Aussems ataka Niyonzima aongezewe mkataba

Kocha mkuu wa Simba Patrick Aussems amependekeza klabu hiyo kumuongezea mkataba wa miaka miwili kiungo wake fundi Haruna Niyonzima ambaye anatarajia kumaliza mkataba wake mwezi ujao

Aussems amesema anamuhitaji Niyonzima kwa ajili ya msimu ujao

Amesema Niyonzima ameimarisha kiwango chake na angependa kuendelea kuwa nae kwenye kikosi chake kwa muda mrefu

Niyonzima ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa na mchango mkubwa kwenye mafanikio ya kikosi cha Simba katika michuano ya ligi ya mabingwa ambayo Simba ilitolewa hatua ya robo fainali

Aussems ahakikishiwa mkataba mpya Simba

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems atasaini mkataba mwingine wa kuendelea kuifundisha timu hiyo baada ya mkataba wake wa awali kumalizika imefahamika

Aussems aliyetua Simba mwezi Julai mwaka jana, ametimiza masharti aliyopangiwa msimu uliopita ambapo alitakiwa kuifikisha timu hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa pamoja na kutwaa taji la ligi kuu

Chini yake Simba imefanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa na iko mbioni kukamilisha sharti la pili la kutwaa ubingwa wa ligi kuu

Inaelezwa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba chini ya Mwenyekiti wake Mohammed Dewji ‘Mo’ itampa Aussems mkataba wa mwaka mmoja na atasaini mkataba huo kabla ya kurejea kwao kwa ajili ya mapumziko baada ya ligi kumalizika

Ubingwa bado unaenda Simba, mechi tatu kuamua

Licha ya kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar jana, hesabu za kutwaa ubingwa kabla ya kucheza na Sevilla ziko palepale

Keshokutwa Jumatatu May 13 Simba itashuka uwanja wa Uhuru kucheza na Azam Fc katika mchezo ambao mabingwa hao watetezi wanahitaji ushindi

Katika mchezo wa duru ya kwanza Azam Fc ilipokea kichapo cha mabao 3-1

Baada ya mchezo huo Simba itacheza na Mtibwa Sugar May 16 kisha kucheza na Ndanda Fc May 19 michezo yote ikitarajiwa kupigwa uwanja wa Uhuru

Ushindi katika michezo hiyo mitatu utaifanya Simba ifikishe alama 90 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine

Aidha lengo la kukabidhiwa kombe kwenye mchezo dhidi ya Sevilla litafanikiwa kama Simba itashinda michezo hiyo iliyobaki

Simba imeshuka dimbani mara 32, inaongoza ligi ikiwa imejikusanyia alama 81 ikifuatiwa na Yanga yenye alama 80

Uchovu umechangia kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar – Aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wemepoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar leo kutokana na changamoto mbalimbli likiwemo suala la uchovu kwa wachezaji wake

Aussems amesema wamecheza mechi nyingi ndani ya muda mfupi hivyo baadhi ya makosa yaliyofanywa na wachezaji wake yanasameheka

Nahodha Msaidizi Mohammed Hussein alijifunga bao pekee lililoipa Kagera Sugar ushindi wa bao 1-0

“Nawapongeza Kagera Sugar kwa kupata ushindi leo. Tulifanya makosa tukajifunga, tumepata nafasi kadhaa za kufunga tukashindwa kuzitumia, tumekubali matokeo ndio mpira,” amesema

“Kikosi changu kinakabiliwa na uchovu pamoja na majeruhi ya baadhi ya wachezaji. Tunajitahidi kuwapa mapumziko wachezaji lakini sasa tunakabiliwa na changamoto nyingine ya mfungo wa Ramadhani, wachezaji wengine wamefunga”

“Kabla ya mchezo wa leo tumeshinda michezo 18 kati ya 19 tuliyocheza, kufungwa ni jambo la kawaida, nampongeza kocha wa Kagera Sugar kwa kushinda leo”

Licha ya kupoteza mchezo wa leo, Simba inahitaji kushinda michezo mitatu kati ya sita iliyobaki ili kutetea ubingwa

Uchovu umechangia kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar – Aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wemepoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar leo kutokana na changamoto mbalimbli likiwemo suala la uchovu kwa wachezaji wake

Aussems amesema wamecheza mechi nyingi ndani ya muda mfupi hivyo baadhi ya makosa yaliyofanywa na wachezaji wake yanasameheka

Nahodha Msaidizi Mohammed Hussein alijifunga bao pekee lililoipa Kagera Sugar ushindi wa bao 1-0

“Nawapongeza Kagera Sugar kwa kupata ushindi leo. Tulifanya makosa tukajifunga, tumepata nafasi kadhaa za kufunga tukashindwa kuzitumia, tumekubali matokeo ndio mpira,” amesema

“Kikosi changu kinakabiliwa na uchovu pamoja na majeruhi ya baadhi ya wachezaji. Tunajitahidi kuwapa mapumziko wachezaji lakini sasa tunakabiliwa na changamoto nyingine ya mfungo wa Ramadhani, wachezaji wengine wamefunga”

“Kabla ya mchezo wa leo tumeshinda michezo 18 kati ya 19 tuliyocheza, kufungwa ni jambo la kawaida, nampongeza kocha wa Kagera Sugar kwa kushinda leo”

Licha ya kupoteza mchezo wa leo, Simba inahitaji kushinda michezo mitatu kati ya sita iliyobaki ili kutetea ubingwa

TETESI ZA USAJILI YANGA: Makambo atengewa Sh228 million

SAWA msimu ujao wa kimataifa, Yanga ni kama haina chake vile kwani tayari tiketi ya Kombe la Shirikisho Afrika ilishaipoteza mbele ya Lipuli Iringa, ila hilo halijaufanya uongozi wa klabu hiyo kuacha kujipanga kukisuka upya kikosi chake kwa msimu ujao wa michuano ya ndani.
Lakini katika ya mipango yake hiyo ya kufanya usajili mzito habari mbaya ni kwamba moja kati ya klabu za Afrika kuhitaji saini ya straika wake matata, Heritier Makambo na kama kocha wake, Mwinyi Zahera atakubali, basi jamaa hatabaki Jangwani.
Taarifa ambazo uongozi wa Yanga unazifanya kuwa siri kubwa ni juu ya ofa hiyo ambayo imetua klabuni hapo hivi karibuni ikimtaka mshambuliaji huyo raia wa DR Congo, lakini Mwanaspoti limefanikiwa kupenyezewa bila chenga juu ya mchongo huo.
Bosi mmoja wa Yanga ameliambia Mwanaspoti, Makambo ana ofa ya sio kwenda kujaribiwa, bali ni kuuzwa, huku klabu hiyo (ikifichwa jina lake) ikitaka kutoa kiasi kisichopungua Dola 100,000 (zaidi ya Sh.228 milioni).

Dau hilo sasa lipo mezani kwa Yanga likisubiri kujua kipi kitaamuliwa na Kocha Zahera ambaye ndiye aliyemshusha nchini mwishoni mwa msimu uliopita akitokea kwao, DR Congo.

Hata hivyo, kitu pekee ambacho Zahera na mabosi wa klabu hiyo wanaweza kukitumia ni kusalia kwa mkataba wa mwaka mmoja ambapo kama wataendelea kuitingisha klabu hiyo inaweza kuongeza mzigo zaidi.
Bosi huyo (jina tunalo) alisema haoni kama Yanga itapata hasara kwa kuchukua kiasi hicho kutokana na klabu hiyo kutumia kiasi kidogo kumpata mshambuliaji huyo aliyetokea DC Motema Pembe baada ya kuvunja mkataba.

“Makambo anatakiwa na klabu moja sitaki kukutajia kwa sasa kwa vile mambo hayajakamilika na iko tayari kutoa kiasi cha Dola 100,000” alisema bosi huyo ambaye alihusika kwa kiasi kikubwa katika usajili wake.

“Tunachosubiri ni jibu na uamuzi wa Kocha Zahera ambaye kimsingi ndiye mwamuzi kiufundi, lakini kwa kiasi hicho au hata zaidi sioni kama ni shida kwa Yanga naona ni faida kwa kuwa tulimpata kwa bei rahisi kupitia mpango wetu wa kuepuka usajili wa gharama kubwa.
“Kwa sasa uamuzi upo kwa Zahera na hata uongozi mpya chini ya Mwenyekiti Dk. Mshindo Msolla kama watakubaliana sawa.”
Hata hivyo, aliongeza, licha ya ofa hiyo ambayo ipo wazi zaidi lakini wakala wa mchezaji huyo ambaye anaishi Afrika Kusini ana ofa tatu za majaribio za mshambuliaji huyo.
“Hiyo ni ofa ambayo imejitosheleza na tuliwaambia wasubiri kwanza amalize ligi kwa kuwa hatukutaka achanganyikiwe wakati ule tulipokuwa tunacheza mechi muhimu za Kombe la FA.
“Unajua wachezaji wa Kikongomani wanaposikia wanahitajika sehemu ni habari kubwa kwao, unaweza kuona hata uwezo wake uwanjani unapungua sasa tusubiri kuona kipi kitaamuliwa na uongozi.”

Makambo tangu atue Yanga msimu huu amefanikiwa kuifungia timu yake mabao 16 katika Ligi Kuu, huku akifunga mengine manne katika michuano ya Kombe la FA ambapo Vijana wa Jangwani waling’olewa hatua ya nusu fainali za Lipuli FC katika Uwanja wa Samora, Iringa.

Straika huyo pia ameweza kunyakua tuzo mbili mfululizo za Mchezaji Bora wa Miezi ya Novemba na Desemba na kuisaidia Yanga kukaa kileleni kwa muda mrefu kabla ya juzi Jumatano kushushwa na Simba.

YANGA YAKUBALI KICHAPO CHA BAO 1-0 DHIDI YA BIASHARA

Yanga imeshindwa kutamba mbele ya Biashara United leo baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara uliopigwa uwanja wa Karume


Bao pekee la Biashara United lilifungwa kwenye dakika ya 8 na Tariq Kiakal baada ya kuwazidi maarifa walinzi wa Yanga waliokuwa wakidhani ameotea
Ulikuwa ni mchezo uliotawaliwa na Biashara United kwa muda mwingi huku mazingira ya uwanja wa Karume yakitajwa kuwa kikwazo kikubwa kwa Yanga

Aidha mvua iliyonyesha wakati mchezo huo ukiendelea iiufanya uwanja uwe na mazingira magumu zaidi mpira kuchezeka kwa upande wa Yanga huku wenyeji wao wakionekana kuzoea hali hiyo
Baada ya mchezo huo Yanga inarejea jijini Dar es salaam kumalizia michezo mitatu iliyobaki

Aidha watani zao Simba nao wameendeleza uteja mbele ya Kagera Sugar baada ya kukabali kipigo cha bao 1-0 kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru

SIMBA YAENDELEZA UTEJA MBELE YA KAGERA SUGAR YAKUBALI KICHAPO CHA BAO 1-0

Kagera Sugar imeendeleza umwamba dhidi ya Simba baada ya leo tena kushinda kwa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru


Bao la kujifunga la beki Mohammed Hussein katika dakika ya 42 liliihakikishia Kagera Sugar alama tatu muhimu ambazo huenda zikawanusuru na janga la kuteremka daraja

Licha ya kosakosa kadhaa kutoka kwa Simba, mchezo huo ulimalizika kwa vijana wa Meckie Mexime kupata ushindi wa pili dhidi ya Simba msimu huu

Hata hivyo bado Simba iko kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya Yanga nayo kuchezea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Biashara United

Mchezo unaofuata ni dhidi ya Azam Fc, utapigwa May 13 katika uwanja wa Uhuru

Simba yaita mashabiki uwanja wa Uhuru

Uongozi wa klabu ya Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Uhuru leo wakati mabingwa hao wa nchi watakapokuwa wakichuana na Kagera Sugar

Simba inahitaji ushindi kwenye mchezo huo ili kuendelea kuukaribia ubingwa ambapo wanahitaji kushinda michezo minne tu

Msemaji wa Simba Haji Manara amesema baada ya kupoteza mchezo wa mkoani Kagera, leo ni zamu ya Wana Msimbazi kufurahi kwenye dimba lao la nyumbani

“Kutesa kwa zamu, zamu yao iliishia Kagera na sisi leo zamu yetu. Wanasimba tujitokeze kwa wingi kuwashangilia wachezaji wetu mwanzo wa mchezo hadi mwisho,” amesema

Licha ya hali ya hewa ya mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es salaam, mchezo huo utapigwa kama ulivyopanga