
YANGA YAUTUMIA UWANJA WA UHURU VIZURI, YAICHAPA RUVU SHOOTING BAO 1-0
Mo Simba awards kutolewa May 30 2019

Tuzo za mwaka huu zitahusisha wachezaji na mashabiki wa Simba ambao juhudi zao zimesaidia kupatikana kwa mafanikio makubwa msimu huu
Tuzo hizo zitakuwa na vipengele 11 ambavyo ni Mchezaji Bora, Goli Bora, Golikipa Bora, Beki Bora, Kiungo Bora na Mshambuliaji Bora
Nyingine ni Mchezaji Bora Mwanamke, Mchezaji Bora Mdogo, Shabiki Bora, Tuzo ya Heshima na Mhamasishaji Bora katika mitandao ya kijamii
Simba kurejea dimba la Uhuru Alhamisi, kuikabili Mtibwa Sugar

Katika michezo miwili iliyopita Simba imepoteza alama tano, mabingwa hao watetezi wanahitaji kushinda mchezo huo
Simba haikuwa imecheza na Mtibwa Sugar msimu huu, huo utakuwa mchezo wa duru ya kwanza na timu hizo zitarudiana May 28 siku ya kuhitimisha ligi kuu msimu huu
Katika michezo mitano iliyobaki, miwili ni dhidi ya Mtibwa na mingine mitatu ni dhidi ya Biashara United (nyumbani), Ndanda Fc (nyumbani) na Singida United (ugenini)
Simba inahitaji kukusanya angalau alama nane kuweza kutetea ubingwa wake
Sare dhidi ya Azam Fc haikubadili mipango yetu – Aussems

Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya mchezo, Aussems alisema timu yake ilifanya jitihada zote za kusaka ushindi kwenye mchezo huo lakini walikosa bahati
Aidha amekosoa mbinu waliyotumia Azam FC kuwa hawakuwa na lengo la kushinda
“Tumejaribu kila mbinu kuweza kupata ushindi lakini imeshindikana. Sisi tulihitaji kushinda mchezo huu lakini mwenzetu walikuja kusaka alama moja na wameipata,” amesema
“Hata hivyo matokeo haya hayabadili chochote katika mipango yetu ya kutetea ubingwa”
Simba imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imefikisha alama 82
Bado hesabu za ubingwa ziko upande wao kwani wanahitaji alama nane tu ili kutawazwa mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo
Simba imebakisha michezo mitano
SIKU CHACHE BAADA YA UCHAGUZI…BILIONEA MPYA AIBUKA YANGA
HIKI HAPA KIKOSI CHA YANGA KITAKACHO CHEZA LEO DHIDI YA RUVUSHOOTING
Magazeti ya leo, Jumanne, May 14 2019
SIMBA YASHINDWA KUFURUKUTA MBELE YA AZAM FC WATOKA SARE TASA
Kikosi ch Simba vs Azam fc Leo

































