Simba yapambanana kuinasa saini ya Justin shonga toka South Africa

credit: @sokaonline_…

HII NI FUJO ISIYOUMIZA: Chukua hii. .

.

Justine Shonga ni jina linalozungumzwa sana katika soko la usajili wa vilabu barani Afrika kwasasa. .

.

Huyu ni mzambia anayekipiga katika klabu ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini. .

.

Ubora wake umefanya aingie kwenye kinyang’anyiro cha baadhi ya vilabu barani Afrika pamoja na baadhi ya vilabu vya ulaya. .

.

Taarifa kutoka Afrika Kusini zinadai Orlando Pirates wapo tayari kumuuza nyota huyo, wababe wa Misri Al Ahly wameonyesha nia ya kumhitaji fundi huyo mwenye udambwi udambwi katika eneo lake la kushambulia. .

.

Lakini zipo taarifa ambazo inasemekana klabu ya Simba nayo imeingia kwenye shindano la kuwania saini yake. Ikumbukwe Mo Dewji ambaye ndiye mwekezaji mkuu wa klabu ya Simba aliwahi kutamka kuwa klabu hiyo ina uwezo wa kushindana na klabu yoyote Afrika kwenye saini za wachezaji. .

.

Simba Sc katika orodha yake ya usajili wa wachezaji wa kigeni imebaki nafasi moja, Unafikiri wataweza kuipata saini yake mbele ya Al Ahly ? Tusubiri tuone. .

.

Takwimu za nyota huyo katika msimu uliopita ni kama zinavyosomeka hapo juu. .

.

Trippier atua rasmi athletico Madrid

credit: @sokawaytz_…

✍️ Rasmi, Kieran Trippier amejiunga na Atletico Madrid kwa Mkataba wa miaka mitatu kutoka Tottenham ya Uingereza… Inafahamika kwamba Atletico imelipa Β£21.7m kama dau la uhamisho wa Beki huyo wa Kimataifa wa Uingereza ambaye alifaulu vipimo vya Afya ndani ya klabu hiyo ya Hispania mapema hii leo Jumatano.

.

– Spurs walipewa fursa ya Kumsajili Mshambuliaji, Angel Correa wakati wa mazungumzo lakini wamechagua kupewa fedha moja kwa moja..Trippier anatoka Tottenham baada ya kucheza Michezo 114 ndani ya misimu Minne..

.

– Muingereza mpya ndani ya Laliga, alikuwepo Patrick Roberts pale Girona kwa mkopo akitoka Man City lakini alitimka na Sasa yupo Norwich City..

#TransferNewsUpdates

@Sokawaytz_

De light akubalina na juventus

_…

JUVENTUS IMEKUBALI KUMSAJILI DE LIGT:

✍🏻 Rasmi, Juventus wamekubaliana na Klabu ya AFC Ajax juu ya uhamisho wa Beki wa Kimataifa wa Uholanzi, Matthijs de Ligt..

.

✍🏻 Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 atawasili Turin hii leo Jumanne na kufanyiwa vipimo vya Afya kesho Jumatano katika dili la uhamisho wenye thamani ya Β£67.5m (€75m) ikiwa ni pamoja na bonasj.

.

✍🏻 Mabingwa hao wa Serie A tayari wamekubaliana Maslahi binafsi na wakala wa De Ligt, Mino Raiola kwamba mchezaji huyo atasaini mkataba wa Miaka Mitano wenye thamani ya Β£10.8m kwa mwaka pamoja na bonuses wakati wake wote akiwa na Miamba hao wa Turin…

#TransferNewsUpdates #SerieATransfersUpdates

Galatasalay wammia kwa mbwana sammata

credit: @sokawaytz_…

– Mabingwa wa Ligi Kuu Nchini Uturuki πŸ‡ΉπŸ‡·, Klabu ya Galatasaray wameingia Katika mbio za kuwania saini ya Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania πŸ‡ΉπŸ‡Ώ, Mbwana Samatta kutoka Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji πŸ‡§πŸ‡ͺ.

.

– Mabingwa hao wanakuwa Ni Klabu ya Nne kumtaka Samatta Ambaye Ni Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania πŸ‡ΉπŸ‡Ώ, Baada ya Leicester City, Cardiff City na Middlesbrough zote za Uingereza.. Genk ipo tayari kumuachia mfungaji wao Bora huyo kwa msimu uliopita akifunga Magoli 32 Kwenye Michuano yote, lakini kwa dau lisilopungua Β£10m (Tshs 28b).

#TransferNewsUpdates

@Sokawaytz_

Azam yadhidi kutakata kagame cup

– Mabingwa Watetezi wa Michuano ya CECAFA Kagame Cup, Klabu ya Azam FC imefanikiwa kutinga hatua ya Nusu fainali ya Michuano hiyo kufuatia kuwatupa nje Mabingwa wa zamani wa Afrika na Mabingwa wa DR Congo πŸ‡¨πŸ‡©, Klabu ya TP Mazembe…

:

FULL-TIME : Azam FC 2-1 TP Mazembe

[Seleman Iddi 27; Obrey Chirwa, 69 | Ipamy Giovanni 21]

.

✍️ Baada Ushindi huo, Azam FC itamjua mpinzani wake Siku ya kesho Mshindi Kati ya APR FC ya Rwanda πŸ‡·πŸ‡Ό au AS Meniema ya kutoka pia DR Congo πŸ‡¨πŸ‡©..

#CECAFAKagameCup #KagameCup2019

Cameroon yamfukuza kucha wao wa timu ya taifa

credit: @sokawaytz_…

OFFICIAL | Shirikisho la Soka Nchini Cameroon πŸ‡¨πŸ‡², Limethibitisha kumfuta kazi ya ukocha mk6uu wa timu yao ya taifa, kocha Clarence Seedorf na Msaidizi wake, Patrick Kluivert, hii imekuja Baada ya Wawili hao kuiongoza timu hiyo ya taifa kutupwa nje ya Fainali za Mataifa ya Afrika “AFCON” huko Misri.

:

– The Indomitable Lions walipokea kipigo Cha Magoli 3-2 dhidi ya Nigeria na kuondoshwa Katika hatua ya 16 Bora, Seedorf na Kluivert waliteuliwa mwezi wa Agosti Mwaka jana wakiiongoza Cameroon πŸ‡¨πŸ‡² kwa Mechi takribani 12 tu…

#Updates

@Sokawaytz_

Paris saint Germany ipo Tayari kumsajili kiungo wa Everton iddris Agey

credit: @sokawaytz_…

– Paris Saint-Germain wamerudi mawindoni kumuwinda Kiungo, Idrissa Gana Gueye wa Everton, Kwa mujibu wa L’Equipe, Gueye anawindwa kwa dau la uhamisho wa €30m (Β£27m / $34m) na majadiliano kati ya timu zote mbili yanaendelea.

:

– PSG walimfuata Gueye mwenye umri wa miaka 29 wakati wa dirisha lililopita la Januari, lakini hawakuweza kupata Saini ya Kiungo huyo wa Kimataifa wa Senegal πŸ‡ΈπŸ‡³.. tayari Everton imeanza majadilio na Klabu ya Southampton wakimtaka Kiungo wao wa Kimataifa wa Gabon πŸ‡¬πŸ‡¦, Mario Lemina Kama mbadala wa Gueye.. kwenye uhamisho wa Lemina watakutana na upinzani kutoka kwa Arsenal na Manchester United ambazo zote zinamuhitaji..

#EPLTransfersUpdates #EPLUpdates