Watanzania Waombwa kuichangia Taifa STARS

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ iko nchini Afrika Kusini ikiendelea na maandalizi ya mchezo wa kusaka tiketi ya kutinga fainali za AFCON 2019 dhidi ya Lesotho.

Mchezo huo utapigwa Jumapili ijayo, Novemba 18 huko Masseru.

Ili kuhakikisha Stars inafuzu, viongozi wa Shirikisho la soka nchini (TFF) wameomba sapoti ya mashabiki waichangie timu hiyo ili ifanye maandalizi ya uhakika.

Rasmi: Yusuf MANJI Arejea Yanga Sc

Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa Yanga Kapteni George Mkuchika amesema Yussuf Manji amerejea katika nafasi yake baada ya kumuandikia burua ya kukubali ombi la Wanachama wa klabu hiyo kumtaka atengue uamuzi wake wa kujiuzulu

Akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya kikao kilichoitishwa na Baraza hilo, Kapteni Mkuchika ameonyesha barua iliyoandikwa na Manji kuridhia kurejea katika nafasi ya Uwenyekiti wa Yanga.

Kapteni Mkuchika amesema Manji aliandika barua ya kujiuzulu lakini wanachama walilikataa ombi lake kupitia Mkutano halali wa klabu hiyo na kumuomba arejee katika nafasi yake.

Barua hiyo aliyoandika ni uthibitisho kuwa ameridhia maombi ya wanachama wa Yanga na sasa ni rasmi amerejea katika nafasi yake.

Kapteni Mkuchika amesema Manji ndio Mwenyekiti wa Yanga huku Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Thobas Langalanga aliyekuwa ameteuliwa kukaimu wadhifa huo hatambuliki

Full Time : Yanga 1-0 African Lyon

Yanga imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya African Lyon katika mchezo wa kirafiki uliopigwa dimba la Uhuru leo Jumapili.

Bao pekee la Yanga lilifungwa na Pius Buswita kwenye dakika 43 kwa bao maridadi kabisa akiuvusha mpira juu ya mlinda lango aliyekuwa ametoka.

Kwenye mchezo wa leo Yanga iliwapa nafasi wachezaji wake ambao mara kwa mara wamekuwa hawapangwi kwenye kikosi cha kwanza.

Baada ya mchezo huo Yanga itashuka tena dimba la Uhuru Jumatano kuikabili Reha FC kabla ya kusafiri mkoani Lindi kucheza na Namungo Fc.

Michezo yote ni kwa ajili ya kukiandaa kikosi cha Yanga kabla ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mwadui Fc utakaopigwa mkoani Shinyanga Novemba 22, 2018

Manchester United vs Manchester City UPDATES

EPL: Manchester City vs Man United
.
:
Manchester City wanategemea kumrudisha Kun Aguero kikosini baada ya kumpa mapumziko katika mchezo wa UCL vs Shakhtar Donetsk.
Kevin de Bruyne, Eliaquim Mangala na Claudio Bravo wataendelea kuwa nje ya kikosi kutokana na majeruhi. :
Manchester United wataamua kumpa nafasi Lukaku kutokana na ushauri wa daktari kama atakuwa na utimamu wa kiafya.
:
United pia wana wasiwasi mkubwa juu ya utimamu aa kiafya wa Paul Pogba, ambaye hakufanya mazoezi Ijumaa na hata jana hakuonekana kambini katika hotel ya Lowry..
:
Diogo Dalot bado ataendelea kuwa nje – wakati nahodha Tony Valencia amepona na fiti kucheza, jumatano alisafiri na timu kwenda Italy.
:
:
Takwimu:
:
•Tangu walipopoteza Derby iliyopita mnamo April 2018, City wameshinda pointi 25 katika pointi 27 walizokuwa wakishindania kwenye uwanja wa Etihad, wamefunga magoli 32 na kuruhusu magoli manne tu.
:
•Manchester United hawajafungwa katika uwanja wa Etihad katika mechi 3 zilizopita, wameshinda 2 na kutoa sare 1.
:
•Endapo leo Manchester United watashinda – wataweka historia ya kushinda mechi mbili mfululizo katika uwanja aa Etihad kwa mara ya pili. :
•City wameshinda mechi mbili tu dhidi ya Manchester United katika mechi 8 zilizopita za mashindano yote, wamefungwa 4 na sare 2.
:
•Pep Guardiola hajawahi kupoteza mechi mbili mfululizo za ligi zilizochezwa uwanja wa nyumbani dhidi ya timu moja. Je Mourinho ataichafua rekodi hiyo leo usiku saa 1:30. Only on @dstvtanzania

TFF yawatahadharisha Wanaopanga kuvuruga mchakato wa UCHAGUZI Yanga

Mwenyekiti Kamati ya Uchaguzi ya TFF Malangwe Ally Mchungahela amesema wanazo taarifa kuwa kuna wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga kwa kushirikiana na baadhi ya Wanachama wamepanga kuitisha Mkutano kesho Jumapili kutangaza kumtambua Yusufu Manji kuwa Mwenyekiti halali wa Yanga na kupinga uchaguzi wa kujaza nafasi yake.

TFF imewatahadharisha wote wanaopanga ajenda hiyo na kusisitiza kuwa mchakato wa uchaguzi kwa nafasi zote zilizotangazwa utaendelea kama ulivyopangwa.

Mchungahela amesema wote wanatakaoshiriki katika ajenda hiyo watachukuliwa hatua za kinidhamu na TFF bila ya kujali nafasi zao

Aidha, kutokana na kuchelewa kwa zoezi la utolewaji wa fomu, zoezi hilo sasa litafikia tamati Jumatano Novemba 14 baada ya TFF kuongeza siku moja