FT : Kagera Sugar 2-1 Simba

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba leo wamepoteza mchezo wa pili msimu huu baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Kagera Sugar

Kagera Sugar ilikuwa bora zaidi kwenye kipindi cha kwanza ambapo ilipachika mabao yake mawili yaliyofungwa na Kassim Khamis na Ramadhani Kapera

Simba ilikuja juu kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga bao lake kupitia kwa Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 64

Wekundu wa Msimbazi walikosa nafasi kadhaa ambazo zingewawezesha kuondoka na angalau alama moja dhidi ya Kagera Sugar ambayo kwa mara nyingine imedhihirisha umwamba wake dhidi ya Simba

Simba haikuwa katika kiwango bora leo, pengine uchovu uliosababishwa na timu kucheza mfululizo umechangia kukosa matokeo muhimu

Baada ya mchezo huo Simba inaelekea mkoani Mwanza ambapo Jumanne, April 23 itacheza na Alliance Fc

Heri ya sikukuu ya Pasaka kwa Wanamsimbazi

Wakristo nchini, leo wanaungana na wenzao duniani kusherehekea Sikukuu ya Pasaka ya kukumbuka ufufuko wa Yesu Kristo zaidi ya miaka 2,000 iliyopita.

Maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na ibada kwenye makanisa mbalimbali nchini pamoja na burudani zitakazofanyika kumbi tofauti za starehe, fukwe za bahari na sehemu nyingine.

Sherehe hii ambayo kwa Wakristo huwakumbusha upendo, inatakiwa kusherehekewa katika hali ya amani na utulivu.

Tunawatakia Wanamsimbazi na Watanzania wote Pasaka Njema.

Aussems ataja kilichoiponza Simba mchezo dhidi ya Kagera Sugar

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema timu yake haikucheza vizuri kwenye kipindi cha kwanza katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar ambao Simba ilipoteza kwa mara ya pili msimu huu kwa kufungwa mabao 2-1

“Nawapongeza Kagera Sugar kwa sababu walikuwa na mchezo mzuri katika kipindi cha kwanza, sisi hatukuwa bora,” alizungumza Aussems baada ya mchezo jana

“Walitumia udhaifu wetu kuweza kufunga mabao mawili ambayo kwetu haikuwa rahisi kuyarejesha yote kwenye kipindi cha pili licha ya kurekebisha makosa tuliyofanya kwenye kipindi cha kwanza”

“Wachezaji wangu walicheza dakika 45 za kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga bao moja na kutengeneza nafasi nyingine ambao tulishindwa kuzitumia. Hata hivyo mchezo ni dakika 90”

Baada ya mapumziko ya Pasaka, Simba itaelekea mkoani Mwanza kuikabili Alliance Fc kwenye mchezo mwingine wa ligi utakaopigwa keshokutwa April 23 katika dimba la CCM Kirumba

SIMBA YANYUKWA NA KAGERA SUGAR BAO 2-1

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba leo wamepoteza mchezo wa pili msimu huu baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Kagera Sugar
Kagera Sugar ilikuwa bora zaidi kwenye kipindi cha kwanza ambapo ilipachika mabao yake mawili yaliyofungwa na Kassim Khamis na Ramadhani Kapera

Simba ilikuja juu kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga bao lake kupitia kwa Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 64
Wekundu wa Msimbazi walikosa nafasi kadhaa ambazo zingewawezesha kuondoka na angalau alama moja dhidi ya Kagera Sugar ambayo kwa mara nyingine imedhihirisha umwamba wake dhidi ya Simba

Simba haikuwa katika kiwango bora leo, pengine uchovu uliosababishwa na timu kucheza mfululizo umechangia kukosa matokeo muhimu

Baada ya mchezo huo Simba inaelekea mkoani Mwanza ambapo Jumanne, April 23 itacheza na Alliance Fc

Tulishamuondoa Beno kwenye mipango yetu – Kaya

Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga Omary Kaya amesema mlinda lango Beno Kakolanya alishaondolewa kwenye mipango ya Yanga na suala lake liko katika hatua za kumalizwa kisheria

Kaya amesema baada taratibu zote za kishasheria kukamilishwa, Beno atakuwa huru kuendelea na maisha yake ya soka mahali pengine

“Suala la Beno lipo katika sheria zaidi, Yanga na Beno walishaachana kwa sababu angekuwa bado anahitajiwa kufanya kazi Yanga sidhani mpaka leo kama angekuwa nje ya timu,” Kaya ameiambia UFM

“Sidhani kama ni sawa kulizungumzia suala ambalo tayari limeshapita”

“Taratibu nyingine za kumalizana zipo nyuma ya pazia tutamalizana na ataendelea na maisha yake kama ambavyo sasa hivi anavyoendelea na maisha yake na Yanga inaendelea na maisha yake”

Beno aliondolewa kikosini mwishoni mwa mwaka jana baada ya kufanya mgomo uliosababisha mgogoro baina yake na kocha Mwinyi Zahera

Kagera Sugar vs Simba, mchezo wa kisasi leo

Simba mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara, leo Jumamosi saa kumi kamili jioni watashuka kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera kuikabili Kagera Sugar katika mchezo muhimu kwa kila timu

Wakati Simba ikihitaji alama tatu kuendelea kusogea kileleni katika mpango wake wa kutetea ubingwa, Kagera Sugar iko katika hatari ya kuteremka daraja

Lakini pia, ukiachana na mazingira hayo, kwa misimu miwili iliyopita, Kagera Sugar ilihusika katika kuvuruga mipango ya Simba

Msimu wa 2016/17 Kagera Sugar iliisababishia Simba isitwae ubingwa baada ya kunyan’ganywa alama tatu ambazo walikuwa wamepewa awali na Bodi ya Ligi kufuatia Kagera Sugar kumchezesha mchezaji aliyekuwa na kadi tatu za njano katika mchezo ambao Kagera Sugar ilishinda 2-1

Tukio hilo lilisababisha uongozi wa Simba kupeleka malalamiko FIFA, malalamiko ambayo yalitupiliwa mbali

Aidha mwaka jana wakati Simba ikiwa tayari imetangaza ubingwa, Kagera Sugar ikatibua tena siku muhimu kwa mabingwa hao ambayo walikuwa wakikabidhiwa kombe na Rais Dk John Magufuli kwa kuwachapa bao 1-0 kwenye uwanja wa Taifa

Kagera Sugar ndiyo timu pekee iliyopata ushindi dhidi ya Simba msimu uliopita

Msimu huu Simba imejipambanua kwa kuwa na kikosi bora zaidi ikiwa imeshinda michezo yote 11 iliyopita kwenye ligi na kuweka rekodi mpya

Ushindi katika mchezo wa leo utakuwa wa 12

Kocha Patrick Aussems amesema vijana wake wako tayari kuelekea mchezo huo na wamedhamiria kuondoka na alama zote tatu kama walivyofanya katika michezo 11 iliyopita