














Mazoezi ya jana usiku ya As Vita kabla ya kuivaa Simba Sc leo saa 1:00 Usiku katika uwanja wa Taifa






📸: Mazoezi ya mwisho kujiandaa na mchezo wa kesho dhidi ya AS Vita Club. #CAFCL #DoOrDie #NguvuMoja ✊🏽











Zahera ameonekana akiambatana na viongozi wa timu ya Vita Club itakayochuana na Simba hapo kesho
“Hii ni mechi ya kitaifa na ya kimataifa, tunaiwakilisha nchi, kuna kocha yeye kazi yake imekuwa ni kuzunguka na Vita tu na aliaga anaenda kwao Congo hata Iringa hajaenda.
“Hii ni mechi ambayo nchi inajua, Rais anajua, sasa ole wake aendelee kutuharibia mipango,” amesema Manara kwenye mahojiano yake na eFM radio
Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo, Manara amesema kikosi kiko tayari, ari na morali ya wachezaji iko juu kuelekea mchezo huo
Amewataka mashabiki kuwahi mapema uwanja wa Taifa hapo kesho ili wawe sehemu ya historia ambayo Simba imepania kuiandika
Aussems amesema Juuko alipata majeraha na atahitaji kupumzika zaidi ili aweze kuwa sawa kabla ya kuanza kumtumia
“Juuko alipata majeraha, anahitaji kupumzika mpaka Jumatatu. Hivyo hakuna uwezekano wa kumtumia katika mchezo huo wa kesho,” amesema Aussems
Hata hivyo Aussems amethibitisha kuwa kiraka Erasto Nyoni yuko fit kuelekea mchezo huo
“Nyoni alianza mazoezi wiki iliyopita. Hatukusafiri nae kwenda Algeria ili kumpa muda zaidi wa kufanya mazoezi ili aweze kuwa fit”
“Tumefanya nae mazoezi siku hizi mbili, bila shaka atakuwepo Jumamosi”
Nyoni na Okwi walijiunga katika mazoezi ya kikosi cha Simba juzi ambapo wanatarajiwa kujumuishwa katika kikosi kitakachoikabili AS Vita
Kiungo Jonas Mkude ataukosa mchezo huo akitumikia adhabu ya kadi mbili za njano





Vinara wa ligi hiyo Yanga wao watashuka dimbani mkoani Iringa kesho Jumamosi kuikabili Lipuli Fc katika mchezo ambao matokeo ya ushindi yatazidi kuin’garisha timu hiyo kileleni

Jana jioni Simba ilijifua katika uwanja wa Taifa yakiwa ni maandalizi yake ya mwisho katika uwanja huo kabla ya mchezo hapo kesho
Aussems amesema licha ya kuwa tayari wamefikia malengo ya msimu huu ya kutinga hatua ya makundi, lakini wana nafasi adimu ya kutinga robo fainali kama watashinda mchezo huo utakaopigwa mbele ya mashabiki wake takribani elfu 60
“Mimi nipo sawa na hata wachezaji wangu wapo vizuri, ni mechi yenye msisimko sana tunajua tukishinda tutaingia robo fainali na tumesubiri jambo hili kwa miezi 7 sasa,” amesema
“Hata kama matarajio hayakuwa makubwa sisi kufika mbali kwenye ligi ya mabingwa Afrika, lakini bado tuna nafasi kwa hiyo hatuna presha, zaidi presha ipo kwao (AS Vita) kwa sababu ni wanafainali wa kombe la shirikisho mwaka jana na kama hawatafuzu itakuwa jambo baya sana kwao.”
“Hatupo katika hali inayofanana, chochote kitakachotokea ni ziafa kwetu, tuna nafasi adimu ya kucheza mchezo huu muhimu mbele ya mashabiki 60,000 kwa hiyo itakuwa mechi nzuri na wachezaji wapo tayari.”
Mchezo huo utapigwa saa moja usiku sambamba na mchezo kati Al Ahly dhidi ya JS Saoura