
Ikulu ya DR Congo imethibitisha kuwa Tshisekedi atakuwepo uwanjani kushuhudia mchezo huo unaopigwa leo saa kumi kamili jioni
Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Stade TP Mazembe

Ikulu ya DR Congo imethibitisha kuwa Tshisekedi atakuwepo uwanjani kushuhudia mchezo huo unaopigwa leo saa kumi kamili jioni
Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Stade TP Mazembe

Kinara huyo wa kutengeneza mabao ligi kuu huenda akarejea kikosini kwenye mchezo ujao dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa mkoani Morogoro April 17 2019
Kukosekana kwake katika michezo iliyopita kumeibua maswali mengi miongoni mwa mashabiki wa Yanga hasa baada ya kuibuka tetesi kuwa anataka kurudi katika timu yake ya zamani, Simba
Hata hivyo Msemaji wa Yanga Dismas Ten amesisitiza kuwa Ajib amekosa michezo iliyopita kutokana na kuwa majeruhi na si vinginevyo
Amesema atarejea kikosini baada ya kupona majeraha hayo

Ahadi hiyo imetolewa jana na Mlezi wa timu hiyo Dkt.Reginald Mengi pamoja na Kamati ya kuhamasisha ushindi wa timu hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar, es salaam, Paul Makonda.
Serengeti Boys inahitaji kushinda mechi mbili ili kujikatia tiketi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kwa vijana chini ya miaka 17 itakayofanyika nchini Brazil mwaka huu.
Michuano hiyo itafanyika katika viwanja viwili, ambavyo ni Uwanja wa Taifa na Uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Timu shiriki zimepangwa katika makundi mawili, ambapo kundi A lina timu za Tanzania, Nigeria, Angola na Uganda, huku kundi B likiwa na timu za Guinea, Cameroon, Morocco na Senegal.

Simba ina nafasi ya kutinga nusu fainali ya michuano hiyo kama itaibuka na ushindi au kutoka sare yoyote ya mabao
Simba ilitua Lubumbashi mapema jana Ijumaa na jioni kupata nafasi ya kufanya mazoezi katika uwanja wa Mazembe ambao utatumika baadae
Kocha Patrick Aussems amesema kikosi chake kiko tayari kuelekea mchezo huo na amewataka wapenzi, mashabiki wa Simba na Watanzania wote kwa ujumla kuwaombea dua ili waweze kuibuka na ushindi
Ushindi wa Simba leo ni faida kwa Tanzania kwani matokeo hayo yataisaidia Tanzania kuongezewa timu za kushiriki michuano ya CAF kuanzia msimu ujao
Simba tayari imedhihirisha kuwa inaweza kupambana na timu yoyote barani Afrika, mchezo wa leo utadhihirisha mara dufu uimara wa Simba
Kila la kheri Simba, kila la kheri mabingwa wa nchi, kila la kheri wawakilishi wa Tanzania..

















MAKUNDI YOTE SITA: #AFCON2019
Kundi A
Misri
DR Congo
Uganda
Zimbabwe
Kundi B
Nigeria
Guinea
Madagascar
Burundi
Kundi C
Senegal
Algeria
Kenya
Tanzania
Kundi D
Morocco
Ivory Coast
South Africa,
Namibia
Kundi E
Tunisia
Mali
Mauritania,
Angola
Kundi F
Cameroon
Ghana
Benin,
Guinea-Bissau




Kesho Jumamosi Simba itashuka dimba la Mazembe kuwakabili wenyeji wao katika mchezo wa pili wa robo fainali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Simba imetumia usafiri wa Ndege Maalum ya kukodi na wataitumia Ndege hiyo kurejea nchini kesho baada ya mchezo
Mabingwa hao wa Tanzania leo jioni wanatarajia kujifua katika uwanja wa Mazembe ambao utatumika kwenye mchezo wa kesho



Katika droo hiyo, timu zitapangwa kwenye makundi sita ya timu nne nne
Droo ya makundi itafanyika kwa kuchagua timu kutoka kila chungu miongoni mwa vyungu vinne vyenye timu sita sita ambazo zimewekwa kwa kufuata ubora
Tanzania imewekwa kwenye chungu cha nne sambamba na Namibia, Guinea Bissau, Angola, Burundi na Zimbabwe
Timu zinazokuwa kwenye chungu kimoja haziwezi kupangwa kundi moja hivyo Stars haiwezi kupangwa na timu zilizotajwa hapo juu