Mchezaji wa mtibwa sugar nickson kibabage amesaini mkataba wa miaka 4 kuitumikia timu Difaa El jadida ya Morocco

credit: @sokawaytz…

– Mchezaji wa Klabu ya Mtibwa Sugar, Nickson Kibabage, amesaini mkataba wa miaka minne (4) Kuitumikia klabu ya Difaa El Jadida ya Ligi Kuu Nchini Morocco… Kibabage anaungana na Mtanzania mwingine kwenye timu hiyo ambaye ni nyota wa Taifa Stars, Simon Msuva.

:

– Kibabage anaweza kucheza kama Mlinzi wa kushoto au winga wa kushoto, nafasi zote huzimudu vizuri akiwa na timu za taifa mwanzo U17 na Sasa yupo U20 na U23..

#transfers

Hazard siwez lazimisha kuvaa jezi number 10 wala kupiga penati

credit: @sokawaytz…

– Eden Hazard amesema kuwa yeye hajali juu kutovaa jezi namba 10 au kutokuwa na majukumu ya kupiga mikwaju ya penalti katika Klabu yake mpya ya Real Madrid; Mshambuliaji huyo wa Kimataifa wa Ubelgiji alijiunga na Blancos kwa €100 (£88m / $112m) kutoka Chelsea wiki iliyopita.

.

— “Nimezungumza na Modric kwa kupitia kwa Kovacic, nikamuuliza kama angeweza kuniachia Mimi jezi No.10, alisema hapana, ni lazima nitafute namba nyingine,” alisema Hazard.

.

— Nyota huyo Pia aliongeza kuwa “Kwangu mimi namba 10 ya jezi si muhimu, lakini kucheza na jezi hii, na nembo hii inatosha”.

.

– Hazard pia amesema hatolazimisha kutaka kuchukua penati ili apige yeye ndani ya Real Madrid, kwani kawakuta wapiga wengine wengi wa penati ndani ya Klabu… Sergio Ramos msimu uliopita alipiga penati Nane Kati ya 12 za Klabu hiyo, Karim Benzema akipiga penati tatu na Gareth Bale akipiga penati moja..

#Updates

@Sokawaytz

Kibabage amfuata Msuva difaa Morocco

credit: @simbamakini…

KIBABAGE AMFUATA MSUVA DIFAA

Mlinzi wa kushoto wa Mtibwa Sugar, Nickson Kibabage amesaini mkataba wa miaka minne kuitumikia klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco ambayo anachezea Mtanzania, Simon Msuva.

Kibabage aling’ara na kuonekana akiwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ kilichoshiriki michuano ya Afcon nchini Gabon mwaka 2017.

Source: Boiplus Media

De light atua Rasmi Paris sant Germany kwa mkataba wa miaka 5

credit: @sokawaytz…

– Rasmi!! Matthijs De Ligt leo amepokea ofa rasmi ya mkataba kutoka Klabu ya Paris Saint-Germain ambao ni Mabingwa wa Ufaransa; Ofa hiyo ni kwa Mkataba wa miaka mitano na Mshahara wa £350k kwa Wiki.

.

– Kwa mujibu wa @fabriziorom, Wakala Wake, Mino Raiola sasa yuko Paris, Ufaransa kuanza mazungumzo na mkurugenzi mpya wa PSG, Leonardo. Mchezaji huyo lakini bado hajaamua juu ya klabu yake ijayo wapi atatimkia, lakini PSG inatajwa kutaka kumaliza dili hilo mapemaa kabla ya Miamba wengine hawajapanda dau.. De Ligt anasubiri kama vilabu vingine (zaidi ya Barcelona, kuliko Manchester United au Liverpool ambapo hawezi kwenda) watawasilisha dau lingine Baada ya na hapo basi atatangaza uhamuzi wake.. 🇳🇱🔵

#deligt #psg #mufc #lfc #barcelona #transfers

@Sokawaytz

Pogba hauzwii !!!!⚽️

credit: @simbamakini…

Manchester United imeiambia Real Madrid kuwa kiungo wao Paul Pogba hauzwi kwa dau lolote. Madrid wamepanga kuimarisha kikosi chake ili kurejesha makali yao yaliyopteza katika misimu miwili iloyopita.

Madrid itamshawishi Pogba kuomba barua ya kuondoka (Transfer request) ili kupata nafasi ya kumsajili la sivyo haitawezeka kupata saini yake kwakua United imewakomalia.