































Jana Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahela aliweka wazi kuwa uchaguzi utafanyika May 05 badala ya April 28 kutokana na siku hiyo kutakuwa na mchezo wa fainali za AFCON U17. Uchaguzi huo utasimamiwa na Yanga, wao TFF watakuwa waangalizi tu
Tayari kipenga kimepulizwa na leo fomu zinaanza kutolewa Makao Makuu ya klabu Mtaa wa Twiga na Jangwani jijini Dar es salaam
Hii ni nafasi adhimu kwa Wanayanga kuijenga timu yao upya baada ya mateso ya takribani misimu miwili
Ni wakati kwa Wanachama wenye sifa na uwezo wa kuipeleka Yanga mbele kujitokeza kuchukua fomu
Aidha si vibaya kwa wanachama wengine kushawishiwa wachukue fomu kugombea pale tunapoona wanazo sifa na tuna imani nao
Huu ni wakati wa kuijenga Yanga imara ambayo itakuwa na mafanikio zaidi
Wanachama wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu na siku ya uchaguzi, haipaswi kufanya makosa kwa wapiga kura.
Wanachama watumie muda wao kuwasikiliza wagombea wote wakati wa kampeni ili waweze kuchagua viongozi ambao wataweza kuitoa Yanga hapa ilipo

Mkataba wa Okwi unatarajiwa kumalizika ndani ya siku 60 huku mchezaji huyo raia wa Uganda akionyesha dalili zote za kutaka kuondoka Msimbazi
Okwi anahusishwa na vilabu kadhaa vinavyoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini, Orlando Pirates na Kaizer Chiefs
Kocha Patrick Aussems alimuondoa Okwi katika kikosi kilichokwenda mkoani Morogoro baada ya mchezaji huyo kuchelewa kuripoti kambini
Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema hana taarifa kuhusu mshambuliaji huyo ambaye alikuja nchini na kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda Cranes na alicheza mchezo dhidi ya Stars
“Mimi sijui chochote kuhusiana na Okwi labda waulizwe viongozi wangu wa juu, hayupo kwenye msafara wetu huu unaoelekea Morogoro, hivyo waulizwe viongozi wa juu suala lake,”Rweyemamu alinukuliwa na Championi jana
Hata hivyo Okwi amekuwa na kawaida ya kuchelewa kuripoti kambini kila anapotoka kutimiza majukumu ya timu ya Taifa
Hali ni tofauti kwa Juuko Murshid ambaye tangu aliporejeshwa kikosini, amekuwa akiwajibika ipasavyo
Juuko alikuwa miongoni mwa wachezaji waliowahi kuripoti kambini baada ya kumalizika michezo ya AFCON
Taarifa zilizopatikana mapema leo zimebainisha Okwi amerejea na ameshatua mkoani Morogoro kuungana na wenzake



Okwi na Chama hawakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichoifumua Mbao Fc mabao 3-0 baada ya wachezaji hao kuchelewa kurudi kutoka nchini kwao walikokwenda kutimiza majukumu ya timu ya Taifa
Baada ya mchezo wa kesho, Simba itaendelea kubaki mkoani Morogoro kuendelea na maandalizi ya mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, April 06 kwenye uwanja wa Taifa

Licha ya kukabiliwa na mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa siku ya Jumamosi, April 06 dhidi ya TP Mazembe, TFF imegoma kusogeza mbele mchezo dhidi ya JKT Tanzania ambao utapigwa April 03 2019 kama ulivyopangwa
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema kwa sasa wanaelekeza nguvu zao kuelekea mchezo huo kabla ya kuanza maandalizi ya mchezo dhidi ya TP Mazembe
“Nitalazimika kubadili kikosi ili kila mchezaji apate nafasi kwani baada ya mchezo huo tutakuwa na siku mbili tu za kujiandaa kabla ya kuivaa TP Mazembe,” amesema
Akizungumzia ushindi wa mabao 3-0 ambao Simba ilipata jana dhidi ya Mbao Fc, Aussems alisema mipango yao ni kuhakikisha wanashinda kila mchezo ili waweze kutetea ubingwa hivyo ushindi huo unaendelea kuweka hai mipango yao
“Kila mechi tunacheza kushinda, hata huu mchezo tulistahili kushinda, tulianza kushambulia tangu mwanzo hadi mwisho, mchezo ulikuwa mgumu lakini tulitengeneza nafasi”



















Kocha Mkuu wa vinara hao wa ligi kuu Mwinyi Zahera, amewapa wachezaji mapumziko ya siku moja kabla ya kuendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ndanda Fc
Mchezo huo utapigwa Alhamisi April 04 mkoani Mtwara kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona

Hiki hapa kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani;
