za Uingereza na 2 za Hispania zinataka kumsajili, lakini amesema ndoto yake ni kucheza Uingereza.
. .. . . 👉Msimu huu @samagoal77 ameifungia Genk jumla ya magoli 32.

Mwinyi Zahera amewapongeza wachezaji wa timu hiyo kwa kufanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City

Licha ya kuwakosa wachezaji saba wanaougua Malaria, kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amewapongeza wachezaji wa timu hiyo kwa kufanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City

Zahera amesema katika mchezo wa leo alitumia wachezaji wanne kutoka katika kikosi cha U20

“Tulikosa wachezaji wetu saba wanaumwa Malaria, nimetumia vijana wanne wa U20, nafurahi wachezaji wameweza kutupatia matokeo,” amesema

“Tulitengeneza nafasi nyingi, tulipaswa kufunga mabao zaidi, nafikiri leo hatukuwa na nidhamu ya mchezo”

Kuhusu maoni yake baada ya Simba kutwaa ubingwa jana, Zahera ameshikilia msimamo wake kuwa hawakustahili kutwaa ubingwa kutokana na upindishwaji mkubwa wa sheria uliofanywa kuwawezesha washinde taji hilo

“Simba waliwapa ubingwa jana, maoni yangu mie nilicheza mpira ambao uko na sheria, ule sio ubingwa,” amesema

“Ninapoishi nakaa na watu wa Simba, wananiambia kweli hata kama mpira wetu tunapenda Simba, tunaona kama sio hivyo”

“Tunapata kikombe lakini ukiangalia sheria kabisa mwaka huu hatungepata kikombe”

Wadau mbalimbali wametoa maoni tofauti juu ya ubingwa wa Simba

Wakati wengine wakiamini kuwa Simba ilistahili ubingwa huo, wapo wanaoamini mazingira yaliyotengenezwa na TFF kwa kuiacha timu hiyo isicheze mpaka michezo 12 wakati nyingine zikiendelea na ligi, yameirahisishia timu hiyo kutwaa ubingwa

“Simba walikuwa na michezo 12 ya viporo. Walikuwa wanafahamu matokeo ambayo wanatakiwa wapate ili watwae ubingwa, pengine hali ingekuwa tofauti kama wangecheza sambamba na timu nyingine,” amesema Rajabu Issa kutoka Buguruni

“Umeona wapi na ligi gani duniani ambapo timu moja inakuwa na michezo ya viporo 12? kushiriki ligi ya mabingwa haitoshi kuwa sababu ya kurundikiwa michezo mingi kiasi hicho mbona timu walizokuwa wakishindana nazo zilikuwa zikicheza ligi zao?”

“Hawa Simba baada ya kutolewa kombe la FA walipanga mkakati na TFF kuhakikisha wanatwaa ubingwa wa ligi kuu kupitia ratiba na hujuma kwa Yanga”

“Angalia mchezo dhidi ya KMC ilikuwa wafungwe lakini refa akawatafutia ushindi kwa nguvu halafu baadae TFF wanatangaza kumfungia mwamuzi wakati mpango umeshakamilishwa”

Simba kuweka kambi Marekani au Ureno Pre- Season

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji amesema kuwa bodi ya wakurugenzi imepanga kuipeleka timu hiyo Marekani au Ureno kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na Mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Dewji alisema hayo wakati wa kuipongeza timu hiyo kutwaa ubingwa kwa mara ya pili mfululizo na zoezi wapi watakwenda itajadiliwa ndani ya wiki hii.

Alisema kuwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mara mbili mfululizo ni mafanikio makubwa ambayo yametokana na ushirikiano baina ya viongozi, wanachama, mashabiki na wadau wa soka kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Dewji, Ligi Kuu ilikuwa ngumu na hasa baada ya klabu ya Yanga ilikuwa inaongoza ligi hiyo kwa pointi 21.

“Haikuwa kazi rahisi kutafuta pointi ambazo wapinzani wetu wameweza kupata. Wachezaji waliweza kupigana kiume mpaka kupata ushindi wakiwa na mechi mbili mkononi.

FT: Yanga 1-0 Mbeya City

Yanga imeendeleza umwamba wake katika dimba la Uhuru baada ya kuichapa Mbeya City bao 1-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara mzunguuko wa 37

Bao pekee la Yanga lilipatikana kwenye dakika ya 26 likiwekwa kimiani na Heritier Makambo aliyeunganisha kwa kichwa krosi ya Haji Mwinyi

Hilo ni bao la 17 kwa Makambo, akishika nafasi ya pili sawa na Salim Aiyee katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu nyuma ya Meddie Kagere wa Simba mwenye mabao 23

Licha ya kuwakosa nyota wake wengi ambao ni wagonjwa na majeruhi, Yanga ilitandaza kandanda safi na kutawala mchezo huo kwa muda mwingi

Kiungo kinda Gustapha Simon ameendelea kudhihirisha ubora wake, hakuna shaka msimu ujao atapata nafasi zaidi kwenye kikosi cha Zahera

Yanga imefikisha alama 86 sasa ikibakiwa na mchezo mmoja wa kumaliza msimu dhidi ya Azam Fc

Mchezo huo utapigwa May 28 2019

MO DEWJI

“Niwapongeza na kuwashukuru wachezaji wamejitolea kwa namna moja au nyingine hadi tunaupata huu ubingwa, niwashukuru wanachama na wapenzi wote wa Simba kwa kujitokeza kutushangilia.”- Mo Dewji
.

“Kocha ameshafikia malengo tuliyomuwekea tulikuwa tunataka ubingwa na kufika kwenye makundi ya Ligi ya Mabingwa, Mungu akitujalia kwenye wiki moja tutakaa nae tumuongeze mkataba … tutamueleza sehemu ambazo kuna mapungufu ili aendelee kufanyia kazi”- Mo Dewji
.
“Tunaanza kupanga maandalizi ya msimu, mimi binafsi naongea na timu za Ulaya na Marekani… kuna rafiki yangu anamiliki DC United nimeongea nae watualike tukafanye maandalizi Marekani, kuna uwezekano wa kwenda Ureno, kwenye wiki mbili zijazo tutajua timu itakwenda wapi”- Mo Dewji
.

“Kwenye mechi ambayo tutacheza kesho naomba niwashukuru sana SportPesa, hii ni mara ya kwanza kwa timu kutoka ligi kuu ya Hispania kuja kucheza Tanzania, ni historia kubwa kwa nchi yetu, tupo tayari kucheza na Sevilla, naomba mashabiki tujitokeze kwa wingi sana”- Mo Dewji
.
“Simba itakuwa kwenye soko kushindinda na Al Ahly, Zamalek, TP Mazembe kushindana kutafuta wachezaji wenye vipaji, tupo tayari kuwabakisha wachezaji ambao mwalimu atapendekeza, wengine watatoka kwa mkopo … bajeti ya mwaka huu itakuwa kubwa kuliko mwaka jana”- Mo Dewji
.

“Katika mechi ya kesho ya Sevilla nawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi ili na sisi tuweze kuwaonyesha mpira wa Ulaya”- Mwenyekiti wa klabu, Swedi Mkwabi.
#NguvuMoja #SportPesa Challenge #TukutaneMei23

MO DEWJI: Apongeza UBINGWA – SIMBA, Aweka wazi Mipango ya Msimu UJAO

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewapongeza wachezaji, viongozi na mashabiki wa timu baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mo amesema ubingwa huo matokeo ya ushirikiano na umoja ulioonyeshwa na Wanamsimbazi tangu mwanzoni mwa msimu

Aidha Mo amesema shamrashamra za ubingwa zitafanyika May 25 wakati timu hiyo itakabidhiwa kombe katika mchezo dhidi ya Biashara United

Katika hatua nyingine Mo ameipongeza Yanga kwa kuipa changamoto Simba katika mbio za kuwania ubingwa.

Amewapongeza viongozi wapya wa timu hiyo na kuwataka waimarishe timu yao ili iweze kuipa changamoto zaidi Simba kwani anaamini uimara wa timu zote utaongeza ubora wa soka la Tanzania

Aussems kuendelea kuinoa Simba

Mo amesema baada ya kocha Mkuu Patrick Aussems kutimiza masharti yote ya mkataba wake, wanakusudia kumpa mkataba mpya

Mwaka jana Aussems aliposaini mkataba wa mwaka mmoja, alipewa masharti mawili ambapo moja ni kutwaa ubingwa wa ligi kuu na la pili ni kutinga hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Maboresho ya kikosi

Mo amesema Aussems leo atawasilisha ripoti ya maboresho ya Simba kwa ajili ya msimu ujao.

Aussems atapendekeza wachezaji ambao anataka waachwe/watolewe kwa mkopo pia kocha huyo anatakiwa kupendekeza wachezaji ambao anataka wasajiliwe

Mo amesema wamedhamiria kuifanya Simba iwe imara mara dufu ili kuhakikisha inafanya vizuri zaidi kwenye michuano ya CAF msimu ujao

Amesema watashindana na vilabu vikubwa barani Afrika kama Al Ahly, TP Mazembe, Zamalek nk katika kuwania wachezaji wazuri

Kuhusu Kambi

Kama ilivyokuwa msimu uliopita, Mo amesema msimu huu Simba itaweka kambi barani Ulaya katika nchi ya Ureno au nchini Marekani

HAJI MWINYI: Ajiandaa na Maisha Nje ya YANGA

Beki Haji Mwinyi ni miongoni mwa wachezaji wa Yanga ambao mikataba yao inamalizika baada ya mchezo wa mwisho wa ligi

Beki huyo aliyeitumikia Yanga kwa zaidi ya miaka minne, atakuwa huru baada ya Yanga kuumana na Azam Fc wiki ijayo

Amezikaribisha timu zinazohitaji huduma yake kwa ajili ya msimu ujao

“Mkataba wangu na Yanga unamalizika msimu huu. Baada ya hapo nitakuwa huru”

“Nakaribisha klabu yeyote inayohitaji huduma yangu kwa msimu ujao waje tukae mezani tuzungumze, lakini kuhusiana na ofa nilizonazo mezani hadi sasa siwezi kuweka wazi hadi hapo nitakapomaliza msimu wangu kwa michezo miwili iliyobaki,” Mwinyi aliiambia Mwanaspoti

“Sikuwa na namba kikosi cha kwanza, lakini hiyo haina maana kwamba kiwango changu kimeshuka, nipo vizuri na nina uwezo wa kupambana. Kutokana na uzoefu nilionao na naweza kucheza timu yeyote”

Haji Mwinyi hakuwa na wakati mzuri msimu huu katika kikosi cha Zahera akishindwa kutamba mbele ya Gadiel Michael aliyekuwa chaguo la kwanza

Yanga imepanga kutowaongezea mikataba wachezaji ambao hawakucheza angalau nusu ya michezo ya ligi kuu msimu huu