NIYONZIMA : Bado ana nafasi Simba Sc

Kiwango kilichoonyeshwa na kiungo Haruna Niyonzima jana kimedhihirisha mchezaji huyo bado ana sehemu yake kwenye kikosi cha Simba.

Niyonzima aliyecheza kwa dakika 83 mchezo wa kirafiki dhidi ya Nyasa Big Bulltes, alidhihirisha uwezo wake na kuwa miongoni mwa wachezaji walion’gara kwenye mchezo huo.

Mchezo huo uliopigwa dimba la Taifa ulimalizika kwa suluhu ya bila kufungana

Niyonzima amerejea katika kikosi cha Simba mwezi uliopita baada ya kutatua mgogoro baina yake na uongozi wa mabingwa hao wa Tanzania Bara.

Tangu arajee kikosini bado hajaweza kumshawishi kocha Patrick Aussems kuweza kumtumia kwenye michezo ya ligi.

Lakini hali hiyo huenda ikabadilika kwenye michezo ijayo kutokana na juhudi kubwa anazoonyesha sasa.

Kapombe Kuikosa Lesotho

Mlinzi wa kulia wa Simba na timu ya Taifa, Shomari Kapombe amepata majeraha nchini Afrika Kusini kwenye mazoezi ya Stars inayojiandaa kuikabili Lesotho keshokutwa.

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa Simba mapema leo imethibitisha kuhusu kuumia kwa Kapombe

“Mchezaji wetu Shomari Kapombe ameumia na hivyo hatacheza mchezo wa kutafuta tiketi ya kufuzu AFCON 2019 kati ya Tanzania na Lesotho ambao utachezwa siku ya Jumapili 18/11/2018 nchini Lesotho,” imesema taarifa hiyo

Kuumia kwake ni pigo kwa Stars ambayo inasaka ushindi dhidi ya Lesotho katika mchezo wa raundi ya tano kusaka tiketi ya kutinga fainali za AFCON 2019

TFF: Hatumtambui MANJI lazima Uchaguzi Ufanyike

Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF mchana huu limesema kuwa hawatambui kurejea kwa aliyekuwa mwenyekiti wa Yanga Sc Yusuph Manji hivyo uchaguzi utafanyika kama kawaida. .
.
Aidha shirikisho hilo limesisitiza mbele ya waandishi wa habari kuwa zoezi la kuchukua fomu kwaajili ya wagombea wanaowania nafasi zilizowazi ndani ya klabu hiyo linaendelea hivyo kama wanayanga wanamtaka Manji basi achukue fomu na kama wana Yanga wanamtaka basi atapita bila wasiwasi ila cha msingi uchaguzi kufanyika. .
.
Mbali na hilo TFF wamefika mbali zaidi na kusema wamepata taarifa za mkutano wa dharura wa Yanga wanaotarajia kuufanya November 24 na kuhudhuriwa na Yusuph manji, hivyo Manji anatakiwa kuhudhuria kama mwanachama wa Yanga na si kama Mwenyekiti kwani wao wanatambua nafasi ya Mwenyekiti ndani ya Yanga Sc iko wazi.
.
.
Katika hatua nyingine shirikisho hilo limesema litakuwa tayari kushirikiana na kamati ya uchaguzi ya Yanga Sc kusimamia zoezi zima la uchaguzi na si kuwaachia kama wao wanavyotaka kwakuwa walishapata barua kadhaa kutoka TFF kuwataka wafanye uchaguzi lakini hawakufanya, hivyo ni wakati wa TFF kusimamia suala hilo.
#sokaonlineUpdates

Hatima Ya safari ya Cameroon Mikononk mwa STARS

Wakati Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania (Taifa Stars), Mnigeria Emmanuel Amunike, akisema haikuwa rahisi kuwafunga Cape Verde na kurejesha matumaini ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika zitakazofanyika Cameroon mwakani, hesabu za Tanzania kushiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1980 ziko mikononi mwetu.

Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Cape Verde mwezi iliyopita, uliifanya Stars ifikishe alama tano na huenda ushindi kwenye mchezo wa keshokutwa dhidi ya Lesotho utaipeleka Stars Cameroon kutegemea na matokeo ya mchezo wa Uganda dhidi ya Cape Verde.

Kwani kama Uganda itaifunga Cape Verde itafikisha alama 13 huku Stars ikifika alama nane kama itaifunga Lesotho.

Alama hizo haziwezi kufikiwa na Cape Verde wala Lesotho hata zikishinda mchezo mmoja utakaokuwa umebaki.

Stars imeweka kambi nchini Afrika Kusini kwa takribani wiki nzima ikijiandaa na mchezo huo utakaopigwa Jumapili Novemba 18 huko Lesotho.

Kikosi cha Stars kinakwenda Lesotho bila ya nahodha wake Mbwana Samatta ambaye atakosa mchezo huo kutokana na kutumikia adhabu ya kadi mbili za njano.

Amunike amesema wanakwenda Lesotho wakiwa na lengo moja tu la kuhakikisha wanaibuka na ushindi ambao utaisogeza tiketi ya kufuzu karibu zaidi.

Azam Fc Yalamba Matapishi Yake

AZAM YALAMBA MATAPISHI YAKE

Klabu ya Azam FC imeiandika barua ofisi ya Bodi ya Ligi ikiomba mechi zake za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga zichezwe katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Azam wametaja sababu ya kufanya hivyo ni kutokana na uwanja wao (Azam Complex) kuwa mdogo kuingiza mashabiki na watazamaji.

Msimu uliopita 2017/18 zilichezwa mechi mbili (Azam vs Simba na Azam vs Yanga) kwenye uwanja wa Azam Complex, Azam wamekiri kulikuwepo changamoto kubwa iliyotokana na inada kubwa ya watazamaji na kupelekea wengine kukosa kuushuhudia mchezo huo jambo ambalo siyo zuri kwa maendeleo ya mpira wa miguu.

Barua hiyo imeandikwa November 15, 2018 na kusainiwa na Abdulkarim Amin ‘Popat’ Mtendaji Mkuu wa Azam FC.

Tanzania U23 vs Azam Fc : Friend Match

Baada ya kipigo cha bao 2-0 kutoka kwa Burundi, kikosi cha timu ya Taifa ya vijana ya Tanzania U23 kesho kinatarajia kushuka dimbani kuumana na Azam FC.

Mchezo huo wa kirafiki unatarajiwa kuchezwa saa moja usiku katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es salaam.

Akizungumzia kuhusu mchezo huo, Meneja wa Azam FC, Philipo Alando amesema mchezo huo una umuhimu kwa vijana wa Stars U23 na Azam Fc pia.

Tanzania U23 inajiandaa na mchezo wa marudiano wa kusaka tiketi ya kutinga fainali za AFCON 2019 dhidi ya Burundi ikiwa tayari iko nyuma kwa mabao 2-0.

Mchezo huo utapigwa Jumanne ijayo, Novemba 20 2019

Kwa upande wa Azam Fc ni sehemu ya maandalizi kuelekea mchezo wa ligi dhidi ya Ruvu Shooting.