Kiungo mkabaji wa Yanga, raia wa DRC, Pappy Kabamba Tshishimbi muda huu amesaini mkataba wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea Yanga.
Category: usajili
Breaking News: Mshambuliaji wa Gor Mahia Jacques Tuyisenge amejiunga na klabu ya Petro Atletico ya Angola kwa dau la milioni 400 za Kitanzania (Goal)
Breaking News: Mshambuliaji wa Gor Mahia Jacques Tuyisenge amejiunga na klabu ya Petro Atletico ya Angola kwa dau la milioni 400 za Kitanzania (Goal)
MKUDE Haendi Popote – MO
Mwenyekiti wa Bodi wa Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewatoa hofu wapenzi, wanachama na mashabiki wa timu hiyo juu ya kiungo mkata umeme Jonas Mkude
Mo amesema Mkude ataendelea kubaki Msimbazi
Mkude amekuwa akihusishwa na timu kadhaa ikiwemo klabu ya Yanga inayodaiwa kumuahidi zaidi ya Tsh Milioni 120
“Wanasimba msiwe na wasiwasi, Mkude haendi popote! Jumaah Kareem,” ameandika Mo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram
Mkude ni miongoni mwa wachezaji waliomaliza mikataba Simba na alikuwa akisubiri kusaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Msimbazi
TEN: Awaaga AJIBU, MAKAMBO: Amkaribisha KOUKPO
Heritrier Makambo na Ibrahim Ajib wamebakisha wiki moja tu ya kuitumikia Yanga kwani baada ya mchezo dhidi ya Azam Fc, wachezaji hao hawatakuwa mali ya Yanga
Wakati Makambo akisubiri kutimkia Horoya AC, Ajib anaelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kujiunga na mabingwa wa nchi hiyo, TP Mazembe
Afisa Habari wa Yanga Dismas amewatakia kila la kheri wachezaji hao waliokuwa na mchango mkubwa kwa kikosi cha Yanga msimu huu


Wakati Makambo akifunga mabao 17, Ajib amehusika katika mabao 23, akitengeneza 17 na kufunga sita
Ten amesema wawili hao wangetengeneza ‘combination’ ya hatari na Marcellin Koukpo ambaye anatajwa kusajiliwa na Yanga
“Simba kuna utatu wa Kagere, Bocco na Okwi nawaza sijui ingekuwaje kama nasi tungepata utatu wa Ajib, Makambo na Koukpo”
“Simaanishi kwamba waliokuwepo hawawezi, lakini wakati mwingine si vibaya kuwaza kwa mafanikio ya mwingine. Kikubwa kila timu ijenge kikosi imara ili tuwe na ligi ya ushindani kweli mwakani” amendika Ten kwenye ukurasa wake wa Instagram
Yanga itamkumbuka Ajib kwa mchango wake aliotoa kwa klabu hiyo tangu alipojiunga kutoka Simba misimu miwili iliyopita, wakati Makambo amecheza Yanga kwa msimu mmoja lakini atakumbukwa kwa uhodari wake wa ‘kuzijaza’ mabao timu pinzani
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera ana kazi ya kusaka wachezaji watakaoziba nafasi zao.
Mwenyewe amewatoa hofu mashabiki wa Yanga akiwahakikishia kuwa atasajili wachezaji wenye uwezo sawa au zaidi yao
Majembe ya nje yanayoshuka yanga ni ya KIMATAIFA
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wachezaji wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo wote wanacheza katika timu zao za Taifa
Zahera amesema usajili wa wachezaji wa kigeni umezingatia umuhimu wa kusajili wachezaji ambao wataongeza ushindani na kuinua kiwango cha wachezaji wa ndani
“Miongoni mwa wachezaji tutakaowasajili, sita au saba ni wachezaji wa kigeni. Wageni wote wanaokuja Yanga wanacheza timu za Taifa. Watasaidia kuongeza ushindani wa kikosi chetu na kuinua viwango vya wachezaji wazawa,” amesema
Kuhusu usajili wa wachezaji wa ndani, Zahera amesema hawatafanya usajili mkubwa wa wachezaji wa ndani
“Nafikiri tutasajili wachezaji watatu au wanne wa ndani. Tunao wachezaji wazuri ambao tutawaimarisha ili msimu ujao wawe bora zaidi”
Kuhusu wachezaji wanaoachwa, Zahera amesema wataachana na wachezaji 10 ambao majina yao yatafahamika baada ya kumalizika kwa mchezo wa mwisho wa ligi dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumanne, May 28 2019
NIYONZIMA: Asubiria Mkataba mpya SIMBA
Kiungo fundi Haruna Niyonzima amekuwa kwenye kiwango bora sana. Tangu kuanza kwa mwaka 2019, Niyonzima amekuwa mchezaji wa kutegemewa wa kikosi cha Simba kinachonolewa na Mbelgiji Patraick Aussems
Niyonzima ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika na tayari mazungumzo ya kumuongezea mkataba yameanza
Akiwa miongoni mwa wachezaji walioisaidia Simba kutwaa ubingwa wa pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara, hakuna shaka, ataendelea kubaki Msimbazi
Kiungo huyo wa zamani wa APR, amekiri juu ya kuanza kwa mazungumzo ya mkataba mpya
“Kwa sasa hivi siwezi kuweka kila kitu wazi, muda utakapofika taarifa zitawekwa hadharani, ngoja tumalizie msimu huu kwanza,” alisema Niyonzima
Juzi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ alisema Bodi hiyo ilikuwa ikisubiri ripoti ya kocha Patrick Aussems ili kuanza michakato ya usajili
Inaelezwa tayari Aussems ameshawasilisha ripoti hiyo
TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO IJUMAA
Manchester United wanatarajiwa kumsaini mshambuliaji mshambuliaji Dillon Hoogewerf baada ya kucheza mechi ua vijana wa Ajax. (Metro)
Arsenal ni moja ya vilabu vinavyofuatilia mchezo wa mshambuliaji Danny Loader, 18 raia wa Ungereza. (Goal)
Haki miliki ya pichaSNS
Manchester United wanatarajiwa kumsaini mshambuliaji mshambuliaji Dillon Hoogewerf baada ya kucheza mechi ua vijana wa Ajax. (Metro)
Arsenal ni moja ya vilabu vinavyofuatilia mchezo wa mshambuliaji Danny Loader, 18 raia wa Ungereza. (Goal)
Haki miliki ya pichaSNS
TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO ALHAMISI
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amethibitisha kuwa ataondoka KRC Genk mwishoni mwa msimu huu
⚽Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amethibitisha kuwa ataondoka KRC Genk mwishoni mwa msimu huu, na kwamba klabu 6 za Uingereza na 2 za Hispania zinataka kumsajili, lakini amesema ndoto yake ni kucheza Uingereza.
. .. . . 👉Msimu huu @samagoal77 ameifungia Genk jumla ya magoli 32.
BREAKING NEWS: PEP GUARDIOLA AKIBALI KUTUA JUVENTUS


















