Beki Haji Mwinyi ni miongoni mwa wachezaji wa Yanga ambao mikataba yao inamalizika baada ya mchezo wa mwisho wa ligi
Beki huyo aliyeitumikia Yanga kwa zaidi ya miaka minne, atakuwa huru baada ya Yanga kuumana na Azam Fc wiki ijayo
Amezikaribisha timu zinazohitaji huduma yake kwa ajili ya msimu ujao
“Mkataba wangu na Yanga unamalizika msimu huu. Baada ya hapo nitakuwa huru”
“Nakaribisha klabu yeyote inayohitaji huduma yangu kwa msimu ujao waje tukae mezani tuzungumze, lakini kuhusiana na ofa nilizonazo mezani hadi sasa siwezi kuweka wazi hadi hapo nitakapomaliza msimu wangu kwa michezo miwili iliyobaki,” Mwinyi aliiambia Mwanaspoti
“Sikuwa na namba kikosi cha kwanza, lakini hiyo haina maana kwamba kiwango changu kimeshuka, nipo vizuri na nina uwezo wa kupambana. Kutokana na uzoefu nilionao na naweza kucheza timu yeyote”
Haji Mwinyi hakuwa na wakati mzuri msimu huu katika kikosi cha Zahera akishindwa kutamba mbele ya Gadiel Michael aliyekuwa chaguo la kwanza
Yanga imepanga kutowaongezea mikataba wachezaji ambao hawakucheza angalau nusu ya michezo ya ligi kuu msimu huu













