
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Yanga jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa timu hiyo Dk Mshindo Msolla amesema tayari uteuzi umeshafanyika kwa sasa wanafanya majadiliano na wajumbe walioteuliwa kabla ya kuwaweka hadharani
“Wajumbe wa Kamati hiyo tumeshawateua lakini hatuwezi kuwatangaza kabla nao hawajaridhia,” amesema Dk Msolla
“Wiki ijayo tutakuwa na kikao na benchi la Ufundi, pengine katika kikao hicho tutaitangaza Kamati”
“Msimu huu tumedhamiria kufanya usajili makini wenye tija”
Aidha Dk Msolla amesema hata hivyo jukumu la kutafuta wachezaji litabaki kwa kocha Zahera na benchi lake la ufundi, Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kumsaidia kukamilisha michakato ya usajili baada ya makubaliano kufikiwa
Dk Msolla amesema kuanzia msimu ujao watawatumia wachezaji waliocheza Yanga zamani kutafuta wachezaji
“Msimu ujao kazi kubwa itafanywa na wachezaji wetu wa zamani kwani tutawapa jukumu la kutembea mikoani kutafuta wachezaji wenye vipaji”


Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni na John Bocco waliotua Simba kutoka Azam Fc misimu miwili iliyopita, wanatajwa kuwaniwa tena na timu hiyo
Baada ya kuachana na mpango wa kubana matumizi, Azam Fc imepanga kufanya usajili mkubwa ili kuwa washindani wa kweli katika kuwania ubingwa wa ligi kuu msimu ujao
Inaelezwa uongozi wa Simba umepanga kuanza michakato ya usajili baada ya kukamilisha mpango wa kutetea ubingwa
Zaidi ya nyota 10 wa kikosi cha Simba mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu

Kiingilio cha chini cha mchezo huo utakaopigwa May 23 saa moja jioni, Mzunguuko ni Tsh 5,000/- wakati majukwaa ya VIP ni Tsh 15,000/-
Pia kutakuwa na tiketi za Platinumambazo zitapatikana kwa Tsh 100,000/-, kwa wanaohitaji tiketi hizi wawasilane na 0745346687
Mchezo huu wa Kimataifa utakuwa wa kihistoria, sio wa kukosa!

Kupitia msemaji wa TFF, Clifford Marion Ndimbo aliliweka sawa jambo hilo kwamba hakuna kanuni ya shirikisho inayoruhusu bingwa akabidhiwa kombe nje na mechi ya Ligi Kuu Bara.
“TFF ina kanuni zake hata Simba wakiandika barua kama alivyosema msemaji wao Manara kwamba endapo wangeshinda mechi zao wakabidhiwe taji la ubingwa kwenye mechi yao na Sevilla hakuna kitu kama hicho na hakitafanyika.
“Kama Zahera ana wasiwasi na hilo basi ajue kabisa kwamba TFF ina kanuni zake hata wakiandika barua hiyo, majibu yao ni rahisi kuwa kanuni haziruhusu mambo hayo”anasema.
Kuna video inayomuonyesha Zahera kwamba Simba watakabidhiwa ubingwa wakati sio mabingwa baada ya kusikia kauli ya msemaji wa Simba, Manara kuwa wataiomba TFF wawakabidhi kombe wakati wa mchezo wao na Sevilla.

Ratiba ya mechi zilizobaki za Wekundu hao wa Msimbazi inaonyesha keshokutwa May 16 watakuwa uwanja wa Uhuru kuikabli Mtibwa Sugar kisha kurejea tena uwanjani hapo May 19 kucheza na Ndanda Fc
May 21 Simba itasafiri kwenda mkoani Singida kuikabili Singida United kisha kurejea jijini Dar es salaam kucheza mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sevilla May 23
May 25 itarudi uwanja wa Uhuru kuikabili Biashara United na itamaliza msimu mkoani Morogoro kwa kuikabili Mtibwa Sugar May 28

Tuzo za mwaka huu zitahusisha wachezaji na mashabiki wa Simba ambao juhudi zao zimesaidia kupatikana kwa mafanikio makubwa msimu huu
Tuzo hizo zitakuwa na vipengele 11 ambavyo ni Mchezaji Bora, Goli Bora, Golikipa Bora, Beki Bora, Kiungo Bora na Mshambuliaji Bora
Nyingine ni Mchezaji Bora Mwanamke, Mchezaji Bora Mdogo, Shabiki Bora, Tuzo ya Heshima na Mhamasishaji Bora katika mitandao ya kijamii