SEVILA YAWASILI BONGO

Kikosi cha Sevilla kimewasili jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa Tanzania Bara Simba

Sevilla ilikaribishwa nchini kwa burudani ya Msanii maarufu Mrisho Mpoto ‘Mjomba’ aliyetumbuiza uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati timu hiyo ilipowasili

Wapinzani wao Simba wanatarajiwa kurejea leo Dar kutoka mkoani Singida ambako jana walitwaa ubingwa wa ligi kuu kwa msimu wa pili mfululizo baada ya kuifunga Singida United mabao 2-0

Baada ya mchezo jana, Simba ilielekea mkoani Dodoma ambako leo inatarajiwa kuunganisha kwa usafiri wa Ndege kurudi jijini Dar es salaam

NIYONZIMA: Azidi Kuweka REKODI

– Kiungo wa Kimataifa wa Rwanda na Klabu ya @simbasctanzania ameendelea kuweka rekodi zake ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara kuwa Mchezaji wa kigeni kutwaa Makombe mengi zaidi ya Ligi Kuu Tanzania Bara; Baada ya kunyakua Ubingwa wa msimu huu 2018/19, Niyonzima Sasa kabeba Ubingwa Mara tano mfululizo Pia kwa jumla ni Mara ya Sita anatesa Ubingwa wa Tanzania 🇹🇿 akiwa na vilabu viwili tofauti na vikongwe nchini.
🏆2012/13 (Yanga)
🏆2014/15 (Yanga)
🏆 2015/16 (Yanga).
🏆 2016/17 (Yanga).
🏆 2017/18 (Simba).
🏆 2018/19 (Simba).
.
– Licha ya Bongo tu, Niyonzima Ana medali tatu za Ubingwa wa Kwao Rwanda 🏆 2008/9, 🏆 2009/10, 🏆 2010/11… Medali tatu za Ubingwa wa Kombe La FA kwao Rwanda 🏆 2007/8, 🏆 2009/10, 🏆 2010/11 na Medali Moja ya Ubingwa wa Kombe La FA nchini 🏆 2015/16.
#LigiKuuTanzaniaBara #TPL
@Sokawaytz

MO DEWJI APONGEZA UBINGWA SIMBA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ ameipongeza timu hiyo kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara kwa msimu wa pili mfululizo

Mo amesema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na juhudi zilizofanywa na wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na wadau wote wa klabu ya Simba kila mmoja kwa nafasi yake

“Mungu mkubwa. Pongezi kwa wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, wanachama, mashabiki, na wapenzi wote wa SIMBA, tumeshinda! Najivunia mafanikio haya,” amesema Mo

Naye Msemaji wa Simba Haji Manara amewapa shukrani za kipekee wachezaji, benchi la ufundi pamoja na mashabiki wa timu hiyo kwani wamekuwa na mchango mkubwa kwa mafanikio ya Simba msimu huu

“Tumshukuru Mungu muweza aliyetaka Simba iwe Bingwa tena”

“Tuwapongeze sana Wachezaji wetu wote, Benchi la ufundi chini ya kocha Patrick Aissems, lakini kipekee tuwashukuru nyie Wanachama na Washabiki wetu ambao mimi nnaamini ndio chachu ya huu ubingwa”

“Kwangu shujaa wa kwanza Simba ni Mshabiki wetu, Tunawashukuru sana”

Simba imetwaa ubingwa leo baada ya kuifunga Singida United mabao 2-0

Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa baada ya kufikisha alama 91 kwenye msimamo wa ligi

Alama hizo haziwezi kufikiwa na timu nyingine yoyote katika michezo iliyobaki

Simba imeibuka na ubingwa huku ikiwa na michezo miwili mkononi

BREAKING NEWS: SIMBA WATWAA UBINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA 2018/2019

Simba imefanikiwa kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Singida United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Namfua
Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa wake wa 20
Simba imefikisha alama 91 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine hata kama zitashinda michezo yote iliyobaki

Wachezaji, benchi la Ufundi na viongozi wa Simba wanastahili pongezi kwa mafanikio haya ya kikosi cha Simba

Ubora wa timu, ushirikiano baina ya Wana Msimbazi ndio sababu kubwa iliyopelekea kuibuka na ubingwa wa pili mfululizo

Msimu haukuwa mwepesi kutokana na Simba kushiriki katika mashindano mengi, lakini juhudi za wachezaji zimewezesha kupatikana kwa mafanikio haya
Simba imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao, mashindano ambayo tayari imepata uzoefu mkubwa msimu baada ya kufika hatua ya robo fainali
Hongera kwa wanamsimbazi

SIMBA BINGWA LIGI KUU TANZANIA 2018/2019

Simba imefanikiwa kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Singida United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Namfua

Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa wake wa 20

Simba imefikisha alama 91 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine hata kama zitashinda michezo yote iliyobaki

Wachezaji, benchi la Ufundi na viongozi wa Simba wanastahili pongezi kwa mafanikio haya ya kikosi cha Simba

Ubora wa timu, ushirikiano baina ya Wana Msimbazi ndio sababu kubwa iliyopelekea kuibuka na ubingwa wa pili mfululizo

Msimu haukuwa mwepesi kutokana na Simba kushiriki katika mashindano mengi, lakini juhudi za wachezaji zimewezesha kupatikana kwa mafanikio haya

Simba imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao, mashindano ambayo tayari imepata uzoefu mkubwa msimu baada ya kufika hatua ya robo fainali

Hongera Wachezaji, Hongera Benchi la Ufundi, Hongera Viongozi, Hongera Mashabiki wa Simba……!

SHEREHE ZA UBINGWA SIMBA KUANZA LEO SINGIDA

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wako mkoani Singida ambapo leo watashuka katika uwanja wa Namfua kuikabili Singida United katika mchezo ambao huenda wababe hao wa soka la Tanzania watatawazwa mabingwa

Simba inayoongoza ligi ikiwa na alama 88, inahitaji alama moja tu katika mchezo huo ili iweze kurudi na kombe jijini Dar es salaam

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wataingia katika mchezo huo kusaka ushindi ingawa wanafahamu pointi moja itatosha kutimiza lengo la kutwaa ubingwa

“Tuko hapa kwa ajili ya kusaka ushindi, Nawakaribisha mashabiki wetu waje kwa wingi uwanjani kutuunga mkono ili tuweze kutimiza lengo la kutwaa ubingwa leo,” amesema Aussems