

























BONYEZA HAPA KUITAZAMA MECHI HII LIVE
Kumbuka kubonyeza X au kitufe cha kurudi nyuma endapo utaona matangazo.
PIA KUMBUKA KU UPDATE APP YAKO ILI KUENDELEA KUPATA HABARI ZETU, HII NI KWA WALE WALIO PAKUA APP YETU KUANZIA LEO MCHANA – KURUDI SIKU ZA NYUMA.
BONYEZA HAPA KUITAZAMA MECHI HII LIVE
Kumbuka kubonyeza X au kitufe cha kurudi nyuma endapo utaona matangazo bonyeza.
PIA KUMBUKA KU UPDATE APP YAKO ILI KUENDELEA KUPATA HABARI ZETU, HII NI KWA WALE WALIO PAKUA APP YETU KUANZIA LEO MCHANA – KURUDI SIKU ZA NYUMA.

Zahera aliyazungumza hayo jana baada ya mchezo kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Yanga, mchezo ambao wenyeji waliondoka na ushindi wa bao 1-0
Zahera amesema kwa mfumo huu wa kuzibeba dhahiri baadhi ya timu, ana mashaka na hatma ya mpira wa Tanzania kuwa utaendelea kubaki chini

Waamuzi hao wameteuliwa kushiriki kozi maalum kuanzia Aprili 28 hadi Mei 5 mwaka huu mjini Rabat, Morocco kunolewa kwa ajili ya Fainali za Misri mwezi Juni.
Marefa hao wanatoka nchi 33 na wataingia kwenye kambi maalum ya mafunzo itakayosaidia uteuzi wa orodha ya mwisho ya marefa watakaochezesha fainali za mwaka huu zitakazoanza Juni 21 hadi Julai 19 katika miji ya Alexandria, Cairo, Ismailia na Suez

Kabwili aliyejiunga na Yanga mwaka juzi baada ya kufanya vizuri kwenye michuano ya AFCON U17 iliyofanyika Gabon, mkataba wake na Yanga uko ukingoni na atakuwa huru ifikapo mwezi Juni
Kabwili amepata nafasi ya kucheza zaidi msimu huu baada ya aliyekuwa mlinda lango namba moja Beno Kakolanya kuingia kwenye mgogoro na kocha Mwinyi Zahera
Kwa sasa hapati nafasi mara kwa mara baada ya mlinda lango aliyeimarisha kiwango chake Klaus Kindoki kumpiku
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amepania kukijenga upya kikosi cha Yanga kwa ajili ya msimu ujao na inaelezwa amewaruhusu wachezaji wote wanaotaka kuondoka, waondoke
Yanga huenda ikamsajili mlinda lango wa Bandari Fc, Farouk Shikalo ambaye usajili wake ulipaswa kukamilishwa mwezi Disemba wakati wa dirisha dogo la usajili kabla ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Yanga Hussein Nyika kushindwa kwenye dakika za majeruhi
Shikalo ni miongoni mwa wachezaji wanne ambao Zahera alisikitika kuwakosa katika usajili huo

Yanga imesalia na michezo sita kumaliza msimu huku imchezo mmoja dhidi ya Biashara United ukitarajiwa kupigwa nje ya Dar
Yanga itarejea jijini Dar es salaam kutumia uwanja wa Taifa baada ya kumalizika fainali za AFCON U17 April 28 2019
Zahera amesema watahakikisha wanashinda michezo yote iliyobaki pamoja na kuweka msisitizo zaidi kwenye michuano ya kombe la FA (ASFC) wakitarajia kucheza na Lipuli Fc mwanzoni mwa mwezi wa tano katika mchezo wa nusu fainali
“Unajua mimi nimezunguka nchi nyingi sana Afrika lakini sijawahi kuona maamuzi ya hovyo kama ya waamuzi wa Ligi ya Tanzania, Hakuna haki na kungekuwa na haki nina uhakika sasaivi tungekuwa tushajihakikishia ubingwa”
“Kwa sasa tumesahau yote, tunajipanga kuelekea michezo inayofuata ukiwemo wa Azam Fc ili kuhakikisha tunashinda mechi zote zilizosalia huku tukihakikisha tunatwaa ubingwa wa Kombe la ASFC ili kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mwakani”

Ndanda Fc pia ilipata alama moja moja kwenye michezo dhidi ya Yanga na Simba iliyopigwa katika uwanja huo
Matokeo hayo yameipandisha Ndanda Fc mpaka nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi baada ya kujikusanyia alama 43
Yanga yenye alama 74, imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama nane dhidi ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili ikijikusanyia alama 66
Simba yenye michezo mingi ya viporo, inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 60

Dk Mganga amesema kitaalam, muda huo sio mzuri kwani unaweza ukasababisha madhara makubwa kwa wachezaji yakiwemo matukio ya vifo
“Wachezaji wanapocheza wakati wa jua kali wanakuwa katika hali ya kukausha maji mwilini kwa haraka na hivyo kuwepo na hatari ya kupatwa na shambulio la moyo au kuziba moyo na misuli kukakamaa,” amesema
“Shambulio la moyo linatokana na mwili kulazimishwa kufanya kazi ngumu wakati wa jua kali, moyo unaziba, ulimi unatoka nje, misuri inashindwa kufanya kazi ni hatari kubwa mchezaji anaweza kupoteza maisha uwanjani kama hakutakuwa na mtaalamu mwenye kujua atoe huduma gani”
Dk Mganga ambaye ni Daktari wa Coastal Union, amesema kama kuna ulazima wa kuchezesha mechi hizo katika muda huo basi mwamuzi anaweza kutenga hata dakika moja ya kuwapa nafasi wachezaji kunywa maji utaratibu ambao hutumika kote duniani ambapo mchezo husimamishwa kwenye dakika ya 25-30 kuwapa nafasi wachezaji kunywa maji
Msimu huu baadhi ya michezo ya ligi kuu imekuwa ikipigwa saa nane mchana ili kutoa nafasi kwa michezo mingi kuonyeshwa ‘mbashara’ na Azam TV
Michezo ya ligi iliyopigwa jana ambayo ilihusisha Mtibwa Sugar dhidi ya Yanga na Coastal Union dhidi ya Simba, ilipigwa saa nane mchana ili kuepusha muingiliano wa ratiba na michuano ya AFCON U17 inayoendelea jijini Dar es salaam

Hii ni taarifa njema sana kwa Simba ambayo katika kipindi cha wiki mbili zijazo inakabiliwa na michezo mingi ya viporo inayopigwa ugenini
Mwanzoni mwa mwezi wa tano Simba itarejea kumalizia michezo iliyobaki katika uwanja wa Taifa ambao umepachikwa jina la ‘machinjioni’
Msimu huu Simba imeweka rekodi ya kipekee uwanja wa Taifa kwa kushinda michezo yote iliyocheza kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kulazimishwa sare michezo miwili tu kwenye ligi