MKUDE Haendi Popote – MO

Mwenyekiti wa Bodi wa Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewatoa hofu wapenzi, wanachama na mashabiki wa timu hiyo juu ya kiungo mkata umeme Jonas Mkude

Mo amesema Mkude ataendelea kubaki Msimbazi

Mkude amekuwa akihusishwa na timu kadhaa ikiwemo klabu ya Yanga inayodaiwa kumuahidi zaidi ya Tsh Milioni 120

Wanasimba msiwe na wasiwasi, Mkude haendi popote! Jumaah Kareem,” ameandika Mo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram

Mkude ni miongoni mwa wachezaji waliomaliza mikataba Simba na alikuwa akisubiri kusaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Msimbazi

TEN: Awaaga AJIBU, MAKAMBO: Amkaribisha KOUKPO

Heritrier Makambo na Ibrahim Ajib wamebakisha wiki moja tu ya kuitumikia Yanga kwani baada ya mchezo dhidi ya Azam Fc, wachezaji hao hawatakuwa mali ya Yanga

Wakati Makambo akisubiri kutimkia Horoya AC, Ajib anaelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kujiunga na mabingwa wa nchi hiyo, TP Mazembe

Afisa Habari wa Yanga Dismas amewatakia kila la kheri wachezaji hao waliokuwa na mchango mkubwa kwa kikosi cha Yanga msimu huu

Wakati Makambo akifunga mabao 17, Ajib amehusika katika mabao 23, akitengeneza 17 na kufunga sita

Ten amesema wawili hao wangetengeneza ‘combination’ ya hatari na Marcellin Koukpo ambaye anatajwa kusajiliwa na Yanga

“Simba kuna utatu wa Kagere, Bocco na Okwi nawaza sijui ingekuwaje kama nasi tungepata utatu wa Ajib, Makambo na Koukpo”

“Simaanishi kwamba waliokuwepo hawawezi, lakini wakati mwingine si vibaya kuwaza kwa mafanikio ya mwingine. Kikubwa kila timu ijenge kikosi imara ili tuwe na ligi ya ushindani kweli mwakani” amendika Ten kwenye ukurasa wake wa Instagram

Yanga itamkumbuka Ajib kwa mchango wake aliotoa kwa klabu hiyo tangu alipojiunga kutoka Simba misimu miwili iliyopita, wakati Makambo amecheza Yanga kwa msimu mmoja lakini atakumbukwa kwa uhodari wake wa ‘kuzijaza’ mabao timu pinzani

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera ana kazi ya kusaka wachezaji watakaoziba nafasi zao.

Mwenyewe amewatoa hofu mashabiki wa Yanga akiwahakikishia kuwa atasajili wachezaji wenye uwezo sawa au zaidi yao

Majembe ya nje yanayoshuka yanga ni ya KIMATAIFA

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wachezaji wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo wote wanacheza katika timu zao za Taifa

Zahera amesema usajili wa wachezaji wa kigeni umezingatia umuhimu wa kusajili wachezaji ambao wataongeza ushindani na kuinua kiwango cha wachezaji wa ndani

“Miongoni mwa wachezaji tutakaowasajili, sita au saba ni wachezaji wa kigeni. Wageni wote wanaokuja Yanga wanacheza timu za Taifa. Watasaidia kuongeza ushindani wa kikosi chetu na kuinua viwango vya wachezaji wazawa,” amesema

Kuhusu usajili wa wachezaji wa ndani, Zahera amesema hawatafanya usajili mkubwa wa wachezaji wa ndani

“Nafikiri tutasajili wachezaji watatu au wanne wa ndani. Tunao wachezaji wazuri ambao tutawaimarisha ili msimu ujao wawe bora zaidi”

Kuhusu wachezaji wanaoachwa, Zahera amesema wataachana na wachezaji 10 ambao majina yao yatafahamika baada ya kumalizika kwa mchezo wa mwisho wa ligi dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumanne, May 28 2019

NIYONZIMA: Asubiria Mkataba mpya SIMBA

Kiungo fundi Haruna Niyonzima amekuwa kwenye kiwango bora sana. Tangu kuanza kwa mwaka 2019, Niyonzima amekuwa mchezaji wa kutegemewa wa kikosi cha Simba kinachonolewa na Mbelgiji Patraick Aussems

Niyonzima ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika na tayari mazungumzo ya kumuongezea mkataba yameanza

Akiwa miongoni mwa wachezaji walioisaidia Simba kutwaa ubingwa wa pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara, hakuna shaka, ataendelea kubaki Msimbazi

Kiungo huyo wa zamani wa APR, amekiri juu ya kuanza kwa mazungumzo ya mkataba mpya

“Kwa sasa hivi siwezi kuweka kila kitu wazi, muda utakapofika taarifa zitawekwa hadharani, ngoja tumalizie msimu huu kwanza,” alisema Niyonzima

Juzi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ alisema Bodi hiyo ilikuwa ikisubiri ripoti ya kocha Patrick Aussems ili kuanza michakato ya usajili

Inaelezwa tayari Aussems ameshawasilisha ripoti hiyo

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO IJUMAA

Liverpool, Manchester United na Arsenal wanataka kumsaini mchezaji nyota wa Colombia James Rodriguez,27,ambaye anatarajiwa kuondoka Bayern Munich mkataba wake wa mkopo utakapokamilika msimu huu. (Mirror)

Rais wa Bayern Munich president Uli Hoeness amethibitisha kuwa mabingwa hao wa Bundesliga wanamtaka winga wa Manchester City Mjerumani Leroy Sane. (Suddeutsche Zeitung – in German)

City wanajiandaa kuweka dau la kumnunua nyota huyo wa miaka 23 kutoka kwa miamba hao wa ujerumani ambalo linatarajiwa kuvunja rekodi. (Mail)

Arsenal wanataka kumsaini winga Ryan Fraser, 25, baada ya fainali ya ligi ya Europa, lakini Bournemouth wanataka kulipwa £30m kumwachilia kiungo huyo wa kimataifa wa Uskochi. (Independent)

Tottenham wamewasiliana na Real Madrid ili kuanza mazungumzo ya kutaka kumnunua kiungo wa kati Marco Asensio, 23, lakini wameambiwa mchezaji huyo rai wa Uhispania hapatikani. (AS – in Spanish)

Marco AsensioHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Marco Asensio (Kulia)
Kocha wa Newcastle Rafael Benitez amewambia Marseille na Roma kuwa kipaumbele chake ni kukubali mkataba mpya St James Park baada ya wao ku kuonesha ari ya kutaka kumpatia kazi ya umeneja. (Chronicle)
Wachezaji Matteo Darmian, 29, Romelu Lukaku 26, Juan Mata, 31, na Marcos Rojo – huenda wakondoka Manchester United msimu huu(Mirror)

Inter Milan itatangaza ofa ya zaidi ya £30m winga wa Croatia winger Ivan Perisic, 30, ili kumnunua Lukaku. (Gazzetta dello Sport – in Italian)

Ivan PerisicHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Ivan Perisic
Manchester City wanataka £15m kumuuza kiungo wa kati Fabian Delph, huku vilabu kadhaa vya ligi ya Premier vikimnyatia nyota huyo wa miaka 29. (Sun)
Mshambuliaji wa Crystal Palace sChristian Benteke, 28, huenda akaondoka Selhurst Park msimu huu baada ya kukubali dau la £15m la kumnuuza nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji kutoka klabu ya China ya Shandong Luneng Taishan. (Times – subscription required)
Christian BentekeHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Christian Benteke(Kulia)
Napoli wanatarajiwa kumsaini beki wa kulia- kushoto wa Tottenham Kieran Trippier, 28, huku Mwingereza huyo akipewa idhini ya kukubali ofa nzuri. (Independent)
Manchester United wanatarajiwa kumsaini mshambuliaji mshambuliaji Dillon Hoogewerf baada ya kucheza mechi ua vijana wa Ajax. (Metro)

Arsenal ni moja ya vilabu vinavyofuatilia mchezo wa mshambuliaji Danny Loader, 18 raia wa Ungereza. (Goal)

Brendan RodgersHaki miliki ya pichaSNS

Image caption Kocha wa Leicester, Brendan Rodgers (Kulia)
Meneja wa Leicester Brendan Rodgers anatathmini uwezekano wa kuungana tena na winga Patrick Roberts, ambaye alicheza chini yake wakati alipokua Celtic. (Sun)
Napoli wanatarajiwa kumsaini beki wa kulia- kushoto wa Tottenham Kieran Trippier, 28, huku Mwingereza huyo akipewa idhini ya kukubali ofa nzuri. (Independent)
Manchester United wanatarajiwa kumsaini mshambuliaji mshambuliaji Dillon Hoogewerf baada ya kucheza mechi ua vijana wa Ajax. (Metro)

Arsenal ni moja ya vilabu vinavyofuatilia mchezo wa mshambuliaji Danny Loader, 18 raia wa Ungereza. (Goal)

Brendan RodgersHaki miliki ya pichaSNS

Image caption Kocha wa Leicester, Brendan Rodgers (Kulia)
Meneja wa Leicester Brendan Rodgers anatathmini uwezekano wa kuungana tena na winga Patrick Roberts, ambaye alicheza chini yake wakati alipokua Celtic. (Sun)

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO ALHAMISI

Nahodha wa zamani wa England na Chelsea John Terry, ambaye kwa sasa ni naibu meneja wa Aston Villa, anashauriana na Middlesbrough kuhusu uwezekano wa kuwa maneja wao mpya.(Talksport)

Manchester City wanakaribia kumsajili beki wa Ureno Joao Cancelo, 24, ambaye thamani yake inakadiriwa na Juventus kuwa euro milioni 60. (Record – in Portuguese)
Atletico Madrid na Napoli wanapania kumsajili beki wa kulia wa Tottenham na mchezaji wa kimataifa wa England Kieran Tripper, 28. (Mirror)

Spurs wameweka dau la £10m kumnunua winga wa Leeds United wa miaka 18, Muingereza Jack Clarke. (Mail)
Manchester United wanashughulikia mpango wa kumsaini Ivan Rakitic, 31, lakini Barcelona wanataka kulipwa uero milioni 48 kumwachilia nyota huyo wa kimataifa wa Croatia. (Record)

Ivan RakiticHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Ivan Rakitic
United wanatarajiwa kuwasilisha dau la kwanza la £25m kumunua beki wa Crystal Palace, Aaron Wan-Bissaka, 21, lakini Eagles wanataka £50m kumwachilia mchezaji huyo. (Evening Standard)

Muargentina Sergio Romero, 32, huenda akapandishwa cheo kuwa kipa wa Manchester United ikiwa David de Gea, 28, ataondoka Old Trafford msimu huu wa joto. (Mail)
United tayari wamewasilisha rasmi ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa Newcastle Sean Longstaff, 21. (ESPN)
Everton, West Ham na Manchester United wamepewa nafasi ya kumsaini kwa mkopo kiungo wa kati wa Uholanzi na Marseille Kevin Strootman, 29. (Sky Sports)
Romelu LukakuHaki miliki ya pichaREUTERS
Image caption Romelu Lukaku
Antonio Conte anatarajiwa kusajili mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, kutoka Manchester United atakapoajiriwa kama meneja wa Inter Milan. (Times – subscription required)

Liverpool wanakaribia kukamilisha mpangowa £200,000 wa kumsajili kipa raia wa Poland Jakub Ojrzynski, 16, kutoka Legia Warsaw. (Liverpool Echo)
Wolves wanaongoza kinyang’anyiro cha kumsaini mshambuliaji Moussa Marega, 28 rai wa Mali ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa £30m-kutoka Porto. (Mirror)

Wales forward Harry WilsonHaki miliki ya pichaBBC SPORT
Newcastle, Southampton na Brighton wote wanataka kusaini winga Harry Wilson, 22, lakini Liverpool wanataka kulipwa £25m kumwachilia nyota huyo wa kimataifa wa Wales. (Sky Sports)

Bournemouth wako tayari kupokea ofa ya kummuuza winga Jordon Ibe, 23 raia wa Uingereza. (Mirror)