Kiungo mkabaji wa Yanga, raia wa DRC, Pappy Kabamba Tshishimbi muda huu amesaini mkataba wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea Yanga.
Sherehe za Ubingwa Simba Kufanyika Leo
Mabingwa wa nchi Simba leo wanakabidhiwa taji la pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya mchezo dhidi ya Biashara United
Mchezo huo utaanza mapema tu, saa tisa Alasiri ambapo hafla ya makabidhiano ya ubingwa itafanyika baada ya mchezo huo
Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola anatarajiwa kuwa mgeni wa rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika uwanja wa Taifa
Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa leo kushuhudia tukio hilo litakalobaki kwenye kumbukumbu za klabu ya Simba
Hilo ni taji la 20 la ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Simba
Baada ya kuichachafya Sevilla juzi, Aussems amepania kushusha mziki kamili ili kunogesha sherehe za ubingwa kwa ushindi mnono
Viingilio vya mchezo huo, VIP A Tsh 15,000/- VIP B na C Tsh 10,000/- wakati mzunguuko ni Tsh 3,000/-
Robert Kidiaba Muteba aliyekua mchezaji wa TP Mazembe. Ameteuliwa kuwa Waziri wa michezo wa DRC Congo
Robert Kidiaba Muteba aliyekua mchezaji wa TP Mazembe. Ameteuliwa kuwa Waziri wa michezo wa DRC Congo. Kidiaba alishinda ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.
Breaking News: Mshambuliaji wa Gor Mahia Jacques Tuyisenge amejiunga na klabu ya Petro Atletico ya Angola kwa dau la milioni 400 za Kitanzania (Goal)
Breaking News: Mshambuliaji wa Gor Mahia Jacques Tuyisenge amejiunga na klabu ya Petro Atletico ya Angola kwa dau la milioni 400 za Kitanzania (Goal)
YASOME HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI YA MAY 25/2019
Kocha wa Sevilla Amvulia Kofia John Bocco, Adai Ana Kiwango Kama cha Drogba
Mkufunzi wa sevia kutoka laliga ya Spain ameshangazwa na uwezo wa john boco drogba kwa kysema hakudhania Kama Tanzania kuna vipaja namna hii!!
Alisema namnukuu “I have never been in east Africa especially Tanzania, I used to know some talented from Africa like drogba and keita but to me that young man with number 22 kit is really magnetic, classical and professional”
Reporter: would you ever sign him?
Why not’ any manager would like to work with “booock’o (Spanish articulation) but i know it is not easy to sign a player from simba which is the richest club in central and east africa
Reporter, three players from simba with best performance tonight boco excluded?
I think kaaagere, nyoni and mkuude performed well
Huyu boco hatari sana tusishangae kesho akalambishwa mkataba na sevia’
Kila la kheri boko umri unaruhusu Wewe bado kijana mdogo na haujapunguza umri
.
LUGOLA – Mgeni Rasmi Sherehe za UBINGWA – SIMBA
Simba kesho itakabidhiwa ubingwa wa ligi kuu baada ya mchezo dhidi ya Biashara United utakaopigwa uwanja wa Taifa kuanzia saa tisa Alasiri
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza mgeni wa heshima wa mchezo huo atakuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola

MKUDE Haendi Popote – MO
Mwenyekiti wa Bodi wa Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ amewatoa hofu wapenzi, wanachama na mashabiki wa timu hiyo juu ya kiungo mkata umeme Jonas Mkude
Mo amesema Mkude ataendelea kubaki Msimbazi
Mkude amekuwa akihusishwa na timu kadhaa ikiwemo klabu ya Yanga inayodaiwa kumuahidi zaidi ya Tsh Milioni 120
“Wanasimba msiwe na wasiwasi, Mkude haendi popote! Jumaah Kareem,” ameandika Mo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram
Mkude ni miongoni mwa wachezaji waliomaliza mikataba Simba na alikuwa akisubiri kusaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Msimbazi
SIMBA vs BIASHARA UNITED TAIFA
Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Jumamosi, May 25, umehamishiwa uwanja wa Taifa na utaanza saa tisa Alasiri
Mabadiliko hayo yatatoa nafasi kwa Simba kukabidhiwa ubingwa baada mchezo huo kumalizika
Uongozi wa Simba umethibitisha mabadiliko hayo na kuwataka mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi kesho uwanja wa Taifa kupokea ubingwa wa ligi kuu
“Mchezo wa Ligi Kuu ambao tutacheza kesho dhidi ya Biashara United utachezwa katika Uwanja wa Taifa kuanzia saa 9:00 alasiri. Sababu ya mabadiliko ya muda ni sherehe za kukabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu 2018/2019 ambazo zitafanyika baada ya mechi kuisha,” imesema taarifa ya Simba




























