
– Aston Villa imefanikiwa kupanda Ligi Kuu Nchini Uingereza “Premier League” Baada ya ushindi wa Magoli 2-1 dhidi ya Derby Country mapema siku ya jana, katika Mafanikio hayo waliyopata kwa Mara ya kwanza takribani miaka Mitatu kwa Kiasi kikubwa imechangiwa na Wachezaji kutoka Bara La Afrika.
.
– Mfungaji bora wao Tammy Abraham licha tu ya kuichezea timu ya taifa ya England U21 lakini Nigeria wameendelea kumshawishi kurejea nyumbani kabla ya kuanza kucheza Senior team Moja kwa Moja, Mshambuliaji Anwar El Ghazi licha tu ya kuichezea timu ya taifa ya Uholanzi U21 Morocco hawajaacha kumshawishi kurejea nyumbani, Beki na nahodha wa Misri, Ahmed Elmohamady, Albert Adomah wa Ghana wa Nyota wa Ivory Coast, Jonathan Kodjia wameisaidia Aston Villa kwa kiasi chake kuhakikisha imerejea Ligi Kuu… Baada ya wao kupanda wanahitimisha Timu tatu Baada ya Mbili kutangulia ambazo ni Norwich City na Sheffield United.
.
– Magoli kutoka Kwa, Anwar El Ghazi na John McGinn yaliweza kutosha na kuwapandisha PL vijana hao wa kocha Dean Smith katika Dimba la Wembley, Martin Waghorn aliwafuta machozi Derby kwa Goli lake Dakika 10 za Mwisho wa Mchezo huo..
#Updates
@Sokawaytz
credit: @sokawaytz


























