Rwandamila Amtaka Beno kakolanya zesco united

credit: @sokaonline_…

Klabu ya Zesco Utd rasmi imeanza harakati za kuinasa saini ya golikipa aliyeachana na Yanga Beno Kakolanya ikiwa ni pendekezo la kocha wa timu hiyo George Lwandamina. .

.

Lwandamina ameithibitishia @sokaonline_ kuwa ni kweli anamhitaji kwa kuwa anatambua uwezo wake tangu akiwa Yanga hivyo endapo watafikia makubaliano basi atahakikisha anatua klabuni hapo. .

.

Lakini huenda Zesco Utd wakapata wakati mgumu kumpata kutokana na Simba Sc nao kuhitaji huduma yake.

Yanga yasijili tena mrundi

credit: @sokawaytz…

✍🏻 Klabu ya Yanga SC Imeendeleza vurugu zao kwenye suala zima la usajili baada ya kushusha beki mwingine wa Kimataifa wa Burundi, Moustafa Selemani; Moustafa ametua jana akitokea kwao Burundi katika Klabu ya Aigle Noir FC Ambao pia ndio Mabingwa wa Burundi msimu huu.

:

✍🏻 Beki huyo ambaye Pia ni Nahodha wa Timu ya taifa ya Burundi U23, kabakiza mwezi tu katika Mkataba wake na Aigle Noir, na kwa mujibu wa Taarifa ni tu ni kwamba kafikia Makubaliano ya Kusaini Mkataba wa Miaka miwili na Mabingwa wa Kihistoria Tanzania Klabu ya Yanga SC.. Nyota huyo Sasa ni beki wa Pili wa Kimataifa kusinyaa Jangwani Baada ya Mghana, Lamine Moro kumwaga wino siku chache zilizopita..

#transfers #updates

@Sokawaytz

Namuonga yaanza kusajili vifaa

credit: @sokawaytz…

– Mshambuliaji wa Klabu ya Alliance FC, Bigirimana Blaise ameripotiwa kusaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia Namungo FC iliyopanda kucheza Ligi Kuu Bara msimu wa 2019/20 ikitokea FDL 2018/19.

.

– Kwa mujibu wa chanzo cha ndani kutoka katika klabu ya Namungo Ni kwamba wamefanikiwa kunasa saini ya mchezaji huyo baada ya kumalizana na timu yake ya Alliance; Blaise alijiunga na Alliance akitokea Stand United ambayo ilishindwa kumlipa maslahi yake ya mshahara sambamba na fedha yake ya usajili..

#updates #transfers

Yanga wasaini chombo kingine

credit: @sokawaytz…

– Mlinda lango wa timu ya taifa ya Tanzania, Metacha Mnata 20″ amejiunga na Klabu ya Yanga SC kwa Kusaini Mkataba wa miaka miwili, Nyada huyo kajiunga na Yanga akitokea kuitumikia Klabu ya Mbao FC kwa mkopo ambapo Sasa kamaliza Mkataba wake na Azam FC..

.

– Usajili mwingine tena Jangwani, Mshambuliaji wa Kimataifa, Maybin Kalengo 20″ nae amesinyaa rasmi Mkataba wa Miaka Miwili kuwatumikia miamba hao msimu ujao.. Kalengo katoka kuitumikia Klabu ya ZESCO United ya kwao Zambia..

#transfers

@Sokawaytz

Bakambo aondoka rasmi yanga

credit: @sokawaytz…

MAKAMBO AONDOKA RASMI YANGA

Straika Heritier Makambo ameaga na kuondoka rasmi nchini tayari kujiunga na timu yake mpya ya Horoya AC ya nchini Guinea huku uongozi wa Yanga ukimpa Baraka zake.

.

.

“Tunakutakia kila lakheri Heritier Makambo kwenye majukumu yako mapya huko uendako tunatambua na tunathamini sana mchango wako kwenye klabu yetu” – Yanga.

@heritier_ebenezer @yangasc @horoyaac