BOSS – SEVILLA Aipongeza Simba kutwaa UBINGWA

Timu ya Sevilla imewasili nchini usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Simba utakaopigwa kesho Alhamisi, saa moja jioni katika uwanja wa Taifa

Katika Mkutano na Waandishi wa habari leo, Rais wa Sevilla Jose Castro ameeleza kufurahia ujio wao hapa nchini hasa ikizingatiwa wao wanakuwa timu ya kwanza kutoka Hispania kucheza Tanzania

Aidha ameipongeza Simba kwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara

“Niwapongeze sana Simba ya Tanzania kwa kuchukua ubingwa wa ligi Kuu, tumekuja kucheza na timu bora. Ni heshima sana kuja Tanzania na bila shaka tutakua ni timu ya kwanza ya Laliga kuja Tanzania,” amesema

Wakati Sevilla ikiwa tayari imewasili, wapinzani wao Simba nao watatua leo kutoka mkoani Dodoma baada ya kufanikiwa kutetea ubingwa wa ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo

YANGA DIMBANI LEO KUIVAA MBEYA CITY

Kikosi cha Yanga leo kinashuka uwanja wa Uhuru kuikabili Mbeya City katika mchezo wa ligi kuu raundi ya 37

Baada ya Simba kutwaa ubingwa hapo jana, mchezo huo ni wa kukamilisha ratiba tu ambapo mabingwa hao wa kihistoria watakuwa wakilinda heshima yao

Jana Yanga ilifanya maandalizi ya mwisho kwenye uwanja wa Uhuru
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema lengo lao ni kumaliza ligi kwa kushinda michezo yote miwili iliyobaki
Ushindi katika michezo miwili iliyobaki utawafanya wafikishe alama 89 ambazo hata hivyo tayari zimeshapitwa na Simba yenye alama 91

Lakini pia hata kama Yanga itapoteza michezo yote iliyobaki, itaendelea kubaki nafasi ya pili kwani hakuna timu nyingine inayoweza kufikisha alama hizo
Yanga leo inatarajiwa kuwakosa wachezaji saba ambao wanaugua Malaria

Hata hivyo Zahera amesema wachezaji watakaopata nafasi ya kucheza, anaamini wataweza kuipa timu hiyo ushindi
Baada ya mchezo wa leo, Yanga itashuka tena dimbani wiki ijayo May 28 kumaliza msimu kwa kuumana na Azam FC

ZAHERAC: Amlilia AJIBU Kwenda TP MAZEMBE

Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga, Mwinyi Zahera amemwambia nahodha na mshambuliaji wa klabu hiyo Ibrahim Ajibu kufikilia mara mbili kuhusu kuihama klabu hiyo mwisho wa msimu huu. Imeelezwa.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Zahera amedai Ajibu ni kiongozi wa wenzake na hapaswi kuwa na mawazo ya kuondoka Yanga na kuwaacha wenzake.

Mkataba wa Ajibu na Yanga unaisha mwisho wa msimu huu na inadaiwa kuwa atajiunga na klabu ya Simba baada ya mkataba wake kuisha na Yanga.

Taarifa za Ajibu kuondoka Yanga zimeanza muda mrefu uliopita na kuleta sintofahamu kwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kutokana na namna mwenendo wa klabu ulivyo.

Zahera amemuomba Ajibu afikirie zaidi ya mara moja kuhusiana na kuondoka kwake kwa manufaa ya Yanga maana anaheshimu mchango wake.

AJIBU Kutimkia TP MAZEMBE

TP Mazembe itamsajili kiungo wa Yanga Ibrahim Ajib Migomba akitarajiwa kujiunga na timu hiyo Julai 01 2019

TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuitaarifu juu ya nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo.

Mazembe itamsajili Ajib baada ya kumaliza mkataba na Yanga

Aidha TP Mazembe imeiomba Yanga impe ruhusa ya siku tatu wiki hii ili aweze kwenda Congo kukamilisha taratibu za usajili

Hii ni habari njema kwa Ajib ambaye msimu huu umekuwa mzuri sana kwake

Ajib ameifungia Yanga mabao sita na kutengeneza mabao 17 kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara inayoelekea ukingoni

SEVILA YAWASILI BONGO

Kikosi cha Sevilla kimewasili jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa Tanzania Bara Simba

Sevilla ilikaribishwa nchini kwa burudani ya Msanii maarufu Mrisho Mpoto ‘Mjomba’ aliyetumbuiza uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati timu hiyo ilipowasili

Wapinzani wao Simba wanatarajiwa kurejea leo Dar kutoka mkoani Singida ambako jana walitwaa ubingwa wa ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo baada ya kuifunga Singida United mabao 2-0

Baada ya mchezo jana, Simba ilielekea mkoani Dodoma ambako leo inatarajiwa kuunganisha kwa usafiri wa Ndege kurudi jijini Dar es salaam

IBRAHIM AJIBU AMALIZANA NA TP MAZEMBE.

Nahodha wa Klabu ya Yanga SC, Ibrahim Ajib anatarajia kujiunga na Mabingwa wa DR Congo, Miamba wa Lubumbashi Klabu ya TP Mazembe kwa uhamisho huru Baada ya Mkataba wake na Klabu yake ya Jangwani kufikia tamati mwishoni mwa mwezi Ujao.. 👏👏👏.
#transfers
.

Klabu ya TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuwaeleza kuwa wamefanya makubaliano ya kuingia mkataba na Ibrahim Ajibu utakaoanza rasmi Julai 1.

Hiyo ni baada ya Mazembe kujiridhisha kuwa mkataba wa mchezaji huyo na Yanga unaisha Juni 30.

Taarifa hii inaua matumaini ya Wanajangwani hao kuendelea kuwa na fundi huyo wa mpira msimu ujao huku ikizima tetesi za kurejea Simba.

#TransferUpdates