Gormahia yachukua wawili kutoka tanzania

credit: @sokawaytz_…

– Mabingwa wa Ligi Kuu Nchini Kenya, Klabu ya GOR Mahia imevamia Tanzania na Kukamilisha usajili wa Nyota wawili wa Tanzania.. yatua Alliance na Singida United.

.

– K’Ogalo Imethibitisha Rasmi Kumsajili Mlinda lango David Kisu kwa Mkataba wa Miaka Mitatu akitokea Klabu ya Singida United ya mkoani Singida. Kisu mwenye umri wa Miaka 23 pia kabla ya kutua Singada amewahi kuzichezea Simba SC na Toto Africans zote za Tanzania kwa Kipindi tofauti tofauti.

.

– Wakati huo huo, Mshambuliaji wa Klabu ya Alliance FC ya Jijini Mwanza, Dickson Ambundo nae amejiunga na Mabingwa hao wa Keny kwa Mkataba wa Mkopo wa Mmoja..

#TransferNewsUpdates

@Sokawaytz_

Ayoze Perez akatibia kutua Leicester city

_…

– Klabu ya Leicester City ipo hatua za mwisho kulamba dume… Kwa mujibu wa @skysports, Newcastle United imekubali dau la £30m kuuza Mshambuliaji wao matata aliyewaokoa Mara kwa Mara msimu uliopita, Ayoze Perez..

.

– Perez 25, Raia wa Hispania amekubali maslahi binafsi ya kimkataba kujiunga na The Foxes na atafanyiwa vipimo vya afya muda wowote kukamilisha dili hilo.

#EPLTransfersUpdates

Simba yapata chombo kingine toka Tp Mapembe

credit: @dimbani_leo…

Uongozi wa klabu ya Simba umemtambulisha mshambuliaji Deo Kanda aliyejiunga na timu hiyo kwa mkataba wa mwaka mmoja

Kanda anatua Simba kwa mkopo akitokea klabu ya TP Mazembe

Simba imethibitisha usajili wa nyota huyo aliyewahi kuitumikia timu ya Taifa ya DR Congo “Kazi ya kusajili wakali watakaohakikisha kikosi cha Mabingwa kinazidi kuwa tishio kwa wapinzani inaendelea” “Mshambuliaji raia wa Congo DR, Deo Kanda (29) amejiunga na Mabingwa wa nchi. “Kanda amesaini mkataba wa mwaka mmoja kukipiga Msimbazi akitokea TP Mazembe ambapo alikuwa mmoja wa wachezaji ambao waliiwezesha kushinda Ubingwa wa Afrika mwaka 2009, 2010 (aliifungia goli kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Esperance) na 2013 lakini pia akiwa ameshiriki Kombe la Dunia la Vilabu mwaka 2009, 2010, 2013”