Aussems apewa mbinu ya kuivusha Simba dhidi ya TP Mazembe

Droo ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika imepangwa juzi usiku, huku Simba wakirudishwa DR Congo kuvaana na TP Mazembe.

Simba wametinga hatua hiyo ya robo fainali baada ya kumaliza nafasi ya pili katika msimamo wa Kundi D, lililoongozwa na Al Ahly, wakiifunga AS Vita ya Congo katika mchezo wa mwisho.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, wataanza kibarua hicho dhidi ya wafalme hao mara tano wa Ligi ya Mabingwa Afrika, TP Mazembe kwa kucheza mchezo wa kwanza Aprili 6, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

AS Vita, iliyochapwa na Wekundu hao wa Msimbazi mabao 2-1 mwishoni mwa wiki iliyopita, kama nawaona watakavyowahadithia Mazembe kilichowakuta ndani ya uwanja huo wa Taifa.

Mara ya mwisho Wekundu wa Msimbazi kukutana na Mazembe ilikuwa mwaka 2011, baada ya hapo hawajakutana tena, kutokana na timu hiyo kukosa nafasi ya kushiriki michuano hiyo kwa kushindwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa misimu mitano.

Simba ina kila sababu ya kuutumia vyema uwanja huo wa nyumbani kama ilivyofanya kwenye hatua ya makundi ya kuhakikisha hakuna kichwa kinachotoka salama bila kunyolewa.

Basi Simba ifanye hivyo hivyo kwa Mazembe kuhakikisha haitoki na inakufa kwa kipigo cha mabao zaidi ya matatu.

Pamoja na Simba kufungwa mechi zote tatu za ugenini katika hatu ya makundi, lakini hawajafungwa nyumbani wala kutoka sare.

Walianza kuichapa JS Saoura mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kisha wakafungwa 5-0 na AS Vita nchini DR Congo na kuchapwa tena kipigo kama hicho cha 5-0 na Al Ahly ya Misri.

Katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahly, Simba walishinda 1-0 kabla ya kupoteza 2-0 dhidi ya JS Saoura nchini Algeria na kuichapa AS Vita 2-1 Uwanja wa Taifa.

Kocha Patrick Aussems anapaswa kukumbuka kile kilichomkuta DR Congo na Misri katika mechi za makundi za ugenini.

Simba ilikwenda kucheza mechi za ugenini kama ipo nyumbani, hali iliyosababisha kuruhusu idadi kubwa ya mabao, lakini sasa Aussems anapaswa kujua hatua hii ni ngumu kidogo, maana ukifungwa mabao mengi ugenini ujue umetoka, hivyo Simba inatakiwa ishinde nyumbani kisha iende kupaki basi ugenini.

Aussems asirudie makosa ya hatua ya makundi katika kipindi hiki, bali aje na mbinu nyingine za kujilinda.

Simba haitakuwa ya kwanza kupaki basi, kwani timu kubwa hata Ulaya kama Chelsea na Manchester United ambazo zilikuwa zikinolewa na kocha Jose Mourinho zilikuwa zikifanya hivyo.

Sina wasiwasi na Simba kutumia vyema uwanja wa nyumbani, zaidi iongeze mbinu na maarifa kwa ajili ya mechi za ugenini.

Katika hatua ya makundi, Aussems alinukuliwa na vyombo vya habari kuwa atashambulia mwanzo mwisho ugenini kama anavyofanya akiwa nyumbani.

Lakini lazima akumbuke kuwa nyumbani ni tofauti na ugenini na kila mtu ana mbinu za kutumia vyema uwanja wake wa nyumbani.

Aussems lazima ajue, Wanasimba sasa hivi hawahitaji mbwembwe sana, wanahitaji ushindi muhimu na kutimiza ndoto zao za kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Simba inakutana na Mazembe ya sasa ambayo si ya kutisha sana, tofauti na ile ya zamani, ingawa bado wapo wachezaji kama Reinford Kalaba, Tresor Mputu, lakini hawana makali kama yale ya miaka ya nyuma.

Lakini ni muhimu kwa benchi hilo la ufundi kujua kwamba Mazembe haijapoteza hata mechi moja ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye uwanja wao wa nyumbani kati ya michezo tisa, wakishinda saba na kutoa sare miwili.

Wakali hao wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamefunga mabao 24 na kufungwa matatu tu katika michezo hiyo waliyoshuka ndani ya Uwanja wa TP Mazembe.

Katika hatua ya makundi msimu huu, timu hiyo haijaruhusu kufungwa bao lolote kwenye uwanja wao wa nyumbani, walifanikiwa kushinda mabao 2-0 dhidi ya CS Costantine, walishusha kipigo cha 8-0 kwa Club Africain na 2-0 dhidi ya Ismaily.

Makala hii imeandikwa na MWANI NYANGASSA kwa hisani ya Bingwa

Aussems asaka dawa ya kupata matokeo ugenini

Droo ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika imefanyika jana nchini Misri Simba ikipangwa kukipiga na TP Mazembe katika hatua hiyo

Simba itaanzia nyumbani kwa kuikaribisha TP Mazembe kwenye dimba la Taifa mchezo utakaopigwa kati ya April 05/06 na mchezo wa marudiano kupigwa Lubumbashi DR Congo kati ya April 12/13 2019

Simba imejipambanua kwa kutumia vyema uwanja wa nyumbani baada ya kushinda michezo yote ya ligi ya mabingwa iliyocheza kwenye dimba la Taifa msimu huu, hivyo hakuna wasiwasi TP Mazembe hawatatoka salama uwanja wa Taifa

Hata hivyo vijana wa Patrick Aussems wamekuwa na wakati mgumu wanapokwenda ugenini. Wamefanikiwa kushinda mchezo mmoja tu dhidi ya Mbabane Swallows na kupoteza michezo mingine yote

Katika hatua ya makundi Simba iliruhusu mabao 12 ugenini huku pia ikishindwa kufunga bao lolote

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema ili waweze kutinga nusu fainali ni lazima wafanye vizuri nyumbani halafu wahakikishe hawafanyi vibaya ugenini

Amesema wamekuwa wakiyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika michezo ya ugenini na anaamini wataweza kufanya vizuri kwenye mchezo huo wa robo fainali dhidi ya TP Mazembe

Hata hivyo Aussems amesema Simba imevuka malengo iliyojiwekea kwa kutinga robo fainali ya michuano hiyo.

Amesema michuano ya msimu huu imewasaidia kubaini mapungufu yao hasa kwa michezo ya ugenini na watayafanyia kazi ili msimu ujao wawe imara zaidi

Wachezaji Simba wapewa mapumziko

Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting juzi, wachezaji wa kikosi cha Simba ambao hawakuitwa katika timu za Taifa walipewa mapumziko ya siku nne kabla ya kuendelea na maandalizi ya michezo inayofuata

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema baada ya kucheza mechi mfululizo kwa takribani mwezi mzima, wamewapa wachezaji mapumziko hayo ili waweze kuondoa uchovu

Simba inatarajiwa kuerejea mazoezini Jumatatu ijayo kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mbao Fc ambao huenda ukapigwa dimba la Jamhuri mkoani Morogoro, March 31 2019

Uwanja wa Taifa unatarajiwa kufungwa baada ya mchezo kati ya Tanzania dhidi ya Uganda utakaopigwa Jumapili, March 24 2019

FT : Simba 2-0 Ruvu Shooting

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba wameendeleza wimbi la ushindi katika ligi baada ya leo kuibamiza Ruvu Shooting mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa

Mabao ya Simba yalipatikana kwenye kipindi cha pili yakiwekwa kambani na beki Paul Bukaba (51′) huku bao la pili likifungwa na Meddie Kagere kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 55 baada ya Adam Salamba kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake leo akiwapumzisha baadhi ya nyota waliocheza mchezo wa ligi ya mabingwa mwishoni mwa wiki

Aidha bao alilofunga Kagere leo limemfanya afikishe mabao 13 sasa akishika nafasi ya pili nyuma ya Salim Aiyee wa Mwadui Fc mwenye mabao 16

Simba inaendelea kushika nafasi ya tatu ikiwa imefikisha alama 54, alama tano nyuma ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili huku Yanga ikiongoza ikiwa na alama 67

Hata hivyo Azam Fc na Yanga zimecheza michezo saba zaidi ya Simba

Kikosi cha Simba vs Ruvu Shooting Leo

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba mda mchache ujao watashuka katika dimba la Taifa kuikabili Ruvu Shooting kwenye mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amekifanyia mabadiliko kikosi kinachoshuka dimbani leo, akiwapa mapumziko baadhi ya wachezaji huku wengine wakikosekana kutokana na kukabiliwa na majukumu ya timu za Taifa

Habari njema ni kujumuishwa kwa kiungo Jonas Mkude na Meddie Kagere ambao watajiunga na majukumu ya timu za Taifa baada ya mchezo wa leo

YANGA SC: Kuna la kujifunza kutokana na mafanikio haya ya Simba

Ushindi wa mabao 2-1 walioupata Simba jana dhidi ya Vita Club umewapeleka robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Hakika wanastahili pongezi kwa mafanikio hayo

Watani zetu wametufundisha jambo kubwa sana, ili kuweza kufanikiwa tunahitaji uwekezaji wa fedha, akili, muda, hali na mali pasipo kukata tamaa

Kama Simba wangekata tamaa baada ya kupigwa zile dozi za tano tano sidhani kama wangekuwa na ubavu wa kushinda michezo yao miwili waliocheza nyumbani dhidi ya vigogo wa soka Barani Afrika

Lakini pia nyuma ya mafanikio hayo yupo mwekezaji wao Mohammed Dewji ‘Mo’ ambaye alimwaga fedha za kutosha kutengeneza kikosi ambacho leo kimewafanya waweze kutembea kifua mbele

Simba ndio klabu pekee kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ya ligi ya mabingwa

Wana Yanga yatupasa kupambana juu chini kuhakikisha nasi tunafanya mabadiliko katika timu yetu ili tuweze kuwavutia wawekezaji walete fedha

Mpango huu wa kuchangia uliopendekezwa na kocha Mwinyi Zahera sio wa kudumu, utaisaidia Yanga kusimama wakati ikijiweka sawa

Mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji ndio kila kitu, kwani mabadiliko waliyofanya Simba tumeona jinsi yalivyokuwa na faida kwao

Uwekezaji aliouweka Mo katika kipindi cha misimu miwili kwenye klabu ya Simba umekuwa na faida kubwa kwake na kwa Simba pia

Kwa kutinga hatua ya robo fainali tu Simba itavuna zaidi ya Bil 1.5 fedha ambazo ni zaidi ya fedha walizotumia kukijenga kikosi chao(bil 1.3)

Ukiongeza na fedha walizovuna kupitia mashabiki ambao waliujaza uwanja wa Taifa katika michezo yote mitatu waliocheza jijini Dar es salaam pamoja na mauzo ya jezi, timu hiyo itakuwa imetengeneza fedha nyingi sana

Simba wametuonyesha kumbe haya yote yanawezekana, ukijipanga vizuri na ukafanya uhamasishaji wa kutosha unaweza kufanya mambo makubwa kuliko wengi tulivyokariri

Nani alitegemea kama Simba itaweza kuifunga Al Ahly, mabingwa mara nane barani Afrika? Al Ahly ambayo ilicheza fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika msimu uliopita

Nani alidhani kama Simba itapata ushindi dhidi ya Vita jana? Hawa Vita walicheza fainali ya kombe la shirikisho msimu uliopita

Simba haikupewa nafasi ya kupenya katika kundi D lililozijumuisha JS Saoura, Al Ahly na Vita lakini wamepita

Hivi kuna atakayeshangaa tena kama Simba itatwaa ubingwa wa Afrika? kwani hatua waliyofikia lolote linaweza kutokea.

Jambo la muhimu kwa Wana Yanga ni kupata somo kutokana na mafanikio haya. Kama hatua hazitachukuliwa, Yanga haiwezi kushindana na Simba katika nyanja zote.

Ni wazi msimu ujao huenda ukawa mgumu zaidi kupambana na Simba kwani watakuwa bora mara dufu kuliko walivyo sasa.

Sababu mpaka hapa walipofikia wameyajua mapungufu yao na tayari wanao ushawishi wa kumsajili mchezaji yeyote wanayemtaka kutokana uwepo wa fedha na mafanikio waliyopata

Itakuwa muujiza kwa Yanga yetu hii kushindani na wenzetu ambao kimsingi mpaka sasa wameshatuacha mbali sana

ERASTO NYONI

Nyoni amepona, huyu ndio ‘Waziri wa Ulinzi’ Simba

Mashabiki wa Simba walikuwa na kila sababu ya kukosa furaha wakati kiraka Erasto Nyoni alipopata majeraha kwenye michuano ya kombe la Mapinduzi na kumfanya akose michezo mitano ya ligi ya mabingwa

Baada ya kuwa nje tangu mwezi Januari, Nyoni alirejea kikosini jana kuwakabili Vita Club na hakika alidhihirisha kwa nini mashabiki walihitaji sana urejeo wake

Licha ya kutocheza kwa muda mrefu Nyoni hakuonyesha dalili yoyote ya kutokuwa ‘fit’ akiwadhibiti ipasavyo washambuliaji wa Vita walio-ongozwa na Makusu

Nyoni alifanya kazi ya ziada kwenye safu ya ulinzi ya Simba akiwa kiongozi aliyesaidia kuwapanga wenzake katika kuhakikisha wapinzani hawalifikii lango

Juzi kocha Mkuu wa Taifa Stars Emmanuel Amunike alimrejesha katika kikosi cha timu ya Taifa kuchukua nafasi ya Andrew Vicent wa Yanga

Unapozungumzia ushindi wa mabao 2-1 iliyopata Simba dhidi ya Vita Club jana, unazungumzia juhudi na kujituma kwa wachezaji wa Simba, Nyoni akiwa mmoja wa wachezaji waliocheza vizuri sana

Baada ya Simba Kufuzu, Manara Atatimiza Ahadi ya Kutoisema Yanga Vibaya?

Simba imeweka historia nyingine kwa Tanzania baada ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika jana katika Uwanja wa Taifa.

Kwenye mchezo huo wa mwisho wa hatua ya makundi dhidi ya AS Vita, Simba ilihitaji ushindi wowote ili ifuzu hatua ya robo fainali, jambo ambalo lilifanikiwa kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, mabao yaliyofungwa na Mohamed Hussein katika dakika ya 36 na Clatous Chama katika dakika ya 90 huku bao pekee la AS Vita likifungwa na Kasendu Kazidi katika dakika ya 13.

Kabla ya mchezo huo, Afisa Habari wa Simba, Haji Manara aliahidi kupitia kipindi cha Kipenga Xtra cha East Africa Radio kuwa endapo klabu yake itaibuka na ushindi, hatowasema mahasimu wake Yanga kama alivyokuwa akifanya hapo awali, bali atakaa kimya.

“Mashabiki wa Yanga wananihofia sana mimi, wanaogopa kuisapoti Simba kisa eti mimi nitasemaje. Sasa naahidi Simba ikishinda sitowasema Yanga, nitaishia kusema tu ‘Alhamdulillah'”, alisema Manara, Ijumaa, Machi 15.

Lakini kinachoonekana hivi sasa baada ya ushindi huo ni muendelezo wa maneno yake ya utani kwa mahasimu wake ambao amesema walikuwa wakiidharau timu yake.

Ahadi nyingine ambayo aliihidi Manara ni kuwa endapo Simba itavuka hatua hii ya makundi na kwenda robo fainali, basi yatakapomalizika mashindano hayo mwezi June, yeye ataitwa Msemaji wa Mabingwa wa Afrika.

Simba imevunja rekodi yake yenyewe kuwa klabu ya kwanza Tanzania tangu mwaka 1974 kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano