Baadhi ya magazeti nchini Zambia yameripoti kuwa klabu ya ZESCO United itamsajili kiungo wa Yanga Papi Tshishimbi mwishoni mwa msimu.
ZESCO inanolewa na kocha wa zamani wa Yanga, George Lwandamina aliyejiunga na timu hiyo mwishoni mwa msimu uliopita.
Mkataba wa Tshishimbi wa kuitumikia Yanga unamalizika mwishoni mwa msimu huu kama Yanga itashindwa kumshawishi asaini mkataba mpya basi huenda akaenda kujiunga na timu hiyo akiwa mchezaji huru.
Alipotua Yanga msimu uliopita akitokea Mbabane Swallows, Tshishimbi alionyesha kiwango cha hali ya juu.
Hata hivyo msimu huu bado haujawa mzuri sana kwake kutokana na kukabiliwa na majeruhi ya mara kwa mara. Ameshindwa kufikia makali yake ya msimu uliopita











