Good Morning Mtu wangu wa nguvu leo March 15, 2019, nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za za nyuma za Magazeti ya Tanzania.














Good Morning Mtu wangu wa nguvu leo March 15, 2019, nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za za nyuma za Magazeti ya Tanzania.



















Nyoni aliyerejea kikamilifu baada ya kupona majeraha, amesema upande wao wachezaji wanajifua kikamilifu ili kuhakikisha wanashinda mchezo huo
“Mchezo huu ni fainali kwetu, tunahitaji kushinda ili tuweze kutinga robo fainali. Mawazo yetu yote yako katika mchezo huo,” amesema
“Tunahitaji sana sapoti ya mashabiki wetu. Tunajua wakija kwa wingi wataongeza hamasa kwetu na kutuongezea ari ya kupambana”
Kikosi cha Simba chini ya kocha Patrick Aussems na Msaidizi wake Denis Kitambi leo kimejifua kwenye uwanja wa Taifa ikiwa ni maandalizi yake ya mwisho kwenye uwanja huo kabla ya mchezo keshokutwa
Wapinzani wao AS Vital Club waliwasili jijini Dar es salaam jana ambapo leo wamefanya mazoezi katika viwanja vya Ghymkhana
Timu hiyo itajifua kwenye uwanja wa Taifa kesho
Mzee Akilimali amewaomba wadau wa Yanga na Watanzania wote kwa ujumla wamuombee ili aweze kupona maradhi yanayomsumbua
“Hali yangu sio nzuri. Niko huku Bagamoyo najiuguza maradhi ya kisukari. Mniombee kwani kisukari kinanitesa sana,” Mzee Akilimali amenukuliwa na Spoti Xtra
Mzee Akilimali ni miongoni mwa wanachama wa Yanga vinara wa kutoa maoni juu ya masuala mbalimbali ya klabu hiyo
Wakati mwingine hujikuta akiingia katika mgogoro na wanachama wenzake, wakimtuhumu kuwa ni mpinga maendeleo.
Yanga itaikabili Lipuli Fc bila ya kuwa na mpishi wake huyo wa mabao aliyehusika katika mabao 21 kati ya 45 yaliyofungwa kwenye ligi
Hata hivyo kukosekana kwake hakuwezi kuwa tatizo kwa kikosi cha Mwinyi Zahera kilichosheheni viungo wengi
Mohammed Issa ‘Banka’, Thabani Kamusoko na Haruna Moshi ‘Boban’ wote wanaweza kucheza nafasi yake.
Kwa michezo ya hivi karibuni, Ajib amekuwa akitokea benchi kuongeza nguvu kwenye kipindi cha pili
Changamoto pekee inayoikabili Yanga huenda ikabaki kwenye safu ya ulinzi baada ya kukosekana kwa Andrew Vicent ambaye ni majeruhi na Abdallah Shaibu ‘Ninja’ aliyefungiwa michezo mitatu
Kocha Noel Mwandila huenda akalazimika kumtumia kiraka Said Juma Makapu kwenye nafasi ya ulinzi sambamba na mkongwe Kelvin Yondani.
Pia yupo beki aliyepandishwa kutoka Yanga B Cleosaf Sospeter

Kamati hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh Paul Makonda leo ilikutana katika kikao chake cha pili kilichofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam
Kamati hiyo ina wajumbe 14.

Kikosi cha As Vita Club tayari kipo nchini baada ya kuwasili jana Jumatano usiku tayari kwa mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Klabu bingwa Afrika dhidi ya Simba Sc Jumamosi hii Marchi 16





Djuma aliyewahi kuhudumu Simba akiwa kocha msaidizi kwa misimu miwili, amesema Simba itakayokuwa nyumbani ina kila sababu ya kushinda mchezo huo Jumamosi
“Timu zinazoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu zimetumia vyema viwanja vyao vya nyumbani. Naamini Simba itatumia uwanja wake vizuri pia,” Djuma aliiambia Radio eFM
Djuma aliondolewa Simba mwezi Oktoba mwaka jana baada ya kutofautiana na kocha Mkuu Patrick Aussems.
Nafasi yake tayari imechukuliwa na kocha Denis Kitambi
Djuma anabaki kuwa miongoni mwa makocha waliopita Simba na kukubalika sana na mashabiki wa timu hiyo

Aussems ambaye msimu huu ameiongoza Simba kwa mafanikio makubwa kwa kuweza kuipeleka hatua ya makundi, amedhamiria kuvuka malengo kwa kutinga robo fainali
“Mchezo huu muhimu kuchezwa katika uwanja wetu wa nyumbani mbele ya mashabiki wetu, inatuongezea kujiamini.
“Tuko katika nafasi nzuri zaidi ya kupata ushindi kuliko wapinzani wetu,” amesema Aussems
“Nafahamu mchezo hautakuwa mwepesi kwani wapinzani wetu nao wanahitaji ushindi ili wafuzu”
“Lakini sisi tuna faida ya kupata uungwaji mkono kutoka kwa mashabiki wetu. Ni muhimu mashabiki wakajitokeza kwa wingi uwanjani, wajaze uwanja na watuunge mkono kwa muda wote wa mchezo, ushindi utakuwa upande wetu”
Mshindi wa mchezo kati ya Simba dhidi ya AS Vita atajihakikishia kutinga hatua ya robo fainali na timu itakayoshinda kwenye mchezo kati ya Al Ahly dhidi ya JS Saoura unaopigwa Misri
Matokeo ya sare yatazipa nafasi JS Saoura na Al Ahly kutinga robo fainali

Wawa alipata majeraha ya kifundo cha mguu kwenye mchezo uliopita dhidi ya JS Saoura ambapo Daktari wa Simba Yassin Gembe alisema beki huyo raia wa Ivory Coast pamoja na kiungo Haruna Niyonzima walipata majeraha ya enka kutokana na mazingira ya uwanja wa Agosti 20 ambao una nyasi bandia
Wawa amesema hali yako imeimarika na atacheza mchezo wa Jumamosi
“Niko vizuri sasa, niliumia katika mechi iliyopita kule Algeria, lakini sasa ninaendelea vizuri na nitacheza mechi ya Jumamosi,” amesema
“Naamini tutafanya vizuri kwenye mchezo huo, tutapambana kwa sababu tunataka kuwafurahisha mashabiki wetu na vilevile tunataka kuweka rekodi ya kutinga robo fainali”
Wawa alishiriki mazoezi ya Simba yliyofanyika kwenye uwanja wa Boko Veterans jana jioni