TEN: Awaaga AJIBU, MAKAMBO: Amkaribisha KOUKPO

Heritrier Makambo na Ibrahim Ajib wamebakisha wiki moja tu ya kuitumikia Yanga kwani baada ya mchezo dhidi ya Azam Fc, wachezaji hao hawatakuwa mali ya Yanga

Wakati Makambo akisubiri kutimkia Horoya AC, Ajib anaelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kujiunga na mabingwa wa nchi hiyo, TP Mazembe

Afisa Habari wa Yanga Dismas amewatakia kila la kheri wachezaji hao waliokuwa na mchango mkubwa kwa kikosi cha Yanga msimu huu

Wakati Makambo akifunga mabao 17, Ajib amehusika katika mabao 23, akitengeneza 17 na kufunga sita

Ten amesema wawili hao wangetengeneza ‘combination’ ya hatari na Marcellin Koukpo ambaye anatajwa kusajiliwa na Yanga

“Simba kuna utatu wa Kagere, Bocco na Okwi nawaza sijui ingekuwaje kama nasi tungepata utatu wa Ajib, Makambo na Koukpo”

“Simaanishi kwamba waliokuwepo hawawezi, lakini wakati mwingine si vibaya kuwaza kwa mafanikio ya mwingine. Kikubwa kila timu ijenge kikosi imara ili tuwe na ligi ya ushindani kweli mwakani” amendika Ten kwenye ukurasa wake wa Instagram

Yanga itamkumbuka Ajib kwa mchango wake aliotoa kwa klabu hiyo tangu alipojiunga kutoka Simba misimu miwili iliyopita, wakati Makambo amecheza Yanga kwa msimu mmoja lakini atakumbukwa kwa uhodari wake wa ‘kuzijaza’ mabao timu pinzani

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera ana kazi ya kusaka wachezaji watakaoziba nafasi zao.

Mwenyewe amewatoa hofu mashabiki wa Yanga akiwahakikishia kuwa atasajili wachezaji wenye uwezo sawa au zaidi yao

Majembe ya nje yanayoshuka yanga ni ya KIMATAIFA

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wachezaji wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo wote wanacheza katika timu zao za Taifa

Zahera amesema usajili wa wachezaji wa kigeni umezingatia umuhimu wa kusajili wachezaji ambao wataongeza ushindani na kuinua kiwango cha wachezaji wa ndani

“Miongoni mwa wachezaji tutakaowasajili, sita au saba ni wachezaji wa kigeni. Wageni wote wanaokuja Yanga wanacheza timu za Taifa. Watasaidia kuongeza ushindani wa kikosi chetu na kuinua viwango vya wachezaji wazawa,” amesema

Kuhusu usajili wa wachezaji wa ndani, Zahera amesema hawatafanya usajili mkubwa wa wachezaji wa ndani

“Nafikiri tutasajili wachezaji watatu au wanne wa ndani. Tunao wachezaji wazuri ambao tutawaimarisha ili msimu ujao wawe bora zaidi”

Kuhusu wachezaji wanaoachwa, Zahera amesema wataachana na wachezaji 10 ambao majina yao yatafahamika baada ya kumalizika kwa mchezo wa mwisho wa ligi dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumanne, May 28 2019

NIYONZIMA: Asubiria Mkataba mpya SIMBA

Kiungo fundi Haruna Niyonzima amekuwa kwenye kiwango bora sana. Tangu kuanza kwa mwaka 2019, Niyonzima amekuwa mchezaji wa kutegemewa wa kikosi cha Simba kinachonolewa na Mbelgiji Patraick Aussems

Niyonzima ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika na tayari mazungumzo ya kumuongezea mkataba yameanza

Akiwa miongoni mwa wachezaji walioisaidia Simba kutwaa ubingwa wa pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara, hakuna shaka, ataendelea kubaki Msimbazi

Kiungo huyo wa zamani wa APR, amekiri juu ya kuanza kwa mazungumzo ya mkataba mpya

“Kwa sasa hivi siwezi kuweka kila kitu wazi, muda utakapofika taarifa zitawekwa hadharani, ngoja tumalizie msimu huu kwanza,” alisema Niyonzima

Juzi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ alisema Bodi hiyo ilikuwa ikisubiri ripoti ya kocha Patrick Aussems ili kuanza michakato ya usajili

Inaelezwa tayari Aussems ameshawasilisha ripoti hiyo

ZANA COULIBALY : Amepoteza Kujiamini

Beki Zana Coulibaly ameshindwa kufikia matarajio ya wengi licha ya kupewa muda wa kutosha kuonyesha makali yake

Beki huyo raia wa Burkina Fasa amepoteza kujiamini, akicheza chini ya kiwango katika michezo ya hivi karibuni

Jana katika mchezo dhidi ya Sevilla, Coulibaly alikumbana na wakati mgumu kutoka kwa baadhi ya mashabiki waliokuwa wakimzomea mara kwa mara kila alipogusa mpira

Kocha Patrick Aussems alimfanyia mabadiliko kwenye kipindi cha pili na nafasi yake kuchukuliwa na Nicholas Gyan

Zana alisajiliwa Simba akiwa na matarajio ya kuziba pengo la Shomari Kapombe ambaye bado yuko nje tangu mwishoni mwa mwaka jana alipopata majeraha wakati akiitumikia timu ya Taifa

Beki huyo huenda akawa miongoni mwa wachezaji watakoachwa katika kikosi cha Simba

AUSSEMS: Ataja sababu ya kubadili kikosi kizima mechi ya Sevilla

Jana Simba nusura iondoke na ushindi wa kihistoria dhidi ya Sevilla katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki uliopigwa uwanja wa Taifa ukimalizika kwa Sevilla kushinda mabao 5-4

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alifanya mabadiliko ya wachezaji tisa kwenye kipindi cha pili, mabadiliko yanayotajwa kupunguza kasi ya Simba na kupoteza uongozi wa mchezo huo baada ya kuruhusu mabao matatu ndani ya dakika 10

Kocha Mkuu wa mabingwa hao wa Tanzania Bara Patrick Aussems ametetea uamuzi wake akisema ilikuwa muhimu kwa kila mchezaji kupata nafasi kwani ulikuwa ni mchezo wa kihistoria kwa wachezaji wa Simba

“Nilitaka kila mchezaji acheze dhidi ya timu bora kama ya Sevilla,” Aussems aliwaambia waandishi wa habari

“Niliona ni fursa ya kila mchezaji kuweza kucheza mchezo huu dhidi ya Sevilla ili kuweza kupata Uzoefu zaidi ndio maana niliwapa nafasi wachezaji karibia wote kucheza mechi hii kubwa na ya kihistoria dhid ya klabu bingwa mara tano ligi ya Europa”

Simba iliongoza mchezo huo kwa muda mrefu lakini ikapoteza mchezo mwishoni

Mabao ya Simba yalifungwa na John Bocco (2) aliyeibuka nyota wa mchezo, Meddie Kagere na Clatous Chama

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO IJUMAA

Liverpool, Manchester United na Arsenal wanataka kumsaini mchezaji nyota wa Colombia James Rodriguez,27,ambaye anatarajiwa kuondoka Bayern Munich mkataba wake wa mkopo utakapokamilika msimu huu. (Mirror)

Rais wa Bayern Munich president Uli Hoeness amethibitisha kuwa mabingwa hao wa Bundesliga wanamtaka winga wa Manchester City Mjerumani Leroy Sane. (Suddeutsche Zeitung – in German)

City wanajiandaa kuweka dau la kumnunua nyota huyo wa miaka 23 kutoka kwa miamba hao wa ujerumani ambalo linatarajiwa kuvunja rekodi. (Mail)

Arsenal wanataka kumsaini winga Ryan Fraser, 25, baada ya fainali ya ligi ya Europa, lakini Bournemouth wanataka kulipwa £30m kumwachilia kiungo huyo wa kimataifa wa Uskochi. (Independent)

Tottenham wamewasiliana na Real Madrid ili kuanza mazungumzo ya kutaka kumnunua kiungo wa kati Marco Asensio, 23, lakini wameambiwa mchezaji huyo rai wa Uhispania hapatikani. (AS – in Spanish)

Marco AsensioHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Marco Asensio (Kulia)
Kocha wa Newcastle Rafael Benitez amewambia Marseille na Roma kuwa kipaumbele chake ni kukubali mkataba mpya St James Park baada ya wao ku kuonesha ari ya kutaka kumpatia kazi ya umeneja. (Chronicle)
Wachezaji Matteo Darmian, 29, Romelu Lukaku 26, Juan Mata, 31, na Marcos Rojo – huenda wakondoka Manchester United msimu huu(Mirror)

Inter Milan itatangaza ofa ya zaidi ya £30m winga wa Croatia winger Ivan Perisic, 30, ili kumnunua Lukaku. (Gazzetta dello Sport – in Italian)

Ivan PerisicHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Ivan Perisic
Manchester City wanataka £15m kumuuza kiungo wa kati Fabian Delph, huku vilabu kadhaa vya ligi ya Premier vikimnyatia nyota huyo wa miaka 29. (Sun)
Mshambuliaji wa Crystal Palace sChristian Benteke, 28, huenda akaondoka Selhurst Park msimu huu baada ya kukubali dau la £15m la kumnuuza nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji kutoka klabu ya China ya Shandong Luneng Taishan. (Times – subscription required)
Christian BentekeHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Christian Benteke(Kulia)
Napoli wanatarajiwa kumsaini beki wa kulia- kushoto wa Tottenham Kieran Trippier, 28, huku Mwingereza huyo akipewa idhini ya kukubali ofa nzuri. (Independent)
Manchester United wanatarajiwa kumsaini mshambuliaji mshambuliaji Dillon Hoogewerf baada ya kucheza mechi ua vijana wa Ajax. (Metro)

Arsenal ni moja ya vilabu vinavyofuatilia mchezo wa mshambuliaji Danny Loader, 18 raia wa Ungereza. (Goal)

Brendan RodgersHaki miliki ya pichaSNS

Image caption Kocha wa Leicester, Brendan Rodgers (Kulia)
Meneja wa Leicester Brendan Rodgers anatathmini uwezekano wa kuungana tena na winga Patrick Roberts, ambaye alicheza chini yake wakati alipokua Celtic. (Sun)
Napoli wanatarajiwa kumsaini beki wa kulia- kushoto wa Tottenham Kieran Trippier, 28, huku Mwingereza huyo akipewa idhini ya kukubali ofa nzuri. (Independent)
Manchester United wanatarajiwa kumsaini mshambuliaji mshambuliaji Dillon Hoogewerf baada ya kucheza mechi ua vijana wa Ajax. (Metro)

Arsenal ni moja ya vilabu vinavyofuatilia mchezo wa mshambuliaji Danny Loader, 18 raia wa Ungereza. (Goal)

Brendan RodgersHaki miliki ya pichaSNS

Image caption Kocha wa Leicester, Brendan Rodgers (Kulia)
Meneja wa Leicester Brendan Rodgers anatathmini uwezekano wa kuungana tena na winga Patrick Roberts, ambaye alicheza chini yake wakati alipokua Celtic. (Sun)