TFF yapongeza uongozi mpya Yanga

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amewapongeza Viongozi wapya wa Klabu ya Young Africans kwa kuchaguliwa kuiongoza klabu hiyo kwa kipindi cha miaka minne (4)

Karia amesema TFF itashirikiana na Viongozi hao katika maendeleo ya Mpira wa Miguu nchini

Wanachama wa Yanga jana walikamilisha salama mchakato wa uchaguzi wa klabu hiyo kwa kuwachagua Dk Mbette Mshindo Msolla kuwa Mwenyekiti na Fredrick Mwakalebela kuwa Makamu Mwenyekiti pamoja na kuchaguliwa kwa wajumbe wengine nane wa Kamati ya Utendaji

Mchezo wa Lipuli vs Yanga kuanza saa tisa na nusu

TAARIFA

Mchezo wa Nusu fainali ya ASFC uwanja wa Samora Utachezwa leo Kati ya Lipuli na Yanga utaanza saa 9:30 Alasiri (sio saa kumi) kama ilivyopangwa awali.

Hii ni kutokana na kwamba kama kutakuwa na suluhu (sare) baada ya dk 90 kutakuwa na Extra Time na baadaye penalty.

Na viingilio vya mchezo wa leo ni kama ifuatavyo

V.I.P – 20,000
MZUNGUKO 5,000
WATOTO – 2,500

Upatapo taarifa hii usisite kumjulisha na Mwenzio ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza

Imetolewa

ALLY NGALA
Katibu Mkuu IRFA

Viongozi Yanga watua Iringa kuongeza nguvu

Viongozi wapya wa klabu ya Yanga wametimiza ahadi baada ya kuwasili mkoani Iringa kuiunga mkono timu yao inayoshuka uwanja wa Samora kuikabili Lipuli Fc katika mchezo wa nusu fainali kombe la FA

Msafara wa viongozi hao umeongozwa na Mwenyekiti Dk Mbette Mshindo Msolla na Makamu Mwenyekiti Fredrick Mwakalebela pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji

Yanga imeweka mkazo katika kuhakikisha wanatinga fainali na baadae kutwaa taji la kombe la FA ili kupata nafasi ya kushiriki michuano ya CAF msimu ujao

Yanga kuikabili Lipuli Fc ikiwa na mzuka wa kutosha

Yanga iko mkoani Iringa ambapo leo jioni itashuka uwanja wa Samora kuikabili Lipuli Fc katika mchezo wa nusu fainali kombe la FA (ASFC)

Habari njema kwa wachezaji wa Yanga ni kuwa leo watashuka dimbani wakiwa na sapoti ya viongozi wao wapya waliopatikana baada ya uchaguzi jana

Makamu Mwenyekiti Fredrick Mwakalebela anatarajiwa kuwepo uwanjani leo kuwaunga mkono wachezaji kuhakikisha wanashinda mchezo huo

Jana baada ya zoezi la uchaguzi kumalizika, Mwakalebela alisema ataondoka jijini Dar es salaam usiku huo kuwahi mchezo

“Mimi na wenzangu wachache tunaondoka usiku huu kuelekea Iringa kwenda kuwaunga mkono wachezaji wetu. Tunahitaji kushinda mchezo dhidi ya Lipuli ili tuingie fainali”

“Lengo letu ni kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao, tunahitaji kutwaa kombe la FA”

Aidha fedha taslim zaidi ya Mil 20 zilichangishwa na Wanachama wa Yanga jana ili kuipa motisha timu kuelekea mchezo huo

Yanga inahitaji kukomaa na kombe la FA ili kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya CAF msimu ujao

Esperance yatinga fainali ligi ya mabingwa, kucheza na Wydad Casablanca

Esperance imetinga fainali ligi ya mabingwa Barani Afrika baada ya kuiondosha TP Mazembe kwa ushindi wa bao 1-0

Esperance leo imeilazimisha TP Mazembe suluhu ya bila kufungana katika mchezo uliopigwa dimba la Mazembe, Lubumbashi huku ikitoka kushinda bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza

Mamelodi Sundowns pia imeshindwa kupindua matokeo ya 2-1 iliyofungwa na Wydad Casablanca kwenye mchezo wa kwanza baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana

Esperance imetinga fainali kwa msimu wa pili mfululizo sasa itachuana na Wydad Casablanca michezo miwili ya fainali itakayopigwa mwishoni mwa mwsi huu

Igangula ajitoa uchaguzi Yanga

Mgombea mwingine wa nafasi ya Mwenyekiti Baraka Igangula amejiondoa katika kinyan’ganyiro cha nafasi hiyo katika uchaguzi wa Yanga utakaofanyika kesho Jumapili

Inaelezwa Igangula ameamua kumuunga mkono Dk Mshindo Msolla ambaye sasa atachuana na Dk Jonas Tiboroha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga

Dk Msolla amepata uungwaji mkono mkubwa na anapewa nafasi kubwa ya kuibuka kidedea kwenye uchaguzi huo wa kesho

Yanga kupata viongozi wapya kesho

Wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika klabu ya Yanga leo wanahitimisha zoezi la kampeni kuelekea uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika kesho Jumapili ukumbi wa Bwalo la Polisi, Osterbay jijini Dar es salaam

Wagombea walianza kunadi sera zao kwa Wanachama Jumanne iliyopita

Nafasi ya Mwenyekiti wa Yanga inawaniwa na wagombea watatu Barak Igangula, Dk Jonas Tiboroha na Dk Mshindo Msolla wakati nafasi ya Makamu Mwenyekiti inawaniwa na wagombea wanne ambao ni Fredrick Mwakalebela, Janeth Mbene, Titus Osoro na Yono Kevela

Aidha wagombea 21 wanawania nafasi nane za wajumbe wa Kamati ya Utendaji

Wanachama wa Yanga wametakiwa kutofanya makosa kwenye uchaguzi wa kesho kwa kuwachagua viongozi ambao wataweza kuipeleka Yanga mbele

Suala la Mabadiliko limekuwa kilio cha Wanayanga. Wagombea wote wameahidi kufanya mabadiliko, ni jukumu la Wanachama kujiridhisha na uwezo wao na ahadi walizotoa katika kutatua changamoto zinazoikabili Yanga

Wanachama wameaswa kutochagua viongozi kwa mazoea badala yake wachague viongozi ambao wana upeo mkubwa

Ni vyema kiongozi atakayechaguliwa awe na uwezo wa kutengeneza mikakati ya kuipeleka Yanga kule ambako kila mdau anahitaji kuona klabu ikielekea

Huu sio wakati wa kujaribu viongozi, Wanachama wawaweke madarakani ‘watu wa kazi’

Wanachama wasichague viongozi kwa papara, mihemko na makundi, kila mmoja afanye uamuzi kwa maslahi ya klabu kwa kuchagua viongozi wenye tija

Yanga ikipata viongozi wazuri, utakuwa mwanzo wa kutengeneza Yanga imara ambayo itagombewa na wawekezaji na kuifanya timu hiyo kongwe zaidi Tanzania kuondokana na dimbwi la ‘umasikini’