MAKAMBO Ajaza Pesa JANGWANI

Yanga imefikia makubaliano na klabu ya Horoya Fc kumuuza mshambuliaji wake Heritier Makambo aliyesaini kunako klabu hiyo mkataba wa miaka mitatu

Habari njema ni kuwa Yanga itafanya biashara ya faida kwani itaingiza zaidi ya Mil 230, ikipata faida ya zaidi ya Mil 170

Makambo alitua Yanga akitokea klabu ya FC Lupopo ya DR Congo kwa dau la takribani Milioni 60

Yanga inaendelea na mchakato wa kukiboresha kikosi chake na bila shaka fedha hizo zitatumia katika usajili unaoendelea

Makambo tayari ametambulishwa kunako klabu ya Horoya Fc, mabingwa wa Guinea

Mkurugenzi wa Ufundi wa Horoya Jaid Martin wiki ijayo atakuwa jijini Dar es Salaam kumalizana na Yanga ili kukamilisha taratibu za mwisho za usajili wa Makambo

Uongozi wa Yanga kupitia Mwenyekiti Dk Mshindo Msolla amethibitisha kuwa na taarifa ya Makambo kwenda kufanyiwa vipimo vya afya

“Ni kweli Makambo aliondoka juzi na mwalimu Zahera kuelekea Guinea kwa ajili ya vipimo kwa klabu ya Horoya huko Guinea,” amesema Dk Msolla

“Tunasubiri warudi tuitazame ofa yao kisha tufanye biashara. Taarifa za kutambulishwa rasmi sizielewi ila mwalimu akirudi tutaitazama ofa yao kulinganisha na klabu zingine nyingi zinazomtaka kisha tutafanya maamuzi”

BREAKING NEWS: MAKAMBO ATIMKA YANGA, AJIUNGA HOROYA AC

Mshambuliaji wa Yanga Heritier Makambo ametimkia Guinea kujiunga na klabu ya Horoya Fc

Taarifa za Makambo kusajiliwa na Horoya zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii mapema leo ambapo timu hiyo imemtambulisha rasmi
Makambo ndiye kinara wa mabao katika kikosi cha Yanga msimu huu akitupia kambani mabao 16

Kulingana na mtandao wa Kalonews, Makambo amesaini mkataba wa miaka mitatu

“Horoya AC imemsajili mshambuliaji kutoka DR Congo Heritier Makambo aliyekuwa akiichezea Young Africans ya Tanzania,” imesema taarifa ya mtandao huo

“Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliyewahi kuichezea Motema Pembe, amefunga mabao 16 kwenye ligi ya Tanzania”
“Amesaini mkataba wa miaka mitatu”

Kuondoka kwa mshambuliaji huyo ni pigo kwa Yanga ambayo iko kwenye mchakato wa kukiimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao

https://play.app.goo.gl/?link=https://play.google.com/store/apps/details?id=com.chumbani.raha&ddl=1&pcampaignid=web_ddl_1

Yanga italazimika kuingia sokoni kusaka washambuliaji wengine wakali

Hata hivyo Yanga itanufaika na mauzo ya mshambuliaji huyo kwani mkataba wake na Yanga ulikuwa bado haujamalizika
Inaelezwa Makambo ameuzwa kwa dau linalokadiriwa kufikia Milioni 230 za Kitanzania




Yanga kuunda Kamati ya Usajili

Uongozi wa klabu ya Yanga uko katika mchakato wa kuunda Kamati ya usajili ambayo itashirikiana na Kocha Mwinyi Zahera kusimamia usajili wa timu hiyo

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Yanga jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa timu hiyo Dk Mshindo Msolla amesema tayari uteuzi umeshafanyika kwa sasa wanafanya majadiliano na wajumbe walioteuliwa kabla ya kuwaweka hadharani

“Wajumbe wa Kamati hiyo tumeshawateua lakini hatuwezi kuwatangaza kabla nao hawajaridhia,” amesema Dk Msolla

“Wiki ijayo tutakuwa na kikao na benchi la Ufundi, pengine katika kikao hicho tutaitangaza Kamati”

“Msimu huu tumedhamiria kufanya usajili makini wenye tija”

Aidha Dk Msolla amesema hata hivyo jukumu la kutafuta wachezaji litabaki kwa kocha Zahera na benchi lake la ufundi, Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kumsaidia kukamilisha michakato ya usajili baada ya makubaliano kufikiwa

Dk Msolla amesema kuanzia msimu ujao watawatumia wachezaji waliocheza Yanga zamani kutafuta wachezaji

“Msimu ujao kazi kubwa itafanywa na wachezaji wetu wa zamani kwani tutawapa jukumu la kutembea mikoani kutafuta wachezaji wenye vipaji”

Yanga yatenga Bilioni Mbili kwa ajili ya usajili

Uongozi wa Yanga umetenga kati ya Tsh Bilioni 1.5 hadi Bilioni mbili kwa ajili ya usajili wa msimu ujao

Katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Makao Makuu ya Yanga jijini Dar es salaam leo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa Lucas Mashauri amesema walikutana na kocha Mwinyi Zahera ambapo aliwapa mchanganuo wa mahitaji yake kwa ajili ya usajili

“Bajeti ya usajili mara nyingi inatolewa baada ya kukamisha zoezi la usajili”

“Lakini kwa sasa tunakuwa na makisio ya Bajeti tunayohitaji ambapo Kamati yetu ilipewa kazi ya kutafuta kati Bilioni 1.5 na Bilioni mbili,” amesema

“lengo letu kubwa ni kuwa na Yanga imara msimu ujao. Kazi tumemuachia kocha Mwinyi Zahera ili atuambie wachezaji anaowahitaji”

“Bajeti halisi itafahamika baada ya kocha kujadiliana na wachezaji anaotaka waje”

“Lakini tumemuhakikishia, hakuna mchezaji ambaye atamuhitaji tutashindwa kumsajili. Awe Tanzania, nje ya Tanzania hata Ulaya akipatikana mchezaji tutamsajili. Yanga imeshawahi kusajili wachezaji kutoka Ulaya”

“Kamati yetu inaendelea na zoezi la kutafuta fedha ili tuweze kutimiza lengo la kusajili timu bora kadiri kocha atavyopendekeza”

Katika hatua nyingine, Mashauri amewataka Wanayanga waendelee kuichangia timu yao waepuke upotoshaji unaosambazwa kwenye mitandao ya kijamii

“Tunawataka wapenzi, wanachama na mashabiki wetu waendelee kuichangia timu wasipotoshwe na taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao”

“Taarifa nyingi zinazosambazwa kuwa tumepokea Bilioni mbili hazina ukweli wowote. Wanaoanzisha taarifa hizo wana lengo la kupunguza kasi ya kuichangia timu yetu”

“Yanga ni timu ya Wananchi na safari hii tumeamua kuisimamia sisi wenyewe. Na kama alivyosema Mwenyekiti, zoezi hili la uchangiaji litandelea kwa kuwa ni wajibu kwa kila Mwanchama wa Yanga kuichangia timu kila mwezi Tsh 1000/- ambayo ni ada ya uanachama”

Azam yanyemelea nyota Simba

Wakati klabu ya Simba ikiwa ‘busy’ kuhakikisha inatetea ubingwa wake, baadhi ya nyota wake ambao mikataba yao imemalizika, wameingia kwenye rada za Azam Fc

Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni na John Bocco waliotua Simba kutoka Azam Fc misimu miwili iliyopita, wanatajwa kuwaniwa tena na timu hiyo

Baada ya kuachana na mpango wa kubana matumizi, Azam Fc imepanga kufanya usajili mkubwa ili kuwa washindani wa kweli katika kuwania ubingwa wa ligi kuu msimu ujao

Inaelezwa uongozi wa Simba umepanga kuanza michakato ya usajili baada ya kukamilisha mpango wa kutetea ubingwa

Zaidi ya nyota 10 wa kikosi cha Simba mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu

SIMBA WASHUSHA MAJEMBE MAPYA

MABOSI wa Simba kwa msimu ujao hawataki mchezo kwani wamedhamiria kukisuka hasa kikosi chao kiwe cha ushindani na kwa kuanza hivi karibuni watazishusha sura mpya nne za kigeni, akiwemo mshambuliaji Mzambia, Lazarus Kambole.
Mabosi wa Simba wanataka kukiboresha kikosi chao kwa kuleta wachezaji wenye viwango vikubwa kutokana na aina ya matokeo ambayo walikuwa wanayapata kwenye michezo ya Ligi ya Mabingwa Afrika ya ugenini kwa msimu huu.
Chanzo kutoka Simba kimeliambia Championi Jumatatu, kuwa wachezaji hao wane wanatarajiwa kuingia nchini hivi karibuni ambapo wanaweza kuwemo kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Simba na Sevilla ya Hispania.

“Viongozi wanataka kuboresha kikosi kiwe na uwezo wa hali ya juu kwenye michezo ya kimataifa kuliko msimu huu, ndiyo maana viongozi wanaleta wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu kuliko ambao wapo kwa sasa.

“Wachezaji hao wanaweza kuwepo hapa nchini kwenye mechi na Sevilla kwa ajili ya kuangaliwa na kuongea na viongozi kabla ya kusaini mikataba kwa msimu ujao.
“Huyo Kambole unayesema anaweza kuwemo katika orodha hiyo, lakini ni suala la kusubiri kuona kama ni yeye ambaye atakuja hapa ama la,” kilisema chanzo hicho.

Katibu wa Simba, Anord Kashembe amesema: “Huu siyo wakati wa kufanya usajili, hatuwezi kulizungumzia hilo, ukifika muda wake kila kitu kitakuwa sawa.”

Chanzo: championi & gpl

TETESI ZA USAJILI YANGA: Kifaa kipya Yanga hiki hapa, ni hatari tupu, kutua nchini mwezi ujao

Kwa mujibu wa mtandao wa michezo wa ‘Kawowo Sports’ kutoka nchini Uganda umeripoti kuwa mshambauliaji wa zamani wa klabu ya Onduparaka FC, Agau Rashid ambaye kwa sasa anaichezea timu ya Maroons FC anatarajiwa kuwasili Tanzania mwezi Juni kwa ajili ya majaribio katika miamba ya soka ya ligi kuu Young Africans SC.
Rashid ni mzuri wa kumiliki mipira na mfumaniaji mzuri wa mabao

Kwa mujibu wa wakala wa mchezaji huyo, amesema kuwa Agau amepata mualiko kwaajili ya kwenda kufanya majaribio kufuatia kufanya vizuri zaidi msimu huu.
Nyota huyo wazamani wa Onduparaka, amejiunga na Maroons msimu wa mwaka 2018/19 akiwa kama mchezaji huru kwa mkataba wa miaka mitatu hata hivyo kama atajiunga na Yanga atakuwa amewatumikia waajiri wake hao mwaka mmoja pekee.

Ndani ya msimu huu mmoja, Agau Rashid amefanikiwa kufunga jumla ya mabao saba na kuwaacha mbali baadhi ya wachezaji wenzake kama Pius Obuya na Seif Batte wenye mabao manne kila mmoja ikiwa pamoja na Isaac Otto, Bronson Nsubuga waliyosajiliwa msimu huu mwezi Januari wakiwa na mabao matatu.

Klabu ya Maroons imetoa baraka zote kwa, Agau endapo atafanikiwa kufuzu majaribio yake ndani ya Yanga, hata hivyo kama atafanikuwa atajiunga na baadhi ya Waganda wenzake kama Emmanuel Arnold Okwi na Murushid Jjuuko wanaotumikia klabu ya Simba.

TETESI ZA USAJILI YANGA: Makambo atengewa Sh228 million

SAWA msimu ujao wa kimataifa, Yanga ni kama haina chake vile kwani tayari tiketi ya Kombe la Shirikisho Afrika ilishaipoteza mbele ya Lipuli Iringa, ila hilo halijaufanya uongozi wa klabu hiyo kuacha kujipanga kukisuka upya kikosi chake kwa msimu ujao wa michuano ya ndani.
Lakini katika ya mipango yake hiyo ya kufanya usajili mzito habari mbaya ni kwamba moja kati ya klabu za Afrika kuhitaji saini ya straika wake matata, Heritier Makambo na kama kocha wake, Mwinyi Zahera atakubali, basi jamaa hatabaki Jangwani.
Taarifa ambazo uongozi wa Yanga unazifanya kuwa siri kubwa ni juu ya ofa hiyo ambayo imetua klabuni hapo hivi karibuni ikimtaka mshambuliaji huyo raia wa DR Congo, lakini Mwanaspoti limefanikiwa kupenyezewa bila chenga juu ya mchongo huo.
Bosi mmoja wa Yanga ameliambia Mwanaspoti, Makambo ana ofa ya sio kwenda kujaribiwa, bali ni kuuzwa, huku klabu hiyo (ikifichwa jina lake) ikitaka kutoa kiasi kisichopungua Dola 100,000 (zaidi ya Sh.228 milioni).

Dau hilo sasa lipo mezani kwa Yanga likisubiri kujua kipi kitaamuliwa na Kocha Zahera ambaye ndiye aliyemshusha nchini mwishoni mwa msimu uliopita akitokea kwao, DR Congo.

Hata hivyo, kitu pekee ambacho Zahera na mabosi wa klabu hiyo wanaweza kukitumia ni kusalia kwa mkataba wa mwaka mmoja ambapo kama wataendelea kuitingisha klabu hiyo inaweza kuongeza mzigo zaidi.
Bosi huyo (jina tunalo) alisema haoni kama Yanga itapata hasara kwa kuchukua kiasi hicho kutokana na klabu hiyo kutumia kiasi kidogo kumpata mshambuliaji huyo aliyetokea DC Motema Pembe baada ya kuvunja mkataba.

“Makambo anatakiwa na klabu moja sitaki kukutajia kwa sasa kwa vile mambo hayajakamilika na iko tayari kutoa kiasi cha Dola 100,000” alisema bosi huyo ambaye alihusika kwa kiasi kikubwa katika usajili wake.

“Tunachosubiri ni jibu na uamuzi wa Kocha Zahera ambaye kimsingi ndiye mwamuzi kiufundi, lakini kwa kiasi hicho au hata zaidi sioni kama ni shida kwa Yanga naona ni faida kwa kuwa tulimpata kwa bei rahisi kupitia mpango wetu wa kuepuka usajili wa gharama kubwa.
“Kwa sasa uamuzi upo kwa Zahera na hata uongozi mpya chini ya Mwenyekiti Dk. Mshindo Msolla kama watakubaliana sawa.”
Hata hivyo, aliongeza, licha ya ofa hiyo ambayo ipo wazi zaidi lakini wakala wa mchezaji huyo ambaye anaishi Afrika Kusini ana ofa tatu za majaribio za mshambuliaji huyo.
“Hiyo ni ofa ambayo imejitosheleza na tuliwaambia wasubiri kwanza amalize ligi kwa kuwa hatukutaka achanganyikiwe wakati ule tulipokuwa tunacheza mechi muhimu za Kombe la FA.
“Unajua wachezaji wa Kikongomani wanaposikia wanahitajika sehemu ni habari kubwa kwao, unaweza kuona hata uwezo wake uwanjani unapungua sasa tusubiri kuona kipi kitaamuliwa na uongozi.”

Makambo tangu atue Yanga msimu huu amefanikiwa kuifungia timu yake mabao 16 katika Ligi Kuu, huku akifunga mengine manne katika michuano ya Kombe la FA ambapo Vijana wa Jangwani waling’olewa hatua ya nusu fainali za Lipuli FC katika Uwanja wa Samora, Iringa.

Straika huyo pia ameweza kunyakua tuzo mbili mfululizo za Mchezaji Bora wa Miezi ya Novemba na Desemba na kuisaidia Yanga kukaa kileleni kwa muda mrefu kabla ya juzi Jumatano kushushwa na Simba.

Mwinyi Zahera ameanza mchakato wa kumsajili mshambuliaji hatari Roderick Mutuma (31)

Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Sc Mwinyi Zahera ameanza mchakato wa kumsajili mshambuliaji hatari Roderick Mutuma (31) raia wa Zimbabwe ambaye kwasasa anakipiga kunako klabu ya Fc Lupopo ya Congo.
.
.
Hata hivyo huenda dili hilo likaota mbawa kutokana na nyota huyo kuwa na mkataba na klabu yake mpaka Disemba 2020 huku thamani yake ikikadiliwa kuwa ni zaidi ya milioni 200.
.
.
Mutuma alijiunga na Fc Lopopo mwishoni mwa mwezi Disemba 2018 kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Nichrut ya kwao Zimbabwe.

Simba yajipanga kuhuisha mikataba nyota nane

Ligi Kuu ya Tanzania Bara inamalizika mwezi ujao na tayari michakato ya usajili wa wachezaji imeanza kushika kasi

Nyota nane wa kikosi cha Simba mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu ambapo Mwenyekiti wa Simba Swedy Mkwabi amesema wako mbioni kuanza mazungumzo ya kuhuisha mikataba ya wachezaji hao

Miongoni mwa nyota ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu ni pamoja na Emmanuel Okwi, John Bocco, Jonas Mkude, Aishi Manula, Erasto Nyoni, James Kotei, Asante Kwasi na Shomari Kapombe

“Tunasubiri ripoti ya Mwalimu Aussems ili tuanze michakato ya usajili. Lakini bila shaka, wachezaji wengi tutaendelea nao” amesema

“Hakuna mchezaji yeyote ambaye mkataba wake wa kuitumikia Simba utakuwa umemalizika na tumempa ruhusa ya kuondoka kwa maana ya kwenda kujiunga na timu nyingine wote tuna mipango nao na tunaimani watasaini mikata mipya ya kubaki hapa.

“Bodi bado haijazungumza na mchezaji yeyote, ambaye mkataba wake unamalizika kutokana na majukumu ya mechi za kimataifa ambazo tunacheza mfululizo, lakini nadhani tutakaa nao na mambo yatakwenda sawa kwa pande zote mbili tutakubaliana”