Wakinadada wa Simba Queens leo watashuka kwenye uwanja wa Karume kupepetana na watani zao wa jadi Yanga Princess katika mchezo wa ligi kuu ya Wanawake, Serengeti Lite
Simba Queens inayoshika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo, imepania kuendeleza umwamba dhidi ya wapinzani wao hao ambao wanashika nafasi ya saba
Katika mchezo wa raundi ya kwanza Simba Queens iliibamiza Yanga Princess mabao 7-0
JKT Queens inaongoza ligi ikiwa imejikusanyia alama 45 ikiwa imeshinda michezo yake yote.
Mlandizi Queens inashika nafasi ya pili ikiwa imejikusanyia alama 32 sawa na Alliance Girls timu hizo zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa
Simba Queens iko nafasi ya nne ikiwa na alama 31 wakati Yanga Princess inashika nafasi ya saba ikiwa na alama 19
Wakati alipokabidhiwajukumu la kuinoa Simba mwanzoni mwa msimu, Patrick Aussems alipewa masharti mawili; moja ni kuipeleka Simba hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na pili ni kutetea ubingwa ligi kuu
Aussems amekamilisha sharti la kwanza na kuvuka malengo baada ya kufanikiwa kuivusha Simba hadi robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa
Sharti lililobaki ni la kutetea ubingwa wa ligi kuu, sharti ambalo nalo anaelekea kulikamilisha
Mbelgiji huyo aliyechukua nafasi ya Pierre Lechantre, hakuna shaka atapewa mkataba mpya kuendelea kuinoa Simba kutokana na mafanikio aliyoipatia timu hiyo msimu huu
Mkataba wake na Simba aliosaini msimu uliopatita utamalizika mwishoni mwa msimu
Kiwango cha mshahara anachokitaka kiungo wa Manchester United Paul Pogba, 26, kinaweza kikawa kikwazo kwa Real Madrid kumsajili nyota huyo raia wa Ufaransa. (AS)
Chelsea wannapiga hesabu za kumnyakua kiungo wa Brazil na klabu ya Barcelona Philippe Coutinho, 26, kama mbadala wa mshambuliaji wao raia wa Ubelgiji Eden Hazard, 28, ambaye mwisho wa msimu anatarajiwa kuhamia Real Madrid.(Calciomercato)
Klabu ya Manchester United ipo tayari kumpandisha Mike Phelan mpaka kuwa mkurugenzi wa ufundi, na nafasi yake ya meneja msaidizi kupewa kiongo wa zamani wa klabu hiyo Michael Carrick. (Mail)
Mchezaji nyota wa zamani wa Arsenal ambaye pia alitimuliwa kwenye kazi ya ukufunzi na klabu ya Monaco, Thierry Henry, 41, yumo kwenye mazungumzo na klabu ya New York Red Bulls ya ligi ya soka Marekani ili kujiunga nao kama mkufunzi. (Sky Sports)
Mshambuliaji nyota wa Ufaransa na klabu ya PSG Kylian Mbappe, 20, amekanusha uvumi ulioenea kuwa ana mpago wa kuhamia Real Madrid. Mbappe ametoa kauli hiyo baada ya kuifunga goli tatu timu yake ya zamani Monaco. (Goal.com)
Beki raia wa Brazil Marcelo, amesisitiza kuwa hana mpango wa kuihama klabu yake ya Real Madrid mwishoni mwa msimu – licha ya uvumi kuenea kuwa mchezaji huyo alikuwa akitammani kuungana tena na Cristiano Ronaldo, katika klabu ya Juventus. (Bein Sports, via Mirror)
Image captionMarcelo (kulia) ameamua kuuzima uvumi kuwa anajipanga kuhamia Juventus mwishon mwa msimu.
Kocha wa muda mrefu wa wachezaji chipukizi wa Aston Villa Sean Kimberley ameikacha klabu hiyo. (Birmingham Mail)
Bosi wa Newcastle Rafa Benitez amedai kuwa mfumo wa mishahara wa klabu hiyo unaifanya timu isiwe na matokeo mazuri kwenye Ligi ya Premia. (Newcastle Chronicle)
Image captionRafa Benitez amekuwa akihusishwa na mipango ya kuihama Newcastle
Mshambuliaji wa Newcastle raia wa Uhispania Ayoze Perez, 25, ameashiria kuwa anataka kuihama klabu hiyo mwushoni mwa msimu. (Mirror)
Rais wa klabu ya Nice ya Ufaransa Gauthier Ganaye amesema klabu yake huenda ikamsajili mshambuliaji wa Chelsea Olivier Giroud, 32. (Goal.com
Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kurejea mazoezini kesho Jumanne kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Azam Fc utakaopigwa Jumatano ijayo April 29 katika uwanja wa Taifa
Kocha Mkuu wa vinara hao wa ligi Mwinyi Zahera aliwapa wachezaji siku tatu za mapumziko ili washeherekee sikukuu ya Pasaka wakiwa na familia zao
Mratibu wa Yanga Hafidh Saleh amesema baada ya mapumziko hayo, kesho wataanza kujifua uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini kujiandaa na mchezo huo
Yanga bado haijakata tamaa katika mbio za kuwania ubingwa licha ya watani zao Simba kuwa na idadi kubwa ya michezo ya viporo ambayo kama watashinda yote, watatetea ubingwa waliotwaa msimu uliopita
Juzi Zahera alisema hesabu zao ni kushinda michezo yote sita iliyobaki huku akiamini wapinzani wao Simba wataendelea kudondosha pointi hivyo kuwapa mwanya wa kutwaa ubingwa
Yanga iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imejukusanyia alama 74 baada ya kushuka dimbani mara 32.
Inafuatiwa na Azam Fc yenye alama 66 ikiwa imeshuka dimbani mara 32 pia. Simba inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 60 ilizovuna katika michezo 24
Baada ya kuwasili jijini Mwanza mapema leo, jioni kikosi cha Simba kiliendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Alliance Fc
Mchezo huo utapigwa keshokutwa, April 23 2019 katika uwanja wa CCM Kirumba
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amemtaka Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara kutofuatilia mambo yasiyomhusu.
Kauli ya Zahera imekuja kufuatia Manara kumsema kocha huyo kuwa amekuwa akiishutumu bodi ya ligi na TFF kuwa inafanya mpango wa kuiwezesha Simba kuchukua ubingwa wa ligi.
Ameeleza kwa kumtaka Manara ni vema akafuatilia mambo yanayomhusu na kuachana na kumzunguzia yeye kwani anaona anachokifanya ni sahihi.
Zahera amesema kamwe hatoweza kukaa kimya kwani kila anachokisema ni sahihi kwake na hataweza kufumbia macho madudu ya TFF.
Amefunguka kwa kusema kama TFF wanaona anakiuka taratibu wamfungie lakini hatoacha kuzungumza mpaka pale uongozi wa Shirikisho hilo utakapobadilika.
Baada ya Simba kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar kwa kuchapwa mabao 2-1, matokeo hayo yamefufua matumaini ya ubingwa kwa Yanga ambayo inaomba wapinzani wao hao wapoteze michezo zaidi
Aidha matokeo hayo yametoa taswira kuwa haitakuwa kazi rahisi kwa Simba kushinda michezo yote iliyobaki
Kama Yanga itashinda michezo yote sita iliyobaki itafikisha alama 92 huku wapinzani wao wakiwa na mzigo wa kupata matokeo kwenye michezo 14 ndani ya mwezi mmoja
Yanga imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imejikusanyia alama 74 ikifuatiwa na Azam Fc yenye alama 66
Simba ni ya tatu ikiwa na alama 60
Azam na Yanga zimeshuka dimbani mara 32 wakati Simba imeshuka dimbani mara 24
Simba inakabiliwa na ratiba ngumu ya michezo ya viporo ambapo katika kipindi cha siku 15 itashuka dimbani mara sita
Baada ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar, kikosi cha Simba kimeondoka leo Jumapili asubuhi mkoani Kagera kuelekea Mwanza tayari kwa michezo miwili ya viporo itakayopigwa jijini humo
Keshokutwa April 23 Simba itashuka uwanja wa CCM Kirumba kuchuana na Alliance Fc na siku mbili baadae, April 25 Simba itarejea kwenye uwanja huo kuchuana na KMC kisha kikosi cha mabingwa hao watetezi kitaelekea mkoani Mara kuikabili Biashara United April 28