Simba vs Azam Fc hapatoshi uwanja wa Uhuru leo

Ligi Kuu ya Tanzania Bara inaendelea leo ambapo mabingwa watetezi Simba watashuka katika uwanja wa Uhuru kuikabili Azam Fc katika mchezo usiotabirika
Huo ni mchezo wa duru ya pili msimu huu Simba ikishinda mchezo wa kwanza kwa mabao 3-1

Simba inayowania ubingwa wa pili mfululizo, kama itaibuka na ushindi leo basi itabakisha alama sita tu ili iweze kutetea ubingwa wake
Azam Fc inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi, haina matumaini ya kutwaa ubingwa wala kumaliza kwenye nafasi ya pili

Hata hivyo kocha Msaidizi wa timu hiyo Iddi Cheche amesema baada ya kufungwa katika mchezo wa kwanza, hawatakubali kupoteza mchezo dhidi ya Simba kwa mara ya pili

Mkufunzi wa Simba Patrick Aussems amesema Azam Fc ni timu nzuri lakini hawaihofii na baada ya kupoteza mchezo uliopita, wanahitaji kushinda leo
Mchezo huo unatarajiwa kuanza saa kumi jioni

Yanga kuivaa Ruvu Shooting kesho, Chikupe kukosa

Mabingwa wa kihistoria Yanga kesho Jumanne watashuka kwenye uwanja wa Uhuru kuikabili Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara hatua za lala salama


Baada ya kupoteza michezo miwili iliyopita dhidi ya Lipuli Fc (FA) na Biashara United, vijana wa Mwinyi Zahera wamepania kuondoka na alama zote tatu dhidi ya Ruvu Shooting

Kwenye mchezo wa kesho Yanga itamkosa beki wake Andrew Vicent mwenye kadi tatu za njano
Hata hivyo Yanga haina hofu ya kukosekana kwake kwani beki Abdallah Shaibu ‘Ninja’ yupo

Yanga imebakisha michezo mitatu ya kumaliza msimu na yote itapigwa kwenye uwanja wa Uhuru

Aussems auhofia mchezo dhidi ya Azam Fc

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema mchezo wa kesho dhidi ya Azam Fc hautakuwa mwepesi na anaamini kama timu yake itaibuka na ushindi, basi wanaweza kutwaa ubingwa wa ligi kuu mapema

Simba ina michezo mitatu mfululizo itakayopigwa uwanja wa Uhuru na kama watashinda yote, basi watatetea ubingwa kabla ya kuivaa Sevilla May 23 mchezo ambao unaweza kutumika kuwakabidhi taji

Baada ya mchezo dhidi ya Azam, mchezo unaofuata ni dhidi ya Mtibwa Sugar kisha kumaliza na Ndanda Fc May 19

“Ushindi mchezo dhidi ya Azam ni muhimu. Matokeo hayo yatatuweka katika nafasi nzuri zaidi ya kutwaa ubingwa,” amesema

“Azam ni timu nzuri, tuliwafunga kwenye mchezo wa kwanza. Tunahitaji kuwa katika kiwango bora ili tuwafunge tena”

Hata hivyo Aussems amesema Simba bado ina michezo mingi (sita) na lengo lao ni kushinda yote

“Mechi zote zilizobaki tunazichukulia kwa umuhimu uliosawa. Tunafahamu hazitakuwa nyepesi lakini tumedhamiria kutetea ubingwa hivyo tunahitaji matokeo a ushindi. Tutapambana kadiri ya uwezo wetu ili kufikia malengo”

Aussems auhofia mchezo dhidi ya Azam Fc

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema mchezo wa kesho dhidi ya Azam Fc hautakuwa mwepesi na anaamini kama timu yake itaibuka na ushindi, basi wanaweza kutwaa ubingwa wa ligi kuu mapema

Simba ina michezo mitatu mfululizo itakayopigwa uwanja wa Uhuru na kama watashinda yote, basi watatetea ubingwa kabla ya kuivaa Sevilla May 23 mchezo ambao unaweza kutumika kuwakabidhi taji

Baada ya mchezo dhidi ya Azam, mchezo unaofuata ni dhidi ya Mtibwa Sugar kisha kumaliza na Ndanda Fc May 19

“Ushindi mchezo dhidi ya Azam ni muhimu. Matokeo hayo yatatuweka katika nafasi nzuri zaidi ya kutwaa ubingwa,” amesema

“Azam ni timu nzuri, tuliwafunga kwenye mchezo wa kwanza. Tunahitaji kuwa katika kiwango bora ili tuwafunge tena”

Hata hivyo Aussems amesema Simba bado ina michezo mingi (sita) na lengo lao ni kushinda yote

“Mechi zote zilizobaki tunazichukulia kwa umuhimu uliosawa. Tunafahamu hazitakuwa nyepesi lakini tumedhamiria kutetea ubingwa hivyo tunahitaji matokeo a ushindi. Tutapambana kadiri ya uwezo wetu ili kufikia malengo”

Sina tatizo na Tshabalala – Manula

Nahodha Msaidizi wa Simba Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ juzi alisababisha ‘majanga’ baada ya kujifunga bao pekee lililoihakishia Kagera Sugar ushindi wa tatu mfululizo dhidi ya Simba

Tshabalala alichanganyana na mlinda lango Aishi Manula hali iliyopelekea wote watokee majaro iliyokuwa imechongwa kutoka wingi ya kushoto tukio lilisababisha Tshabalala aujaze mpira kimiani

Baada ya tukio hilo, Manula alimvaa Tshabalala na wawili hao ‘kushikana mashati’ kabla Mlipili hajaingilia kati kumuondoa Tshabalala eneo la tukio

Manula amesema tukio lililotokea uwanjani kati yao lilisababishwa na presha ya mchezo lakini liliishia palepale uwanjani, hawana tatizo nje ya uwanja

“Hatukuwa na mawasiliano mazuri,” amesema Manula ambaye pia ni mlinda lango namba moja wa timu ya Taifa ya Tanzania

“Kilichotokea pale kilisababishwa na presha ya mchezo tu, Tshabalala ni rafiki yangu na tumekuwa tukishirikiana katika masuala mbalimbali”

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alilizungumzia tukio hilo ambapo alisema limechangiwa kwa kiasi kikubwa na uchovu wa wachezaji wake ambao wamekuwa wakicheza mfululizo

“Tumecheza michezo saba ndani ya siku 16, wachezaji wangu ni binadamu, wanachoka. Ndio maana baadhi ya matukio wanayofanya yanasameheka kwa kuwa najua yanasababishwa na mazingira yanayotukabili”

Wawa arejea kikosini Simba

Beki kisiki wa Simba Paschal Serge Wawa amerejea kikosini baada ya kuwa nje kwa mwezi mmoja akiuguza majeraha ya nyama za paja

Wawa tayari ameanza kujifua na kikosi cha Simba kinachojiandaa na mchezo dhidi ya Azam Fc utakaopigwa kesho

Hata hivyo Wawa hatarajiwi kushuka dimbani kesho kwa kuwa amepewa program maalum ya mazoezi ya pekee yake ambao ametakiwa kuyafanya kwa siku nne

“Nimeanza mazoezi. Kwa sasa nafanya mazoezi ya peke yangu kwa siku nne kabla ya kujiunga na wenzangu,” amesema

Wawa aliumia kwenye mchezo wa kwanza wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe uliopigwa April 06 katika uwanja wa Taifa

Beki huyo mkongwe huenda akarejea kikosini kwenye mchezo dhidi ya Ndanda Fc na bila shaka atakuwepo Simba itakapochuana na Sevilla kwenye mchezo wa kirafiki, May 23

Mzee Muchacho na Fahad wambananisha Haji Manara avae jezi ya Yanga SC

Afisa Habari wa Simba SC Haji Manara kuelekea mchezo wa nusu fainali ya UEFA Champions League aliahidi kuwa endapo Liverpool itaitoa FC Barcelona katika hatua hiyo basi atahama timu kutoka Simba SC na kwenda Yanga, sasa leo akakutana na mashabiki wa Liverpool Mzee Muchacho na Fahad wanamtaka atimize ahadi yake.
Ndio wanabishana na kusema kuwa Fahad atimize kwana ahadi yake ya kutobolewa macho aliyowahi kuitoa ndio Haji Manara nae atavaa jezi ya Yanga, Fahad na Mzee Muchacho wakawa wanamlazimisha Haji Manara aombe radhi kwa kushindwa kutimiza ahadi hiyo.

Aiyee awanyooshea mikono Kagere, Okwi na Bocco

Straika wa Mwadui FC,Salim Aiyee amewataja nyota wa Simba, Meddie Kagere, Emanuel Okwi na John Bocco mmoja wapo kubeba tuzo ya mfungaji bora, huku akimchomoa Heritier Makambo wa Yanga kwenye vita hiyo msimu huu.

Aiyee ambaye alianza kwa kasi msimu huu na kuongoza kwa muda mrefu kwenye orodha ya ufungaji mabao kwa kupachika 16, kwa sasa ameshaachwa nyuma mabao manne na Straika wa Simba Meddie Kagere.

Kagere amefunga mabao 20, Makambo ana mabao 16 sawa na Aiyee (Mwadui) na Bocco akiwa na 14 sawa na Okwi wote wa Simba.

Akizungumza na Mwanaspoti, Straika huyo alisema kwa hali ilivyo ni wazi nyota wa Simba, Kagere, Okwi na Bocco mmojawapo anaweza kubeba tuzo hiyo lakini kwa Makambo wa Yanga hawezi kufurukuta.

Alisema sababu ya kuwapa nafasi wachezaji wa Simba ni kutokana na kuwa na mechi nyingi lakini hata kombinesheni yao inatisha sana lakini pia wana uwezo hata kiuchumi.

“Sijakata tamaa, lakini kiukweli Kagere, Okwi na Bocco mmoja wapo anaweza kubeba tuzo ya mfungaji bora, Makambo hapana hayumo kabisa, wale Simba kombinesheni yao ni nzuriîalisema Aiyee.

Pia mshambuliaji huyo alieleza kuwa kupungua kwa kasi yake kwenye ufungaji mabao ni kutokana na mechi nyingi za ugenini kuwa na changamoto nyingi ikiwamo kukamiwa, alikiri ushindani msimu huu umekuwa mkali kutokana na ongezeko la timu.