



Category: usajili
Man United walia na Ajax kuipata saini ya beki na captain wao kisiki Matthijs de Ligt
– Kwa mujibu wa @skysports, Klabu ya Manchester United Imejitoa katika mbio za kumuwania Beki na nahodha wa Klabu ya Ajax, Matthijs de Ligt.
.
– 
Kwa mujibu wa vyanzo, United ilikuwa tayari kutoa £65m kuinasa saini ya Beki huyo wa timu ya taifa ya Uholanzi mwenye umri wa miaka 19; United imejitoa rasmi kumuwania De Ligt, hivyo kuna uwezekana mkubwa kwa nyota huyo kujiunga na Mabingwa wa Hispania Klabu ya FC Barcelona..
#transfers
credit: @sokawaytz
Kocha simba apewa mkataba mpya

Kocha akisaini mkataba mpya wa mwaka moja kuendelea kuitumikia @simbasctanzania Jee anastairi kupewa mkataba wa mwaka moja au aongezewe zaidi.? #nguvumoja
credit: @simba_view
Benfica imesema haitamuuza nyota wake Joao Felix chini ya dau la £105m msimu huu (Daily Mail) .
Klabu ya Benfica imesema haitamuuza nyota wake Joao Felix chini ya dau la £105m msimu huu (Daily Mail) .
Felix anawaniwa na vilabu ya Man United pamoja na Man City
Simba Sc imeanza kuwania saini ya beki wa Lipuli Fc Willium Lucian “Galas”
Klabu ya Simba Sc imeanza kuwania saini ya beki wa Lipuli Fc Willium Lucian “Galas” ili kuboresha kikosi chao kuelekea kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika msimu ujao. .
Taarifa za awali zinadai kuwa huenda ikaachana na beki wao Zana Coulibaly.
Lamine Moro beki raia wa Ghana ambaye awali aliwahi kufanya majaribio na kikosi cha Simba Sc ametua nchini kumalizana na Yanga Sc tayari kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania.
Lamine Moro beki raia wa Ghana ambaye awali aliwahi kufanya majaribio na kikosi cha Simba Sc ametua nchini kumalizana na Yanga Sc tayari kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania.
HOROYA AC Yamuwahi kuntinyu
Aliyekuwa kiungo wa Azam FC Tafadzwa Kutinyu ambaye alikuwa akihusishwa na Yanga, amesajiliwa na klabu ya Horoya AC, mabingwa wa Guinea
Kutinyu ametua timu hiyo akiwa mchezaji huru baada ya mkataba wake na Azam Fc kumalizika
Kutinyu anaungana na Heritier Makambo ambaye anasubiri kujiunga na timu hiyo baada ya ligi kumalizika
Kutinyu yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Zimbabwe kinachojiandaa na fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika Misri
Kutinyu na Thabani Kamusoko ni wachezaji pekee kutoka Tanzania walioitwa timu ya Taifa ya Zimbabwe
Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba
Kiungo fundi wa Gor Mahia Francis Kahata amegoma kuongeza mkataba katika klabu hiyo huku akihusishwa kusajiliwa na Simba mkataba wake utakapomalizika mwezi wa saba
Msimu huu Kahata ameisaidia Gor Mahia kutwaa taji la ligi kuu ya Kenya pamoja na kuisaidia timu hiyo kufika hatua ya robo fainali kombe la Shirikisho Barani Afrika
Hata hivyo fundi huyo wa mpira anataka kuungana na Meddie Kagere mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia ambaye kwa sasa yuko Simba
Inaelezwa Kagere amemshawishi kiungo huyo ambaye walicheza nae katika klabu ya Gor Mahia
Gor Mahia inakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi na huenda ikawapoteza nyota wake muhimu wanaowania na timu kadhaa
Mshambuliaji tegemeo wa timu hiyo Jacques Tuyisenge yuko mbioni kukamilisha usajili kunako klabu ya Atletico De Luanda ya nchini Msumbiji
Baada ya kumkosa msimu uliopita, Simba ina nafasi nzuri ya kumsajili Kahata msimu huu
Yawezekana na wewe ulikuwa na wasiwasi kuwa Thomas Tuchel angetimuliwa?
Yawezekana na wewe ulikuwa na wasiwasi kuwa Thomas Tuchel angetimuliwa?
:
Hapana. PSG wamemuongezea mkataba mpaka 2021. Licha ya matokeo dhaifu bado wana imani na uwezo wake. Labda nao wamechoshwa na tabia ya kutimua wakufunzi hovyo.
:
💉PSG walipoteza jumla ya mechi 4 ya Ligue 1 kwa misimu miwili 2017 & 2018
💉PSG wamepoteza jumla ya mechi 5 za Ligue 1 ndnai ya msimu mmoja tu 2019
::
✍️Takwimu zake kwa ujumla
– Mechi: 55
– Ushindi: 40
– Vipigo: 9
– Mataji: 2
Nyota wapya yanga wajifua na kikosi cha yanga
Uongozi wa Yanga tayari umewapokea nyota wanne wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema anatarajia kukamilisha usajili wa nyota sita wa kigeni pamoja na wazawa wawili kabla ya kuondoka kwenda DR Congo kujiunga na kambi ya timu ya Taifa
Nyota wa kigeni waliohudhuria mazoezi ya Yanga jana ni pamoja na kiungo mwenye umri wa miaka 20 raia wa Nigeria Victor Patrick Akpan aliyekuwa akikipiga na JKU ya Zanzibar
Akpan yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Nigeria umri chini ya miaka 23
Wengine ni beki wa kati Mohammed Ali Camara mwenye umri wa miaka 21 kutoka klabu ya Horoya AC ya Guinea.
Camara aliitumikia timu ya Taifa ya Guinea U20 na tayari ameitumikia timu ya wakubwa mara moja
Wengine ni mshambuliaji Shehu Magaji Bulama raia wa Nigeria na kiungo Allex Komenan kutoka nchini Ivory Coast
Bulama na Komenan watafanyiwa majaribio na Zahera kabla kuidhinisha kama wasajiliwe au la









