Sherehe za Ubingwa Simba Kufanyika Leo

Mabingwa wa nchi Simba leo wanakabidhiwa taji la pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya mchezo dhidi ya Biashara United

Mchezo huo utaanza mapema tu, saa tisa Alasiri ambapo hafla ya makabidhiano ya ubingwa itafanyika baada ya mchezo huo

Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola anatarajiwa kuwa mgeni wa rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika uwanja wa Taifa

Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa leo kushuhudia tukio hilo litakalobaki kwenye kumbukumbu za klabu ya Simba

Hilo ni taji la 20 la ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Simba

Baada ya kuichachafya Sevilla juzi, Aussems amepania kushusha mziki kamili ili kunogesha sherehe za ubingwa kwa ushindi mnono

Viingilio vya mchezo huo, VIP A Tsh 15,000/- VIP B na C Tsh 10,000/- wakati mzunguuko ni Tsh 3,000/-

Kocha wa Sevilla Amvulia Kofia John Bocco, Adai Ana Kiwango Kama cha Drogba

Mkufunzi wa sevia kutoka laliga ya Spain ameshangazwa na uwezo wa john boco drogba kwa kysema hakudhania Kama Tanzania kuna vipaja namna hii!!

Alisema namnukuu “I have never been in east Africa especially Tanzania, I used to know some talented from Africa like drogba and keita but to me that young man with number 22 kit is really magnetic, classical and professional”

Reporter: would you ever sign him?

Why not’ any manager would like to work with “booock’o (Spanish articulation) but i know it is not easy to sign a player from simba which is the richest club in central and east africa

Reporter, three players from simba with best performance tonight boco excluded?

I think kaaagere, nyoni and mkuude performed well

Huyu boco hatari sana tusishangae kesho akalambishwa mkataba na sevia’

Kila la kheri boko umri unaruhusu Wewe bado kijana mdogo na haujapunguza umri

MKUDE Haendi Popote – MO

Mwenyekiti wa Bodi wa Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewatoa hofu wapenzi, wanachama na mashabiki wa timu hiyo juu ya kiungo mkata umeme Jonas Mkude

Mo amesema Mkude ataendelea kubaki Msimbazi

Mkude amekuwa akihusishwa na timu kadhaa ikiwemo klabu ya Yanga inayodaiwa kumuahidi zaidi ya Tsh Milioni 120

Wanasimba msiwe na wasiwasi, Mkude haendi popote! Jumaah Kareem,” ameandika Mo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram

Mkude ni miongoni mwa wachezaji waliomaliza mikataba Simba na alikuwa akisubiri kusaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Msimbazi

SIMBA vs BIASHARA UNITED TAIFA

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Jumamosi, May 25, umehamishiwa uwanja wa Taifa na utaanza saa tisa Alasiri

Mabadiliko hayo yatatoa nafasi kwa Simba kukabidhiwa ubingwa baada mchezo huo kumalizika

Uongozi wa Simba umethibitisha mabadiliko hayo na kuwataka mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi kesho uwanja wa Taifa kupokea ubingwa wa ligi kuu

“Mchezo wa Ligi Kuu ambao tutacheza kesho dhidi ya Biashara United utachezwa katika Uwanja wa Taifa kuanzia saa 9:00 alasiri. Sababu ya mabadiliko ya muda ni sherehe za kukabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu 2018/2019 ambazo zitafanyika baada ya mechi kuisha,” imesema taarifa ya Simba