
Habari njema kwa wachezaji wa Yanga ni kuwa leo watashuka dimbani wakiwa na sapoti ya viongozi wao wapya waliopatikana baada ya uchaguzi jana
Makamu Mwenyekiti Fredrick Mwakalebela anatarajiwa kuwepo uwanjani leo kuwaunga mkono wachezaji kuhakikisha wanashinda mchezo huo
Jana baada ya zoezi la uchaguzi kumalizika, Mwakalebela alisema ataondoka jijini Dar es salaam usiku huo kuwahi mchezo
“Mimi na wenzangu wachache tunaondoka usiku huu kuelekea Iringa kwenda kuwaunga mkono wachezaji wetu. Tunahitaji kushinda mchezo dhidi ya Lipuli ili tuingie fainali”
“Lengo letu ni kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao, tunahitaji kutwaa kombe la FA”
Aidha fedha taslim zaidi ya Mil 20 zilichangishwa na Wanachama wa Yanga jana ili kuipa motisha timu kuelekea mchezo huo
Yanga inahitaji kukomaa na kombe la FA ili kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya CAF msimu ujao


















































