Tutarekebisha makosa – Ninja

Bekiwa Yanga, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, amewataka mashabiki wa timu hiyo kutokuwa na wasiwasi, kwani kikosi chao kitarekebisha makosa na kufanya vizuri.

Ninja amesema hayo siku moja baada ya Yanga kuchapwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Ninja amewataka mashabiki wa Yanga kuendelea kuwa wavumilivu, kwani wanapambana kwa ajili ya timu hiyo.

“Naomba mashabiki wetu waendelee kuwa wavumilivu, kwani wenyewe wanaona tunavyopambana na hata wanachotufanyia waamuzi,” Ninja amenukuliwa na Bingwa

Alisema kwa sasa matokeo dhidi ya Mtibwa Sugar wameshayasahau na akili zao wamezielekeza kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Azam, ambao utachezwa Aprili 29, mwaka huu.

“Mpira ni mchezo wa makosa, ukifanya kosa moja wenzako wanakuadhibu, ila naamini benchi la ufundi limeona na tutafanyia kazi, ila kikubwa tunaendelea kuvumilia wakati tunazidi kupambana”

Orodha kamili ya wagombea wa nafasi za uongozi Yanga

Baada ya mchujo uliofanyika mapema wiki hii, wagombea waliopita katika mchujo huo wanaunganishwa na wagombea waliopitishwa kwenye mchakato wa kwanza wa kujaza nafasi zilizowazi. Hivyo orodha kamili ya wagombea wote itakuwa kama inavyoonekana hapa chini;

Mwenyekiti

1. Baraka Igagungula (ME)
2. Dr. Jonas Tiboroha (ME)
3. Elias Mwanjala (ME)
4. Dr. Mbette Mshindo Msola (ME)

Makamu Manyekiti

1. Fredrick Mwakalebela (ME)
2.Jannet Mbene (KE)
3. Titus Osoro (ME)
4. Yono Kevela (ME)

Wajumbe

1. Saady Mohamed Khimji (ME)
2. Hassan H. Yahaya (ME)
3. Arafat Hajji (ME)
4. Suma Mwaitenda (KE)
5. Hamad Islam (ME)
6. Dominick Albinus (ME)
7. Sharifu Amour Makosa (ME)
8. Eng. Bahati F. Mwaseba (ME)
9. Eng. Leonard Marango (ME)
10. Haruna H. Batenga (ME)
11. Athanas Kazinghe (ME)
12. Ramadhan Said (ME)
13. Salim Rupia (ME)
14. Dominick Francis (ME)
15. Sharifu Amir (ME)
16. Benjamin Mwakasendo (ME)
17. Christopha Kashiririka (ME)
18. Ally Msigwa (ME)
19. Frank K. Kamugisha (ME)
20. Said Kambi (ME)
21. Silvester Haule (ME).

Mabadiliko makubwa ya kikosi yanakuja Yanga

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amepania hasa kutengeneza kikosi imara ili msimu ujao kuwa na timu itakayotoa ushindani wa kweli kwenye ligi na kwa wapinzani wake Simba ambao kwa msimu wa pili sasa wanaonekana kukosa changamoto

Baada ya kuhakikishiwa ‘fungu la uhakika’ kwa ajili ya kufanya usajili, Zahera amepanga kutengeneza Yanga mpya mapema tu ili wakati anaondoka kwenda Congo kwa ajili ya michuano ya AFCON 2019, aache masuala ya usajili yawe yamemalizika

Mcongomani huyo ana mwezi mmoja tu wa kukamilisha michakato hiyo ambayo tayari imeshaanza kukamilishwa kwa usiri mkubwa

Zahera amepania kufanya mabadiliko makubwa kwenye baadhi ya maeneo ambayo mwenyewe aliyaanisha kuwa na mapungufu

Golikipa

Baada ya ‘kumtosa’ Beno Kakolanya aliyeingia kwenye mgogoro na uongozi, Yanga itasajili mlinda lango mwingine kuziba nafasi yake ambaye atasaidiana na Klaus Kindoki na Ramadhani Kabwili.

Hata hivyo Kabwili nae anawaniwa na timu kutoka Saudi Arabia

Mlindalango wa Bandari Fc Farouq Shikalo anatajwa kuwa kwenye mazungumzo na Yanga

Walinzi wa pembeni

Yanga huenda ikasajili walinzi wawili wa pembeni, mmoja wa kulia mwingine wa kushoto ili kuwaongezea nguvu waliopo

Kwa sasa Yanga inawategemea zaidi Gadiel Michael na Paulo Godfrey huku hatma ya Juma Abdul na Haji Mwinyi ikibaki mikononi mwa Zahera

Mikataba ya wakongwe hao katika kikosi cha Yanga inamalizika mwishoni mwa msimu

Mlinzi wa kati

Eneo la safu ya ulinzi wa kati linatarajiwa kuboreshwa kwa kuongeza mlinzi mwingine licha ya eneo hilo kuwa na walinzi watatu wa kutegemewa Kelvin Yondani, Andrew Vicent na Abdallah Shaibu ‘Ninja’

Mlinzi wa AS Vita Yanick Bangala ambaye yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya DR Congo anatajwa kuwaniwa ili kuongeza nguvu kwenye safu hiyo

Kiungo Mkabaji

Papi Tshishimbi alisajiliwa na Yanga kucheza nafasi ya kiungo mkabaji.

Hata hivyo alipokuja Zahera alimbadilishia majukumu kwa kumchezesha namba 10 au 8 nafasi ambazo amekuwa akifanya vizuri

Feisal Salum ‘Fei Toto’ amekuwa akitumika nafasi ya kiungo mkabaji lakini Zahera alisema analazimika kumtumia kinda huyo kwa kuwa ndiye anayemudu zaidi nafasi hiyo kuliko viungo wengine

Lakini Fei Toto alipaswa kucheza namba nane, na ndio nafasi ambayo kocha wa timu ya Taifa Emmanuel Amunike amekuwa akimtumia kwenye kikosi cha Stars

Yanga huenda ikasajili kiungo mkabaji ‘wa asili’ ambaye pia atakuwa na uwezo wa kucheza nafasi ya ulinzi wa kati

Washambuliaji wa pembeni

Zahera ni muumini wa soka la kushambulia kwa kasi kupitia pembeni na mara kwa mara amelalamika kuwa Yanga haina wachezaji wa nafasi hiyo wanaoendana na mfumo wake na hivyo ndio sababu inayomfanya afanye mabadiliko ya mara kwa mara pembeni

Ni Mrisho Ngasa pekee ambaye kwa sasa amejihakikishia namba kwenye kikosi cha Zahera miongoni mwa washambuliaji wanaotokea pembeni

Yanga huenda ikaongeza viungo washambuliaji wawili wa pembeni kwa kila upande

Safu ya ushambuliaji

Yanga ina washambuliaji wa asili wawili tu, Amissi Tambwe na Heritier Makambo.

Wakati hatma ya Tambwe ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu ikibaki mikononi mwa Zahera, hakuna shaka, safu ya ushambuliaji itaongezewa nguvu

Miongoni mwa washambuliaji wanaotajwa kuwaniwa na Yanga ni Jackues Tuyisenge ambaye mkataba wake na Gor Mahia uko ukiongoni huku ‘mtukutu’ Obrey Chirwa akitajwa kuwa tayari kurejea Yanga baada ya kugoma kuongeza mkataba na Azam Fc. Makataba wake wa miezi sita unamalizika mwishoni mwa msimu

Juzi Zahera alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema kikosi chake cha msimu ujao kitakuwa na mabadiliko makubwa sana, wachezaji wa zamani ambao wataendelea kubaki Yanga hawatazidi 10

Simba kusaka ushindi wa 12 mfululizo Bukoba

Msafara wa wachezaji 18 wa kikosi cha Simba unaondoka leo Ijumaa asubuhi kuelekea Kagera tayari kuwakabili wenyeji wao Kagera Sugar kwenye mchezo utakaopigwa uwanja wa Kaitaba kesho Jumamosi

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema wachezaji wengine wanne watasafiri kesho kuungana na wenzao wanaoondoka leo

Ni beki Paschal Wawa pekee ambaye hakujumishwa kwenye safari hiyo ya kanda ya ziwa kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya nyonga

Baada ya kushinda michezo yote 11 iliyopita na kuweka rekodi mpya kwenye ligi, Simba itakuwa inasaka ushindi wa 12 dhidi ya Kagera Sugar ambayo msimu uliopita ndio timu pekee iliyopata ushindi dhidi ya Simba

Kesho Simba itaingia dimba la Kaitaba ikiwa na kumbukumbu ya kufungwa bao 1-0 kwenye mchezo ambao ulishuhudiwa na Rais Magufuli msimu uliopita

Ratiba haiwezi kutukosesha ubingwa – Aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wamedhamiria kutetea ubingwa wa ligi kuu walioutwaa msimu uliopita hivyo wako tayari kukabiliana na ratiba ngumu ya viporo waliyopangiwa na Bodi ya Ligi

Baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 juzi dhidi ya Coastal Union, kesho Jumamosi Simba itashuka tena uwanjani kumenyana na Kagera Sugar katika mchezo utakaopigwa dimba la Kaitaba mkoani Kagera

Simba imewasili Bukoba mapema leo tayari kwa mchezo huo

Aussems amekosoa mpangilio wa ratiba ikiwemo kupangiwa kucheza saa nane mchana. Hata hivyo amesisitiza kuwa kikosi chake kiko tayari hata wakipangiwa kucheza saa nne asubuhi

“Tumetoka katika kibarua kigumu cha michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, tumekuja kwenye kazi ngumu ya kutetea ubingwa wetu. Tutakabiliana na ratiba tuliyopangiwa hata tukitakiwa kucheza saa nne asubuhi” amesema

“Kuchukua ubingwa si jambo la kuzungumza kwa mdomo, bali linahitaji matendo yenye uthubutu, ikiwa ni pamoja na mipango yake ndani ya kikosi”

Simba inakabiliwa kucheza michezo minne kanda ya ziwa dhidi ya Kagera Sugar, KMC, Alliance Fc na Biashara United kabla ya kuelekea mkoani Mbeya kuzikabili Tanzania Prisons na Mbeya City

HAJI MANARA vs ZAHERA

MICHEZO || Afisa Habari wa klabu ya Simba Sc Haji Manara alitaka shirikisho la soka nchini Tanzania TFF kumchukulia hatua kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Sc Mwinyi Zahera kwa makosa ya kuituhumu Simba Sc na TFF kuwa wanaihujumu klabu yake ya Yanga Sc kwa kuiibia point zao la Ligi kuu Tanzania bara bila kutaja kuwa hizo point wanaiba vipi.