Licha ya kuwa na taaluma ya ukocha Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshindo Msolla amemuhakikishia kocha Mwinyi Zahera kuwa hatamuingilia kwenye majukumu yake
Dk Msolla ana taaluma ya ukocha na aliwahi kuinoa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’
“Nimezungumza na kocha kuhusu hili. Nimemuhakikishia awe huru kutekeleza majukumu yake,” amesema
“Nitajikita zaidi katika uongozi kuhakikisha yale niliyoyaahidi wakati wa kampeni tunayatekeleza”
“Tutampa Zahera ushirikiano wote atakaohitaji, na kama atahitaji ushauri wa kiufundi kutoka kwangu basi nitampatia”
Katika hatua nyingine Dk Msolla amesema wameanza mkakati wa kuongeza wanachama kwa kuanzisha matawi mapya
“Tunataka tuhamasishe sana uanzishwaji wa matawi mapya nchi nzima,” amesema
“Tutaigawa mikoa kwenye kanda ambapo kila kanda tutapeleka Mjumbe mmoja wa kamati ya utendaji, mchezaji mmoja wa zamani na mchezaji mmoja anayecheza sasa”
“Tutahakikisha wanapita kina kona ya nchi kushawishi mashabiki wawe wanachama”
Aidha Dk Msolla amesema wataongeza ushiriki wa wanachama katika kufanya maamuzi ya timu hiyo kupitia teknolojia kwa kuwashirikisha hukohuko waliko
Utaratibu wa sasa unawapa zaidi fursa wanachama wa jijini Dar es salaam