Category: michezo
Bao la Dilunga lawavuruga mashabiki Yanga

Mashabiki wa Yanga wamekuwa wakiiombea ‘dua mbaya’ Simba isishinde michezo yake na pengine wao kuwa na nafasi ya kutwaa ubingwa

Msemaji wa Simba Haji Manara amewataka mashabiki hao waache kuingilia kazi za waamuzi
“Ni jambo la ajabu kusema Simba imependelewa kisa mchezo kuongezwa dakika saba. Dakika hufidiwa pale mwamuzi anapoona muda ulipotezwa isivyo uwanjani,” amesema Manara
Aidha Manara amewakumbusha mashabiki wa timu hiyo kuwa hata wao walipocheza na Lipuli Fc na kukubali kipigo cha bao 1-0 mkoani Iringa, waliongezwa dakika saba
Hesabu za Simba zimeendelea kukaa vizuri kuelekea ubingwa wa pili mfululizo baada ya ushindi wa leo
Simba imefikisha alama 72 ikitofautiana na Yanga kwa alama tano tu huku mabingwa hao watetezi wakiwa na michezo mitano ya viporo
Simba iko katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wake
FT : Simba 1-0 JKT Tanzania

Simba ililazimika kusubiri hadi dakika za nyongeza kujipatia bao la ushindi lililowekwa kambani na Hassani Dilunga huku pasi ya bao ikitotewa na Emmanuel Okwi
JKT Tanzania walitoa upinzani mkali kwa mabingwa hao watetezi lakini uzoefu na kujitolea kwa wachezaji kulifanikisha Simba kuchukua alama zote tatu dakika za majeruhi
Ushindi huo unaifanya Simba izidi kuikaribia Yanga baada ya kufikisha alama 72 ikitofautiana kwa alama tano tu na Yanga inayoongoza ligi




Kituo kinachofuata ni Mbeya ambapo May 03 Simba itashuka dimba la Sokoine kuikabili Mbeya City
Kikosi cha Simba dhidi ya JKT Tanzania, TPL April 30

Hiki hapa kikosi cha Simba kinachoanza mchezo huo;

Magazeti ya leo, Jumanne, April 30 2019














Nimepata maumivu ya kawaida – Gadiel
Gadiel alishindwa kuendelea na mchezo leo dhidi ya Azam Fc baada ya kuumia kwenye kipindi cha kwanza na nafasi yake kuchukuliwa na Jaffar Mohammed
Gadiel amesema alipata mshtuko uliosababisha maumivu ya misuli. Amesema akipata mapumziko ya siku tatu hadi nne atakuwa sawa
“Nimepata maumivu ya kawaida ya misuli, mapumziko ya siku tatu hadi nne yatanisaidia kurejea katika hali yangu ya kawaida,” amesema
Yanga inakabiliwa na mchezo mwingine wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa Alhamisi, May 02 kwenye uwanja wa Taifa
Ninja, Chikupe wawatuliza Chirwa na Ngoma

Walinzi wawili wa kati wa Yanga Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Andrew Vicent ‘Dante’ leo walikuwa na kazi maalum ya kuhakikisha washambuliaji hao hawasababishi madhara
Hakika kazi hiyo wameifanya kwa ustadi mkubwa kwani walifanikiwa ‘kuwaweka mifukoni’ washambuliaji hao
Wakati Ngoma alipata mwanya wa kufunga bao lililokataliwa na mwamuzi baada ya kumfanyia madhambi Chikupe, nafasi pekee aliyopata Chirwa kwenye kipindi cha kwanza iliokolewa kwa ustadi mkubwa na kipa Klaus Kindoki
Ushindi wa Yanga leo umechangiwa kwa kiasi kikubwa na umakini wa walinzi hao na wachezaji wote kwa ujumla ambao walikuwa na nidhamu ya hali ya juu katika ulinzi
Licha ya kumiliki mpira kwa muda mwingi, Azam Fc ilikosa mbinu ya kuipenya ngome ya Yanga
FT : Azam Fc 0-1 Yanga

Ikicheza kwa nidhamu na tahadhari kubwa, Yanga ilifunga bao lake pekee kwenye dakika ya 13 kupitia kwa winga Mrisho Ngasa aliyeunganisha mpira wa krosi uliochongwa na Ibrahim Ajib kutoka winga ya kulia
Krosi hiyo ya Ajib ilikuwa zao la shambulizi la kushitukizwa lililofanywa na Yanga


Ngasa sasa amefikisha mabao 5 msimu huu wakati Ajib ametengeneza bao la 16
Azam Fc ilitawala mchezo huo kwa muda mwingi hata hivyo mbinu ya mahiri ya kujilinda ya kocha Zahera iliwapa wakati mgumu wana ‘rambaramba’ hao kuipenya ngome ngumu ya Yanga iliyokuwa chini ya Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Andrew Vicent ‘Dante’
Azam ilipoteza nafasi pekee adimu kwenye dakika ya 84 baada ya Dani Lyanga kushindwa kuutumbukiza mpira kimiani akiwa amebaki na kipa Klaus Kindoki
Ushindi huo umeendelea kuiweka Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imefikisha alama 77, ikiongoza kwa tofauti ya alama 8 dhidi ya Simba na alama 11 dhidi ya Azam Fc
Mchezo unaofuata ni dhidi ya Tanzania Prisons na utapigwa May 02 kwenye uwanja wa Taifa/Uhuru
KIkosi : Azam Fc vs Yanga, TPL April 29

2. Paulo Godfrey
3. Gadiel Michael
4. Abdallah Shaibu
5. Andrew Vicent
6. Feisal Salum
7. Mrisho Ngasa
8. Mohammed Issa
9. Heritier Makambo
10. Ibrahim Ajib (C)
11. Raphael Daudi

SUB
Ramadhani Kabwili
Juma Abdul
Said Juma
Jaffar Mohammed
Papi Tshishimbi
Amissi Tambwe
Haruna Moshi
Misimu miwili, mabao 35 huyu ndio John Bocco

Bocco aliyetua Simba akitokea klabu ya Azam Fc ambayo aliitumikia kwa takribani miaka 10, nidye kinara wa muda wote wa upachikaji mabao katika ligi ya Tanzania akiwa amefunga mabao zaidi ya 100
Licha ya umri kusonga, Bocco ‘hachuji’, ameendelea kuwa katika ubora uleule wa kupachika mabao
Msimu huu ameifungia Simba mabao 14 kwenye ligi akishika nafasi ya nne katika orodha ya vinara wa upachikaji mabao nyuma ya Meddie Kagere (16), Salim Aiyee (16) na Heritier Makambo (15)
Msimu uliopita Bocco aliifungia Simba mabao 14 na kushika nafasi ya pili nyuma ya Emmanuel Okwi ambaye msimu huu kasi yake ya kuzifumania nyavu imepungua akiwa amefunga mabao 10
Bocco kwa kushirikiana na Kagere na Okwi, wamefungia Simba jumla ya mabao 40 kwenye ligi msimu huu na kuifanya Simba kuwa moto wa kuotea mbali katika kuzifumania nyavu ikiwa imefunga jumla ya mabao 57























