– Kiungo wa Kimataifa wa Rwanda na Klabu ya @simbasctanzania ameendelea kuweka rekodi zake ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara kuwa Mchezaji wa kigeni kutwaa Makombe mengi zaidi ya Ligi Kuu Tanzania Bara; Baada ya kunyakua Ubingwa wa msimu huu 2018/19, Niyonzima Sasa kabeba Ubingwa Mara tano mfululizo Pia kwa jumla ni Mara ya Sita anatesa Ubingwa wa Tanzania 🇹🇿 akiwa na vilabu viwili tofauti na vikongwe nchini.
🏆2012/13 (Yanga)
🏆2014/15 (Yanga)
🏆 2015/16 (Yanga).
🏆 2016/17 (Yanga).
🏆 2017/18 (Simba).
🏆 2018/19 (Simba).
.
– Licha ya Bongo tu, Niyonzima Ana medali tatu za Ubingwa wa Kwao Rwanda 🏆 2008/9, 🏆 2009/10, 🏆 2010/11… Medali tatu za Ubingwa wa Kombe La FA kwao Rwanda 🏆 2007/8, 🏆 2009/10, 🏆 2010/11 na Medali Moja ya Ubingwa wa Kombe La FA nchini 🏆 2015/16.
#LigiKuuTanzaniaBara #TPL
@Sokawaytz
Category: michezo
YANGA: Kuisimamisha DAR June 15
Harambee kubwa ya kuichangia Yanga itafanyika Juni 15 katika ukumbi wa Diamond Jubelee jijini Dar es salaam
Siku hiyo ndio itakuwa kileleni cha kampeni ya kuichangia Yanga iliyoanza takribani miezi miwili iliyopita
Wananchi wa kawaida, Wasanii, Wanamuziki, Wabunge, viongozi wa Serikali,Taasisi Binafsi na Mashirika watahudhuria hafla hiyo ambayo Kamati ya Hamasa inakusudia kukusanya zaidi ya Tsh Milioni 500

Mwana Jangwani weka kumbukumbu ya tarehe hiyo….!
YANGA : Wachezaji wagonjwa
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wachezaji saba wa kikosi cha Yanga hawataweza kucheza kesho mchezo dhidi ya Mbeya City baada ya kukumbwa na Malaria
Wachezaji hao ambao hawakufika kufanya mazoezi yaliyofanyika uwanja wa Uhuru leo ni pamoja na Abdallah Shaibu, Andrew Vicent, Juma Abdul, Haji Mwinyi, Said Makapu, Mohammed Issa na Paulo Godfrey
“Nadhani timu yetu imekumbwa na janga la Malaria, tuna wachezaji karibu saba ambao wanaugua Malari,” amesema Zahera
“Sijui ni kama walikula nini sijui”
Akizungumzia mchezo wa kesho, Zahera amesema hautakuwa mwepesi kutokana na ubora wa kikosi cha Mbeya City
“Tuliwafunga mchezo wa kwanza, lakini wachezaji ilibidi wajitume sana kuweza kupata matokeo,” amesema
“Kesho pia mchezo hautakuwa tofauti lakini nafurahi wachezaji wangu wamepata muda mrefu wa kupumzika hivyo watakuwa ‘fresh'”
“Kwa wale watakaocheza lengo letu ni moja, tumalize mechi mbili zilizobaki kwa kuibuka na ushindi”
SHAMRASHAMRA ZA UBINGWA NAMFUA
Baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida United, wachezaji wa Simba walizianza shamrashamra za kutwaa ubingwa wa pili mfululizo katika uwanja wa Namfua
Picha za matukio ya sherehe za ubingwa;







MO DEWJI APONGEZA UBINGWA SIMBA
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ ameipongeza timu hiyo kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara kwa msimu wa pili mfululizo
Mo amesema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na juhudi zilizofanywa na wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na wadau wote wa klabu ya Simba kila mmoja kwa nafasi yake
“Mungu mkubwa. Pongezi kwa wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, wanachama, mashabiki, na wapenzi wote wa SIMBA, tumeshinda! Najivunia mafanikio haya,” amesema Mo
Naye Msemaji wa Simba Haji Manara amewapa shukrani za kipekee wachezaji, benchi la ufundi pamoja na mashabiki wa timu hiyo kwani wamekuwa na mchango mkubwa kwa mafanikio ya Simba msimu huu
“Tumshukuru Mungu muweza aliyetaka Simba iwe Bingwa tena”
“Tuwapongeze sana Wachezaji wetu wote, Benchi la ufundi chini ya kocha Patrick Aissems, lakini kipekee tuwashukuru nyie Wanachama na Washabiki wetu ambao mimi nnaamini ndio chachu ya huu ubingwa”
“Kwangu shujaa wa kwanza Simba ni Mshabiki wetu, Tunawashukuru sana”
Simba imetwaa ubingwa leo baada ya kuifunga Singida United mabao 2-0
Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa baada ya kufikisha alama 91 kwenye msimamo wa ligi
Alama hizo haziwezi kufikiwa na timu nyingine yoyote katika michezo iliyobaki
Simba imeibuka na ubingwa huku ikiwa na michezo miwili mkononi
BREAKING NEWS: SIMBA WATWAA UBINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA 2018/2019
SIMBA BINGWA LIGI KUU TANZANIA 2018/2019
Simba imefanikiwa kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Singida United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Namfua
Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa wake wa 20
Simba imefikisha alama 91 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine hata kama zitashinda michezo yote iliyobaki

Wachezaji, benchi la Ufundi na viongozi wa Simba wanastahili pongezi kwa mafanikio haya ya kikosi cha Simba
Ubora wa timu, ushirikiano baina ya Wana Msimbazi ndio sababu kubwa iliyopelekea kuibuka na ubingwa wa pili mfululizo
Msimu haukuwa mwepesi kutokana na Simba kushiriki katika mashindano mengi, lakini juhudi za wachezaji zimewezesha kupatikana kwa mafanikio haya
Simba imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao, mashindano ambayo tayari imepata uzoefu mkubwa msimu baada ya kufika hatua ya robo fainali
Hongera Wachezaji, Hongera Benchi la Ufundi, Hongera Viongozi, Hongera Mashabiki wa Simba……!
Kikosi ambacho kitaanza leo dhidi ya Singida United.
Kikosi ambacho kitaanza leo dhidi ya Singida United. #NguvuMoja #SportPesaChallenge #TukutaneMei23 #TPL


SHEREHE ZA UBINGWA SIMBA KUANZA LEO SINGIDA
Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wako mkoani Singida ambapo leo watashuka katika uwanja wa Namfua kuikabili Singida United katika mchezo ambao huenda wababe hao wa soka la Tanzania watatawazwa mabingwa
Simba inayoongoza ligi ikiwa na alama 88, inahitaji alama moja tu katika mchezo huo ili iweze kurudi na kombe jijini Dar es salaam
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wataingia katika mchezo huo kusaka ushindi ingawa wanafahamu pointi moja itatosha kutimiza lengo la kutwaa ubingwa
“Tuko hapa kwa ajili ya kusaka ushindi, Nawakaribisha mashabiki wetu waje kwa wingi uwanjani kutuunga mkono ili tuweze kutimiza lengo la kutwaa ubingwa leo,” amesema Aussems
SEVILLA : Kutua Na Msafara wa watu 60
Timu ya Sevilla kutoka Hispania inatarajiwa kuwasili leo ikiwa na msafara wa watu 60 unaojumuisha wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa timu hiyo
Sevilla ambayo itacheza na Simba mchezo wa kirafiki keshokutwa, ikiwa nchini itashiriki katika shughuli za kijamii
Safari ya Sevilla nchini imedhaminiwa na kampuni a SportPesa ambao pia ni wadhamini wakuu wa timu za Simba na Yanga
Mabingwa hao wa kihistoria wa taji la Europa, wanakuwa timu ya kwanza kutoka ligi kuu ya Hispania kutembelea Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla
Sevilla iliyotwaa taji la Europa mara tano, itacheza na Simba keshokutwa Alhamisi, May 23 katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa, saa moja jioni









