Mazoezi ya mwisho kabla ya kuikabili Kagera Sugar

Kikosi cha Yanga leo kimefanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa CCM Kirumba tayari kwa mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar

Mchezo huo utapigwa kesho Alhamisi katika dimba hilo

Kocha Mkuu wa mabingwa hao wa kihistoria Mwinyi Zahera amesema mazoezi waliyofanya tangu jana yalikuwa ya kuondoa uchovu kwa wachezaji wake

Amesema ana matarajio kuwa vijana wake watakuwa sawa katika mchezo wa kesho baada ya kuwapa mazoezi hayo maalum

Hii ndio kadi rasmi ya kuichangia Yanga

Pichani juu ndio Kadi Rasmi ya Yanga na Lazima iwe na Saini kama inavyoonekana na ina namba chini kulia.

Tahadhari, asitokee mtu akakupa Kadi ili umpe fedha taslimu. Akikupa Kadi nenda kaweke Pesa Bank then mpatie Deposit Slip.

Hii ni kwa wale wanaochangia kuanzia Milioni Moja kupitia mfumo wa Kadi. Ukishadeposit tuma slip kwa namba 0716 881512

Yanga hakuna kulala, yajifua kuikabili Kagera Sugar

Licha ya kushuka dimbani jana, vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga wanakabiliwa na mchezo mwingine dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa keshokutwa Alhamisi April 11 2019 kwenye uwanja wa CCM Kirumba

Kikosi cha Yanga leo kimeendelea na mazoezi katika uwanja wa CCM Kirumba kujiandaa na mchezo huo

Kocha Mwinyi Zahera amesema watahakikisha wanashinda michezo yote nane iliyobaki ili kujiwekea mazingira ya kutwaa ubingwa kwani anaamini upo uwezekano mkubwa kwa Simba kupoteza baadhi ya michezo kutokana na ugumu wa ratiba itakayowakabili kama TFF haitawapendelea

Hawa hapa waliochukua fomu za kuwania uongozi Yanga

Jana April 07 2019 ndio ilikuwa siku ya mwisho kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika klabu ya Yanga kurudisha fomu.

Wagombea 28 walichukua na kurudisha fomu ndani ya muda uliopangwa

Hii hapa orodha ya wagombea wote kulingana na nafasi zao;

MWENYEKITI

Dk Mshindo Msolla

Lucas Mashauri

Elias Mwanjala

MAKAMU MWENYEKITI

Mh Janeth Mbena

Samwel Lukumay

Thobias Lingalangala

Fredrick Mwakalebela

WAJUMBE

Ally Sultan

Saady Mohammed

Hassan Hussein

Siza Lymo

Dminick Albinus

Seko Kingo

Hamad Islam

Shafiru Makosa

Eng Leonard Malango

Cyprian Musiba

Eng Bahati Mwaseba

Nasoro Ally Matuzya

Abdallah Chikawe

Hussein Nyika

Rdgers Gumbo

Said Ntimizi

Palina Conrad

Elias Mkumbo

Suma Mwaitenda

Seif Hassan Seif

Haruna Batenga

NB:

Orodha hii haijumuishi wagombea waliopitishwa kwenye mchakato wa mwanzo wa kujaza nafasi zilizowazi

Kikosi : Yanga Vs African Lyon, TPL

Hiki hapa kikosi cha Yanga mchezo dhidi ya African Lyon

1. Klaus Kindoki

2. Juma Abdul

3. Gadiel Michael

4. Andrew Vicent

5. Kelvin Yondani

6. Faisal Salum

7. Mrisho Ngasa

8. Haruna Moshi

9. Heritier Makambo

10. Papy Tshishimbi

11. Pius Buswita

SUB

Ramadhani Kabwili

Said Juma

Jaffar Mohammed

Thabani Kamusoko

Amissi Tambwe

Raphael Daudi

Mohammed Issa

Yanga yasaka alama tatu dhidi ya African Lyon leo

Vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga leo watakuwa uwanja wa CCM Kirumba kuikabili African Lyon

Huo utakuwa mchezo wa kwanza wa nyumbani kwa Yanga kuchezwa nje ya jiji la Dar es Salaam msimu huu

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema baada ya kulazimishwa sare mchezo uliopita dhidi ya Ndanda Fc, leo wanahitaji alama zote tatu

Viingilio vya mchezo huo ni Tsh 3,000/- kwa majukwaa ya kawaida na Tsh 10,000/- upande wa VIP