Makonda ‘amtuza’ Manula

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh Paul Makonda ambaye ni mdau mkubwa wa klabu ya Simba, amewapongeza wachezaji wa timu hiyo kwa hatua waliyofikia kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Simba ilitolewa kwenye michuano hiyo jana katika hatua ya robo fainali baada ya kufungwa mabao 4-1 na TP Mazembe

Makonda amesema matokeo hayo hayapaswi kuwavunja moyo bali iwe chachu ya kutafuta mafanikio zaidi

Aidha Makonda amempongeza mlinda lango namba moja Aishi Manula kwa kazi kubwa aliyofanya kwenye mchezo dhidi ya TP Mazembe akiahidi kumpa zawadi

“Najua matokeo ya leo (jana) yatatupa tabu sana mtaani ila wewe (Manula) umekuwa nyota wangu ukifika tu DSM njoo uchukue zawadi yako,” amesema

“Watani zangu Naomba mjuwe hatua tuliyofikia ni kubwa sana na hakika Simba inastahiri kupongezwa na Usku nitakuwepo Airpot kuwapokea Makamanda na wapambanaji wetu Simba”

Nahodha Serengeti Boyz ataka sapoti ya mashabiki

Kikosi cha timu ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 17 Serengeti Boyz leo kinashuka dimba la Taifa kuikabili Nigeria kwenye mchezo wa ufunguzi wa michuano ya AFCON U17, mchezo utakaopigwa saa kumi kamili jioni

Tanzania ni mwenyeji wa michuano hiyo inayoanza kutimua vumbi leo katika viwanja vya Azam Complex na Taifa

Nahodha wa kikosi cha Serengeti Boyz Morris Michael amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi uwanja wa Taifa watakapokuwa wakiikabili Nigeria leo

“Nimezungumza na wenzangu na kuwashusha presha kwamba tunaenda kucheza mchezo wa kawaida kama michezo mingine ambayo tumecheza, kwa hiyo tuuone wa kawaida,” amesema

“Ni mechi kubwa lakini hatutakiwi kuwa na presha, tunatakiwa kupambana hadi mwisho kupata ushindi.”

“Tukishinda mchezo huu tutapata picha nzuri ya matarajio yetu hapo mbele tofauti na tukipoteza au kupata sare.”

“Watanzania waje kutuunga mkono kwa sababu tupo nyumbani naamini tutafanya kitu ambacho watanzania hawataamini”

Viingilio vya mchezo huo VIP ni Tsh 5,000/- na upande wa mzunguuko ni Tsh 2,000/-

Tutatetea ubingwa wetu ili tushiriki tena mwakani – Tshabalala

Nahodha Msaidizi wa kikosi cha Simba Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ amesema hatua ya robo fainali waliyofikia kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika imewapa somo na msimu ujao wakipata nafasi anaamini watafanya vizuri zaidi

Aidha Hussein amesema hatua hiyo imewapa nguvu ya kupambana kwenye ligi ili kuhakikisha wanatetea ubingwa wapate nafasi ya kushiriki michuano hiyo mwakani

“Tulianza kwa Kuandika Kitabu cha Historia Mpya ya Soka Letu baada ya Miaka Mingi Kupita Na Tulitegemea Kuendelea Kukiandika Kitabu Hicho Pale LUBUMBASHI Kabla ya Kukifunga Lakini Haikuwa Bahati,” Tshabalala ameandika kwenye ukurasa wa mtandao wa Instagram

“Uzuri na Utamu wa Mashindano Haya ya CAF CHAMPIONS LEAGUEUnatufanya Kama TEAM Na Mimi binafsi Kupambana Kuhakikisha Mwakani Tunarudi Tena INSHAALLAH”

Simba tayari imerejea nchini kuanza ‘mchakamchaka’ wa kula viporo katika kampeni ya kubakisha ubingwa Msimbazi

FT: Simba 1-4 TP Mazembe

Mchezo wa pili wa robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya TP Mazembe dhidi ya Simba umemalizika kwa wenyeji kusonga mbele hatua ya nusu fainali baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1

Licha ya kutangulia kufunga bao la kuongoza kwenye dakika ya pili kupitia kwa Emmanuel Okwi, Simba ilishindwa kulinda bao hilo huku mfumo wa kujihami zaidi uliotumiwa na kocha Patrick Aussems ukitajwa kuigharimu Simba katika kipindi cha kwanza na kujikuta ikiruhusu mabao mawili mpaka wakati wa mapumziko

TP Mazembe ilitawala zaidi mchezo kwenye kipindi cha pili kwa kutengeneza nafasi nyingi huku ikifanikiwa kutumia nafasi nyingine mbili kujihakikishia ushindi wa mabao 4-1

Licha ya kuondoshwa katika hatua ya robo fainali, mafanikio ya kufika hatua hiyo ni ya kujivunia kwa Simba

Aidha bila shaka Simba itaendeleza hapa ilipoishia kwa kuimarisha zaidi kikosi chake ili kuwa cha ushindani zaidi msimu ujao