
Suala la Ninja liliamuliwa juzi katika kikao cha Kamati hiyo kilichoketi jijini Dar es salaam
Ninja atakosa mchezo wake wa kwanza dhidi ya Lipuli Fc, March 16 2019

Suala la Ninja liliamuliwa juzi katika kikao cha Kamati hiyo kilichoketi jijini Dar es salaam
Ninja atakosa mchezo wake wa kwanza dhidi ya Lipuli Fc, March 16 2019


Katika mchezo wa kesho Yanga itakosa huduma ya mlinda lango wake kinda Ramadhani Kabwili ambaye ni mgonjwa
Hata hivyo, mkufunzi wa makipa Juma Pondamali amesema hana wasiwasi na kusokena kwa Kabwili kwa kuwa Kindoki na Hamid wapo
Yanga itaingia kwenye mchezo wa kesho ikiwa na kumbukumbu ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo wa mzunguuko wa kwanza, bao lililowekwa kimiani na Feisal Salum ‘Fei Toto’ kwa mkwaju wa adhabu kwenye dakika za lala salama
Ligi Kuu ya Tanzania Bara inaendelea leo kwa michezo minne kupigwa kwenye viwanja mbalimbali


Chikupe maarufu kama ‘Dente’ alikuwa nje ya dimba tangu alipopata majeraha kwenye mchezo wa kombe la FA dhidi ya Namungo Fc uliofanyika Februari 24 mkoani Lindi
Yanga inajiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya KMC utakaopigwa keshokutwa Jumapili kwenye uwanja wa Taifa
Vinara hao wa ligi watakuwa na nafasi ya kujikita zaidi kileleni mwa msimamo kwani kama wataibuka na ushindi, watafikisha alama 67
Mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya usajili ya Yanga amesema wamebaini kama watasubiri mpaka mwishoni mwa msimu ambapo mikataba yao itakuwa imemalizika kabisa, kuna uwezekano mkubwa wa kuwapoteza wachezaji hao ambao wako katika mipango ya kocha Mwinyi Zahera kwa ajili ya msimu ujao
“Ajib na Tshishimbi ni wachezaji muhimu ambao kocha anawahitaji kwa ajili ya msimu ujao. Sio hao tu, kocha ametuagiza tuhakikishe wachezaji wote anaowahitaji kwa ajili ya msimu ujao hawachukuliwi na timu nyingine,” alisema Mjumbe huyo wa Kamati ya usajili ambaye hakutaka jina lake liwekwe hadharani kwa kuwa yeye sio msemaji wa Yanga

Hivi karibu imeripotiwa kuwa Simba imeanza mkakati wa kumrejesha Ajib kunako klabu hiyo aliyoikacha mwaka 2017 huku Tshishimbi akihusishwa na mabingwa hao wa ligi kuu msimu uliopita pamoja na klabu ya Azam Fc
Zahera ameuagiza uongozi wa Yanga kuhakikisha unawapa mikataba mipya wachezaji wote anaowahitaji kabla ya msimu kumalizika
Zahera amesema kusubiri mikataba ya wachezaji hao kumalizika kabisa kutaigharimu zaidi Yanga hasa kama wachezaji hao watakuwa wakiwaniwa na timu nyingine
Jana kwenye Mkutano wa viongozi wa matawi ya Yanga, Zahera alisema anakusudia kusajili wachezaji sita wa kigeni ambao mchakato wa usajili wao anakusudia kuukamilisha kabla ya msimu kumalizika
Amewataka Wana Yanga waendelee kuhamasishana katika kuichangia timu hiyo kwani fedha hizo ndizo zitakazotumika katika usajili wa wachezaji hao na wale ambao mikataba yao inaelekea ukingoni
Zahera amesema msimu ujao anataka kutengeneza kikosi imara ambacho kitaipa mafanikio Yanga kwenye ligi na michuano ya Kimataifa.
Kwa sasa Yanga inapigania kupata moja ya nafasi za kuiwakilisha Tanzania kwenye michuano CAF msimu ujao
Kutimiza hilo ni lazima itwae taji la ligi kuu au kombe la FA (ASFC)
Mchezo huo utapigwa keshokutwa Jumapili, March 10 2019 saa kumi kamili jioni katika uwanja wa Taifa
Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema wachezaji 20 wanatarajiwa kuingia kambini leo jioni kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo
Tangu irejee kutoka Mwanza ambako iliichapa Alliance Fc bao 1-0, Yanga imekuwa ikijifua kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es salaam
Ndemla nusura asajiliwe na Yanga katika usajili wa mwanzoni mwa msimu huu kabla hajaamua kubaki Simba kwa kuongeza mkataba wa mwaka mmoja
Jana Ten alifunguka kuhusu tetesi za Yanga kumuwania Ndemla ambapo amekiri kuwa kiungo huyo ana uwezo mkubwa lakini ana bahati mbaya hapati nafasi katika klabu yake ya Simba
“Ndemla ni mchezaji mzuri sana. Mtu yeyote ukimuuliza katika wachezaji wa Tanzania wenye vipaji hawezi kukosa kumtaja Ndemla,” amesema Ten
“Ndemla mimi ni rafiki yangu, suala la kusajili au kutosajiliwa na Yanga hilo linahusu benchi la ufundi na Kamati yetu ya usajili. “
“Yote yanaweza kusemwa mwisho wa msimu lakini kwa sasa hivi huwezi kuzungumza lolote lakini anabaki kuwa ni mchezaji mwenye kipaji na kila mtu anaona”
“Amekuwa ni mchezaji mwenye mwenendo mzuri licha ya kuwa sasa hapati nafasi kwenye timu yake”
Wakati msimu ukielekea ukingoni tayari timu zimeanza ‘kupigana vikumbo’ kuwania wachezajia ambao mikataba yao inaelekea ukingoni
Akizungumza mapema leo katika mazoezi ya Yanga yanayofanyika uwanja wa chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es salaam, Zahera amesema wanaotoa taarifa hizo wana lengo la kuwavunja moyo Wana Yanga ili wasiendelee kuichangia timu yao
“Nawaambia watu wengi wanapenda timu yetu iharibike. Kuna watu wanafanya matangazo mengi ya kusema kama mchango unaofanyika viongozi wanakula pesa”
“Wanasema kuna viongozi wanakula milioni tatu, ni uongo. Hakuna hata elfu moja, senti moja ambayo inatoka katika pesa hiyo ambayo watu wanachangia.” amesema Zahera
“Hakuna hata kiongozi mmoja ambaye ana ruhusa ya kugusa iyo pesa”
Naye nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib amesema hakuna namna yoyote ambayo fedha hiyo inaweza kutolewa bila kuidhinishwa na watia saini watatu ambao ni yeye(Ajib), Kocha Mwinyi Zahera na Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh
“Kama fedha inatakiwa kutolewa ni lazima wote watatu tusaini, hivyo taarifa inayosambazwa ni uongo kwani jambo hilo haliwezekani”
Jana kupitia Redio One, mtu aliyejitambulisha kama mwanachama wa Yanga Suleiman Kato alidai kiasi cha pesa milioni tatu zilizochangwa na mashabiki wa Yanga kupitia mitandao ya simu zilitolewa kwenye mtandao husika na kuhamishiwa kwenye Bank moja iliyopo Kariakoo ambapo aliwatuhumu Kaimu katibu Omary Kaaya pamoja na Mhasibu na baadhi ya viongozi kushirikiana katika hujuma hiyo

Yanga itarudi tena Mwanza katika uwanja huohuo kuikabili Alliance Fc lakini ikiwa ni mchezo wa hatua ya robo fainali
Afisa Habari wa Yanga Dismas Ten amesema hawana hofu ya kuikabili Alliance Fc kwa mara nyingine na watajiandaa kikamilifu ili waweze kushinda mchezo huo na kutinga hatua ya nusu fainali
Baada ya kukosa ushindi kwa misimu kadhaa kwenye dimba la CCM Kirumba, msimu huu Yanga imetakata katika dimba hilo kwa kufanikiwa kuzifunga Mbao Fc na Alliance
“Tunafahamu Mwanza ni pagumu, ili kupata ushindi kwenye uwanja wa CCM Kirumba unapaswa kuwa umejiandaa kwelikweli,” amesema Ten
“Msimu huu tumefanya vizuri katika michezo yote miwili tuliocheza Mwanza, naamini tunao uwezo wa kupata matokeo kwa mara nyingine”
“Tunaiheshimu Alliance, tunafahamu ni timu nzuri lakini kucheza na Yanga ni kitu tofauti”
Kama Yanga itashinda mchezo huo utakaopigwa kati ya March 25-28, kwenye hatua ya nusu fainali itachuana na mshindi kati ya Lipuli Fc dhidi ya Singida United, mchezo ambao utakuwa wa ugenini
Mchezo wa fainali utapigwa uwanja wa Ilulu mkoani Lindi mwishoni mwa msimu
Maamuzi ya Kamati ya Nidhamu ALLIANCE FC